“Si kweli!”
“Huo ndiyo ukweli, au kama mmekuja na ukweli wenu mwingine,” alisema mzee Hamidu huku akisimama kwenye kiti, yote hayo ilikuwa ni kutaka kuwaonyeshea watu hao kwamba alikuwa mwanaume imara na kile alichokuwa akikisema ndicho kilikuwa sahihi.
“Hapana! Bado tunajua kwamba walipita hapa, ila walipitaje? Inawezekana wewe hufahamu lakini kuna mtu hapa atakuwa anafahamu,” alisema Gilbert.
“Kwa hiyo kuna mtu alichukua rushwa?”
“Huwezi kujua!”
“Hizo ni dharau,” alisema mzee huyo.
Gilbert hakutaka kubaki ndani ya ofisi hiyo, kwa jinsi mzee Hamidu alivyokuwa akiongea, alihisi moyo wake ukipatwa na hasira kali, na ili kuepusha matatizo, akaamua kutoka ndani ya ofisi ile.
Pale nje akasimama na kuanza kuangalia huku na kule, aliwaangalia jinsi ambavyo askari walivyokuwa wakipekua magari, alikuwa na uhakika kwamba watu hao walipita mahali hapo kwani hata upekuzi ambao ulikuwa ukifanyika, ulifanyika kizembe sana.
“Tuingieni nchini Tanzania, bado moyo wangu una uhakika kwamba watu hawa walipita mahali hapa,” alisema Gilbert, wakaingia ndani ya gari lao na kuingia nchini Tanzania, hapo wakaanza kuitafuta Tanga Mjini.
***
Kila kona katika Tanga Mjini kulikuwa na stori moja tu iliyokuwa ikianza kuzagaa kila kona. Wazungu watatu ambao walichukua chumba kimoja katika nyumba ya wageni iliwashangaza kila mtu aliyekuwa ameisikia.
Watu walijua kwamba Wazungu walikuwa miongoni mwa watu waliokuwa na pesa, watu ambao mara baada ya kufika barani Afrika basi wangekuwa wakiishi katika hoteli nzuri lakini Wazungu waliokuwa wameingia Tanga kwa siku hizo walionekana kuwa tofauti na wenzao kabisa.
Hali hiyo ikaanza kuwatia wasiwasi watu wa hapo Tanga kiasi kwamba wengi wakahisi kwamba kulikuwa na kitu cha siri kilichokuwa kikiendelea ambacho kingeweza kuwa hasara au hata kupoteza maisha kwa wakazi wa hapo.
Walichokifanya siku iliyofuata ni kuwasiliana na polisi. Waliwaambia kila kitu kilichokuwa kimetokea kwamba inawezekana kabisa Wazungu wale hawakuwa watu wazuri na ndiyo maana hawakutaka kupanga katika hoteli kubwa kwa kuogopa kukamatwa.
Polisi walipoambiwa, hawakutaka kusubiri, wakaondoka na kuelekea huko kwa lengo la kuwaona Wazungu hao. Walipofika, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuzungumza na mmiliki wa gesti hiyo na kumuuliza maswali mengi.
Hakuwaficha, aliwaambia kila kitu kuhusu Wazungu hao na hivyo kuhitaji kuzungumza nao. Hilo halikuwa tatizo, alichokifanya ni kuwaita, wanaume hao, wakatoka chumbani, wakafunga mlango kwa ufunguo ili Sharifa asitoke, wakawafuata polisi na kuanza kuzungumza nao.
Waliwaambia kwamba walifika hapo Tanga kwa lengo la kuingia katika mapango ya Amboni lakini kabla ya kwenda huko walijikuta wakiibiwa kiasi cha pesa walichokuwanacho cha dola elfu themanini, laptop na saa zao za mikononi na vijana wa mitaani ambao waliwafuata na kuwatolea visu.
“Poleni sana! Kwa nini hamkutoa taarifa polisi?” aliuliza polisi mmoja, kwa jinsi Tim alivyokuwa akielezea, ilikuwa ni vigumu kuamini kwamba alikuwa akidanganya.
“Tulichanganyikiwa! Hatupo sawa, hata nauli ya ndege kurudi nyumbani hatujui tutaipataje, hapa mnapotuoni, tupo hivihivi pamoja na msichana wa nchini Ghana ambaye tumekuja naye, hatuna kitu,” alisema Tim.
Polisi wakaangaliana, kile alichokuwa amekisema kilionekana kuwagusa kupita kawaida hivyo kuwaambia kwamba wanaondoka na kurudi baadaye huku wakiwa tayari wamejua ni kitu gani walitakiwa kufanya kuwasaidia Wazungu hao.
Walipoona polisi wameondoka, hawakutaka kuendelea kukaa kwenye gesti hiyo, ilikuwa ni lazima waondoke kwani walihisi kwamba mara baada ya kuondoka, wangekwenda kupata ukweli wa wao kuwa hapo na kurudi huku wakiwa na sura nyingine.
Wakaufungua mlango na ufunguo, wakaingia ndani, kilichowashtua ni kwamba Sharifa hakuwemo chumbani humo. Hilo liliwatia hofu kwani walipokwenda nje kuzungumza na polisi walimuacha humo ndani na zaidi ni kwamba waliufunga mlango kwa ufunguo, sasa kama ameondoka, atakuwa amepitia wapi?
“Kwenye dari! Tuangalieni kwenye dari,” alisema Adson na kwa kuwa pale kulipokuwa na mlango wa dari kulikuwa na meza, wakajua kabisa msichana huyo alipanda juu ya meza hiyo na kuingia humo kwa lengo la kuwatoroka hotelini humo.
“Jamani! Ili tuwe salama, huyu msichana ni lazima apatikane,” alisema Kelly, wakautoa mlango wa dari na Tim kuingia huko kumtafuta Sharifa.
***
Sharifa alikuwa ndani ya chumba kile huku akiwa na wasiwasi tele, hakujua ni kitu gani kingeendelea kama tu watu hao wangeendelea kumshikilia kama ilivyokuwa.
Hakutaka kuona akiwa mikononi mwa watu hao, alitamani kuona akiondoka na kurudi kwa mpenzi wake. Kama kulia, alilia sana lakini muda huo haukuwa wa kulia tena, ilikuwa ni lazima kufanya kila liwezekanalo kuondoka ndani ya chumba hicho.
Alikuwa humo, Tim na wenzake walikwenda nje walipokuwa wakihitajika na polisi, yeye mule ndani ilikuwa ni lazima afanye kila linalowezekana kuhakikisha anatoka ndani ya chumba hicho.
Akaufuata mlango, akakishika kitasa na taratibu kuanza kukitekenya kwa lengo la kukifungua. Mlango haukufunguka kuonyesha kwamba ulifungwa kwa nje.
Haraka sana akaacha. Akaangalia huku na kule, akafanikiwa kuuona mlango wa dari ukiwa umefungwa. Kichwa chake kikamwambia kwamba hiyo ndiyo ilikuwa njia pekee ya kuweza kuondoka ndani ya chumba hicho.
Akachukua meza, akaiweka chini ya mlango wa dari na kupanda, akaanza kuufungua mlango huo kwa kuusukuma, ukafanikiwa kufunguka.
Kazi kubwa ilikuwa ni kupanda juu ya dari. Ilikuwa ni kazi ngumu ambayo aliamini kwamba asingeweza kuifanya hata kidogo lakini kitu cha kushangaza kabisa ambacho hata yeye kilimwachia maswali ni kwa namna ambavyo alipanda na kuingia darini, akaurudishia mlango ule wa dari.
Ndani kulikuwa na giza, hakuwa na simu, hakuwa na kitu chochote kile ambacho kingemfanya kumulika mule ndani lakini hilo halikumfanya kubaki mahali pale, kwa kutumia magoti yake akaanza kusonga mbele, sehemu ambayo aliamini kulikuwa na mlango mwingine.
Humo darini, alisikia milio ya panya, hakuoga hata kidogo, kitu alichokuwa akikimbia kilikuwa ni hatari hata zaidi ya panya aliokuwa akiwasikia. Baada ya dakika mbili akafika katika mlango mwingine wa dari na kuufungua.
“Mungu nisaidie,” alisema huku akiangalia ndani ya chumba hicho.
Alisikia sauti za watu wakiongea bafuni kwa furaha, hakutaka kujiuliza kuhusu watu hao, akahisi kabisa kwamba walikuwa wapenzi waliokwenda kuyafurahia maisha yao na muda huo walikuwa wakioga tayari kwa kuondoka.
Bahati ilikuwa upande wake kwani pale kulipokuwa na mlango wa dari kulikuwa na kitanda, haraka sana akaruka mpaka juu ya kitanda.
Akaondoka na kuufuata mlango, akaufungua na kuanza kuangalia nje. Alipoona koridoni hakuna mtu, hakutaka kusubiri, hara sana akatoka na kuelekea nyuma ya gesti hiyo na kuanza kukimbia.
Mule ndani, Tim aliendelea kutambaa ndani ya dari na kufanikiwa kuuona mlango wa kushukua katika chumba kingine. Haraka sana akaufuata, haukuwa umefungwa hivyo akarukia ndani ya chumba hicho.
“She was passing through this room,” (amepitia chumba hiki) alisema Tim na kuufungua mlango na kutoka ndani.
Kichwa chake kilimwambia kwamba msichana huyo alikuwa ameondoka kupitia katika mlango wa nyuma na hivyo kuanza kukimbilia huko.
Alichanganyikiwa, msichana huyo alikuwa mtu muhimu mno, aliwafanya kufika nchini Kenya, wakatoroka mpaka Tanzania na walikuwa wamelipwa kiasi kikubwa cha pesa kwa ajili ya kuhakikisha mpenzi wa msichana huyo, Bruno haondoki kuelekea nchini Marekani.
Kule nje aliwakuta watu wakiwa wamepigwa na taharuki, kilichokuja kichwani mwake ni kwamba walimuona Sharifa akiwa amekimbia na hawakujua sababu iliyomfanya kukimbia na ndiyo maana walikuwa kwenye hali hiyo.
Akaanza kuelekea katika njia iliyokuwa na watu wengi waliokuwa wamesimama kwa kuamini kwamba msichana huyo alipitia njia hiyo. Watu wote wakaanza kumwangalia na yeye, ni kweli walimuona msichana mmoja akiwa amekimbia lakini ghafla, baada ya sekunde kadhaa wakamuona mwanaume wa Kizungu naye akikimbia kuelekea kule alipokimbilia mwanamke yule.
“Jamani! Kuna nini tena?” aliuliza jamaa mmoja aliyekuwa amevaa msuli kama mtu aliyekuwa na busha.
“Hata mimi nashangaa! Hawa watoto wetu siku hizi wana visa sana, utakuta huyo Mzungu kamtoa Instagram halafu anamkimbia,” alisema mzee mwingine.
Tim alikimbia mpaka katika barabara kuu kabisa lakini hakuweza kumuona Sharifa. Alichanganyikiwa, kwa wakati huo msichana huyo alikuwa muhimu kuliko kitu chochote kile.
Akamtafuta na alipoona hajafanikiwa, akarudi kule gesti na kuwaambia wenzake kile kilichotokea. Kila mmoja alichanganyikiwa, kitendo cha kumkosa msichana huyo kilimaanisha kwamba Bruno angekwenda nchini Marekani na kuweka ushahidi juu ya kile kilichokuwa kimetokea.
“Ni lazima tuondoke kurudi Marekani haraka sana,” alisema Tim huku akiwaangalia wenzake, yeye alionyesha kuchanganyikiwa zaidi ya wenzake.
“Tukiulizwa?”
“Tunakwenda kimyakimya!”
“Halafu?”
“Huyu mtu tutamvizia uwanja wa ndege, najua tutajua siku ambayo atakwenda nchini Marekani, nadhani hapo ndipo tutakapofanya utekaji hukohuko mbele ya safari! Mnaonaje?” alisema na kuuliza.
“Linaingia akilini! Hakuna kuchelewa, kama vipi kesho tuondokeni,” alisema Kelly.
Hivyo ndivyo walivyokubaliana, hakukuwa na sababu ya kuendelea kubaki nchini Kenya na wakati kulikuwa na kazi kubwa ambayo walitakiwa kuifanya haraka iwezekanavyo.
Usiku huohuo wakaondoka na kuelekea katika hoteli ya kifahari ya Jumanji iliyokuwa Tanga Mjini na kuchukua vyumba hapo. Siku iliyofuata, wakapanda ndege na kuelekea Dar es Salaam ambapo huko wakaunganisha mpaka nchini Marekani.
Ndani ya ndege kila mmoja alikuwa akifikiria lake, mbele yao kulionekana kuwa na kazi kubwa lakini ilikuwa ni lazima kuhakikisha wanaikamilisha kwa haraka sana.
Hawakutaka kuzungumza mambo mengi kuhusu jambo hilo ila walipanga kuzungumzia zaidi mara baada ya kufika nchini humo.
Baada ya saa ishirini na tano, wakaingia nchini humo. Wakafikia hotelini, hawakutaka kuwasiliana na Maxwell, walitaka kukamilisha kila kitu haraka sana pasipo mwanaume huyo kufahamu jambo lolote lile.
Wakajipanga na baada ya siku tatu tangu wafike nchini Marekani wakapata taarifa kwamba Bruno alikuwa njiani akielekea nchini Marekani. Kwa kuwa walitakiwa kukamilisha mpango wao haraka sana, wakajipanga kwa kwenda uwanja wa ndege na kufanya uchunguzi ili wagundue ni ndege ipi ambayo ingemfikisha hapo nchini Marekani.
Wakapewa taarifa kwamba Bruno alipanda ndege ya Shirika la American Airlines na angeingia mahali hapo majira ya saa 05:43 usiku, hivyo walitakiwa kusubiri.
***
Gilbert na wenzake waliingia nchini Tanzania katika jiji la Tanga na kuanza kufanya upelelezi kugundua kile kilichokuwa kikiendelea. Walianza kuzunguka katika vituo vya polisi kwa lengo la kupata ukweli juu ya kile kilichokuwa kikiendelea.
Huko, wakaambiwa kwamba hakukuwa na taarifa yoyote ile juu ya mtu waliyekuwa wakimtafuta lakini kama wangewapa muda, basi bila shaka wangejua kila kitu kilichokuwa kikiendelea.
Japokuwa walikuwa katika kituo kikuu cha Tanga, wakaondoka na kuelekea katika vituo vingine vidogo, walikuwa na uhakika kwamba kama Sharifa alikuwa amepelekwa nchini humo basi ilikuwa ni lazima kupatikana hata kama kungetokea jambo gani.
Huko, wakapewa taarifa kuhusu Wazungu waliokuwa wamefika hapo Tanga na kuchukua chumba katika gesti moja ya uchochoroni ambapo huko walionekana wakiwa na mwanamke mmoja kutoka nchini Ghana.
“Mwanamke kutoka nchini Ghana?” aliuliza Gilbert.
“Ndiyo!”
“Ulimuona huyo mwanamke?”
“Hapana! Ila tuliambiwa na mwenye gesti kwamba walikuwa watalii,” alisema polisi aliyekuwa akijibu maswali kwa niaba ya mkuu wa kituo ambaye hakuwa mahali hapo.
Hapo hakukuonekana kuwa msaada tena, wakahisi kabisa kwamba watu hao ambao waliambiwa kuhusu stori zao na kwamba walikuwa na mwanamke kutoka nchini Ghana iliwezekana kabisa wakawa watu waliokuwa wakiwatafuta, wakaelekea katika gesti hiyo huku wakisindikizwa na polisi, walipofika, wakaingia ndani.
Wakakutana na mhudumu na kumuuliza kuhusu Wazungu hao, aliwaambia kwamba walikuwa ndani hivyo kwenda katika chumba walichokuwa wamechukua huku Gilbert na wenzake wakiwa na bastola mikononi mwao kwa ajili ya jambo lolote baya lile ambalo lingetokea huko.
Walipokifikia chumba, wakaufungua mlango na kuingia ndani huku wakiwa na bastola zao. Walipofika, hakukuwa na mtu yeyote yule, Wazungu wale ambao waliambiwa kwamba walikuwa humo na mwanamke mmoja, hakukuwa na yeyote yule, chumba kilikuwa kitupu kabisa.
“Wapo wapi?” aliuliza polisi.
“Mmh! Walikuwa humu! Sijui wapo wapi!” alisema jamaa mwenye gesti.
Wakatoka kwa kuhisi kwamba watu hao walikuwa wamekwenda sehemu fulani hivyo walitakiwa kuwawahi. Nje, kila kona hawakufanikiwa kuwaona watu hao zaidi ya wananchi kuwashangaa tu kwani kwa tukio lililokuwa likitokea siku hiyo kila mtu lilimshangaza kwani haikuwa na kawaida kwa Wazungu kuwa katika hali kama waliyokuwa wale wa mwanzo na hata hao wa kipindi hicho.
“Wametoroka! Wamekwenda naye wapi?” aliuliza Gilbert, kwa kumwangalia tu usoni alionekana kuwa na hasira kupita kawaida.
***
Sharifa alikuwa akikimbia huku akiangalia nyuma, kila mtu aliyekuwa akipishana naye alimshangaa, hawakujua kitu kilichokuwa kimetokea mpaka msichana huyo kukimbia huku akionekana kuwa na hofu kubwa.
Alikimbia mpaka alipofika mahali kulipokuwa na nyumba nyingi zilizokuwa milango wazi, hakutaka kuendelea kukimbia tu kwa kuona kwamba angekamatwa kwa kuwa hakuwa na kasi, hivyo akaingia ndani ya nyumba moja na kuomba msaada.
Watu walikuwa vyumbani mwake, wakatoka na kumwangalia Sharifa aliyekuwa ukumbini, aliwaambia watu hao kwamba alihitaji msaada kwa kuwa alikuwa akikimbizwa.
Wakati akiwa hapo ukumbini, akamuona Tim akipita nje kwa kasi huku akikimbia, Sharifa akajificha kwani hakutaka kuonekana na mwanaume huyo. Watu wote wakabaki wakimshangaa, kwao, alionekana kama mtu aliyekuwa na matatizo fulani, yaani kama changudoa aliyemkimbia mteja gesti.
“Bibie vipi?” aliuliza mwanamke mmoja.
“Kuna mtu ananikimbiza anataka kuniua,” alisema Sharifa huku akiangalia huku na kule, kwa kifupi alikuwa na wasiwasi.
Kwa lafudhi yake tu, kwa jinsi alivyokiongea Kiswahili chake hakukuwa na swali kwamba msichana huyo alikuwa Mkenya. Mwanamke mmoja akamchukua na kumuingiza chumbani mwake na kumuuliza tatizo alilokuwanalo ambapo akaanza kumwambia kila kitu kilichotokea.
Alishangaa, hakuamini kama kweli kungekuwa na watu ambao wangetoka nchini Marekani mpaka Kenya kwa lengo la kumteka mtu fulani, haikumuingia akilini, wakati mwingine aliona kama alikuwa akidanganywa na msichana huyo lakini akaamua kukubaliana naye.
“Nikusaidie nini?” aliuliza mwanamke huyo baada ya kusikiliza maneno ya Sharifa.
“Nataka kuwasiliana na mume wangu! Naomba unisaidie,” alisema.
Hilo halikuwa tatizo hata kidogo, akampa simu na msichana huyo kumpigia Bruno aliyekuwa nchini Kenya, baada ya sekunde kadhaa alikuwa akiongea naye.
Alimwambia mahali alipokuwa, Bruno aliposikia hivyo, alichanganyikiwa, hakuamini kama mpenzi wake alitoroka mikononi mwa watu hao na hivyo kuanza safari ya kuelekea Tanga.
Hakuwa akienda peke yake, aliwasiliana na polisi na kuwaambia kila kitu kilichotokea kwamba mpenzi wake alikuwa salama kabisa nchini Kenya hivyo alitakiwa kwenda huko na kumchukua.
Njiani, Bruno alikuwa na presha kubwa, moyo wake ulikuwa umekwishakata tamaa na alihisi kabisa kwamba huo ungekuwa mwisho wa kumuona mpenzi wake huyo akiwa mzima, kitendo cha kumwambia kwamba aliwatoroka watu wale kilimfanya kuwa na furaha kupita kawaida.
“Ila kawatoroka kweli au wanamtumia ili kunipata mimi?” alijiuliza Bruno, upande wake mwingine ulionekana kuwa na wasiwasi.
“Haiwezekani! Kama ingekuwa wanamtumia, wangemwambia aniambie niende peke yangu,” alijijibu.
Polisi hao wa Kenya walichokifanya ni kuwasiliana na polisi wa Tanzania kupitia Interpol na kuwaambia kile kilichokuwa kikiendelea.
Wao, yaani polisi wa Tanzania walitakiwa kwenda mahali alipokuwa Sharifa na kumchukua lakini baada ya Bruno kuambiwa hivyo, hakutaka kabisa hilo litokee, alichohitaji ni kwenda yeye mwenye mpaka alipokuwa mpenzi wake na kumchukua.
Baada ya saa kadhaa, wakafika Tanga. Akampigia simu Sharifa ambaye alimpa mwenyeji na kumuelekeza mahali nyumba yake ilipokuwa. Kutoka hapo walipokuwa mpaka kulipokuwa na nyumba hiyo hakukuwa mbali sana kwani ni mwendo wa dakika ishirini kwa gari wakawa wamekwishafika.
Wakamkuta mwenye nyumba nje, wakamfuata na yeye kuanza kuwapeleka ndani ambapo huko Bruno akakutana na Sharifa, kwa furaha aliyokuwanayo, akamsogelea na kumkumbatia.
“Walitaka kuniua,” alisema Sharifa huku akilia, alikuwa amekumbatiana na Bruno tu.
“Wasingeweza. Nipo pamoja na wewe, kukumaliza wewe inamaanisha walihitaji vita na mimi,” alisema Bruno huku akiwa amemkumbatia mpenzi wake huyo.
Wakamchukua na kuanza safari ya kurudi Mombasa. Njiani, kila mmoja alionekana kuwa na furaha, mioyo yao ilifurahia kuungana tena kwa mara nyingine tena.
Baada ya saa kadhaa wakafika Mombasa ambapo huko, kitu cha kwanza kilikuwa ni kwa Bruno kuwasiliana na akina Gilbert na kuwaambia kile kilichotokea na hivyo kukutana na kuzungumza.
Wao wenyewe walifurahi lakini bado walionekana kuwa na hofu na usalama wa maisha ya Bruno. Walijua kabisa kwamba kama lengo la kumteka Sharifa lilikuwa ni kuhakikisha kwamba Bruno haendi nchini Marekani basi ingekuwa ni lazima watu hao wafanye jambo lolote lile kuhakikisha mwanaume huyo hatoi ushahidi katika kesi hiyo.
“This is not the end,” (huu si mwisho) alisema Gilbert huku akimwangalia Bruno.
“What do you mean,” (unamaanisha nini?)
“They are going to look for you,” (watakutafuta)
“And kill me?” (na kuniua?)
“That what they want. Bruno, we have to take you to USA by ourselves,” (Hicho ndicho wanachokitaka. Bruno, tutakupeleka Marekani sisi wenyewe) alisema Gilbert.
Hicho walichokifanya, baada ya siku mbili wakaanza safari ya kuelekea nchini Marekani. Kwa kuwa walikuwa na uhitaji wa kuwapata watu hao, hawakutaka kujionyesha, ilikuwa ni lazima na wao wajifanye abiria ili iwe rahisi kwao kufanikiwa kwa kile walichokuwa wakikitaka.
Ndege ilichukua saa zaidi ya ishirini angani na ndipo ikaanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JFK. Abiria wakaanza kuteremka akiwemo Bruno. Walitembea kwa mwendo wa taratibu kuufuata mlango uliokuwa ukielekea katika jengo la uwanja huo.
Hakuonekana kuwa na hofu hata kidogo, alijiamini mpaka alipochukua begi lake lililokuwa limechunguzwa na kuanza kutoka nje ya jengo lile.
Alipofika, harakaharaka mwanaume mmoja akamfuata na kumwambia kwamba alikuwa dereva teksi ambaye alitumwa na mwanaume aliyeitwa Todd kwa lengo la kumpokea.
“Alikuagiza?” aliuliza Bruno.
“Ndiyo! Au nimekuchanganya?”
“Ni mimi! Nilidhani ungekuwa na bango lililokuwa na jina langu,” alisema Bruno huku akiachia tabasamu pana.
“Hapana! Alinionyeshea picha yako. Karibu,” alisema mwanaume huyo huku akimpa mkono, wakaanza kuifuata teksi iliyokuwa maeneo hayo.
Bruno akaingia ndani ya teksi ile, hakuonekana kuwa na hofu hata kidogo, aliamini maneno aliyoongea mwanaume yule kwamba alitumwa na mzee Todd kwenda kumchukua hapo uwanjani.
“Ni mara yako ya kwanza kufika hapa?” aliuliza mwanaume huyo.
“Ndiyo! Ni mara yangu ya kwanza, nimekuja kutoa ushahidi kwenye kesi yake kisha nitarudi Kenya,” alijibu huku tabasamu likiwa usoni mwake.
“Ooh! Sawasawa! Nadhani atafurahi sana akisikia umefika salama,” alisema dereva, safari ikawa inaendelea kama kawaida.
***
Tim na wenzake wakajipanga vilivyo, ilikuwa ni lazima Bruno atekwe uwanjani na kupelekwa sehemu kwa lengo la kuuawa na kisha mwili wao kuutupa.
Hilo likapangwa na hivyo kuanza kumtafuta dereva ambaye walimwambia kuwa ingekuwa vizuri kama angekwenda uwanjani hapo na kumchukua Bruno na kujifanya kwamba alikuwa ametumwa.
Siku ilipofika, Tim akaenda na dereva huyo mpaka uwanja wa ndege, akachukua namba yake ya simu na wakati abiria wanatoka ndani ya jengo la uwanja huo, alikuwa akizungumza naye na alipomuona Bruno, akamwambia kwamba alikuwa mwenyewe na ndipo dereva huyo alipoanza kumfuata.
Alifuatilia kila hatua mpaka alipoingia ndani ya teksi na kuanza safari ya kuondoka mahali hapo. Mipango yao ilikuwa ni kwenda katika jengo moja lililokuwa hapohapo New York.
Hawakuchukua muda mrefu, wakafika, dereva akasimamisha gari, hapohapo akateremka na Kelly na mwenzake, Adson kutokea na kuanza kuifuata teksi ile, walipoifikia, wakaufungua mlango na kumtoa kwenye gari.
“What is going on?” (nini kinaendelea?) aliuliza Bruno huku akionekana kushangaa.
“Shiiiiiiiiii!” alimnyamazisha Kelly huku akiwa na kipande cha nondo mkononi mwake.
Wakambeba na kuondoka naye, wakamuingiza ndani ya jumba hilo, kitu kilichokuwa kikitakiwa kufanywa haraka ni kumuua na kisha kuuacha mwili wake hapohapo na wao kuondoka.
“Don’t kill me, please,” (tafadhai, msiniue) alisema Bruno lakini hakukuwa na mtu aliyejali, kila mmoja alichokuwa akikihitaji mahali hapo ni kuona mwanaume huyo akifa haraka sana.
***
Gilbert na wenzake walikuwa wakifuatilia kila kitu, waliteremka kutoka ndani ya ndege huku wakimwangalia Bruno, walikuwa makini naye na waliamini kwamba kwa namna moja ama nyingine ilikuwa ni lazima watu wamfuatilie kwa sababu kile alichokuwa akienda kukifanya nchini Marekani kilionekana kuwa kitu hatari.
Waliingia ndani ya jengo la uwanjani hapo huku wakiwa pamoja naye, walijifanya abiria na ilikuwa vigumu kwa watu wengine kugundua kwamba watu hao walikuwa pamoja kwani walijitenga naye kupita kawaida.
Walipofika nje, wakamuona akiongea na dereva teksi, kwa jinsi walivyoongea, walionekana kama watu waliokuwa wakifahamiana, akaambiwa aingie ndani ya gari, akafanya hivyo.
Gilbert na wenzake hawakutaka kuchelewa, walikuwa na uhakika kabisa kwamba dereva teksi yule alikuwa ametumwa hivyo kuanza kuifuatilia teksi ile.
Walikuwanayo kwa umakini kabisa, hawakutakiwa kuwa na presha yoyote ile, ila walitakiwa kuwa makini kwa kuwa kama wangekosea hatua moja basi Bruno angeweza kuuawa.
Waliifuatilia teksi ile mpaka ikafika mahali fulani, nje ya nyumba moja, kwa jinsi walivyoangalia huku na kule, haikuwa vigumu kugundua kwamba eneo hilo lilikuwa la hatari sana, wakazima taa za gari lao na kisha kulisimamisha kwa mbali kidogo huku macho yao yakiwa katika teksi ile iliyokuwa imesimama.
“Tufanye nini? Tupige risasi?” aliuliza Putt.
“Hapana! Subiri kwanza!” alisema Gilbert.
Hapohapo wakamuona Kelly akielekea ilipokuwa teksi ile, akaufungua mlango huku akiwa na kipande cha nondo. Hakuwa peke yake, alikuwa na Adson ambapo wakambeba Bruno na kuingia naye ndani ya jumba lile.
“Tuwafuate?” aliuliza Bull.
Wakati wakiwa wamejiandaa, wakashtuka kuliona gari jingine likifika mahali hapo, mlango ukafunguliwa na mwanaume mmoja kuteremka.
Alikuwa Tim ambaye alikwenda uwanja wa ndege kuhakikisha kwamba Bruno anakamatwa. Alipofika maeneo yale, akasimamisha gari na kuteremka, naye akaingia ndani ya jumba lile.
Haraka sana Gilbert na wenzake wakateremka na kuanza kuelekea lilipokuwa jumba lile. Walikuwa na bastola mikononi mwao ili kuhakikisha wanafanya mauaji pale ambapo ingewabidi kufanya hivyo.
Walipofika katika dirisha la jumba lile wakaanza kuchungulia ndani. Wakawaona vijana wale wakiwa wamemuweka Bruno chini tayari kwa kuanza kumpiga.
Hawakuwa na bunduki, kama kumuua ilikuwa ni lazima wafanye hivyo kwa kutumia vipande vya nondo walivyokuwanavyo.
Kilichotokea ni kuanza kumshambulia Bruno na vipande vya nondo walivyokuwanavyo. Gilbert na wenzake walikuwa wakiangalia na kila walipotaka kuingia, Gilbert alikuwa akiwazuia kwa kuwaambia kwamba hawakutakiwa kuwa na presha hata kidogo.
“Watamuua!” alisema Putt huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Tunakusanya ushahidi, subiri!”
“Tunakusanya ushahidi?”
“Ndiyo! Subiri!”
Bruno alizidi kupigwa na vipande vya nondo ile mpaka akawaida hoi. Wakati wakijiandaa kummalizia, haraka sana Gilbert akanyoosha mkono wake uliokuwa na bastola, zilitoka risasi tatu mfululizo, kila mtu akapigwa, wakaanguka chini.
Gilbert na wenzake wakatoka kule walipokuwa na kuingia ndani, wakawafuata wanaume wale, wote watatu walikuwa chini wakiugulia maumivu, Gilbert hakutaka kuchelewa, hapohapo akawapiga risasi za vichwa Adson na Tim kisha kumuacha Kelly akiwa peke yake huku akiugulia maumivu.
Wakamshika Bruno pale alipokuwa, alikuwa amepasuliwa, alipigwa vibaya, hawakutaka kumuacha, wakamchukua na kumpeleka ndani ya gari huku wakiwapigia simu polisi na kuwaambia kwamba walitakiwa kuelekea katika jumba lile kuchukua maiti za waharifu ambao waliwashambulia kwa risasi.
“Na huyu?” aliuliza Putt huku akimaanisha Kelly.
“Tunaondoka naye!”
Japokuwa alikuwa na maumivu makali, hawakutaka kujali, walimchukua kwa kumshika hovyohovyo mpaka ndani ya gari na kuliondoa mahali hapo.
Njiani Kelly alikuwa akilia, alisikia maumivu makali katika paja lake la kulia, damu zilikuwa zikimtoka lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyejali. Walimchukua mpaka hospitalini na kumtaka kutibiwa huku akiwa chini ya ulinzi mkali.
Kwanza risasi ikatolewa na kuendelea na matibabu mengine. Wakati huo, pia Bruno alichukuliwa na kupelekwa katika chumba kingine na madaktari kuambiwa kwamba walitakiwa kuhakikisha mwanaume huyo anapona haraka iwezekanavyo kwa kuwa walikuwa na kazi naye.
Wakati hayo yote yakiendelea, mzee Todd alikuwa selo, kama kawaida yake alikuwa akilia mno, moyo wake ulimuuma kwa kuwa aliona kama Bruno alimsaliti kwa kile kilichokuwa kikiendelea.
Hakupokea taarifa yoyote ile, moyo wake uliumia kwani miongoni mwa watu aliokuwa akiwaamini alikuwa Bruno, na yote hiyo ni kwa sababu alikuwa naye kwa kipindi kirefu na hata kumpa kiasi kikubwa cha pesa.
Siku zikaendelea kukatika, baada ya siku ya kusikiliza tena kesi hiyo kwa upande wa mashahidi ilipofika, Bruno akachukuliwa na kupelekwa mahakamani huku akiwa amefungwa bandeji katika sehemu kubwa kichwani mwake kwani alikuwa amejeruhiwa mno.
Watu wengi hawakujua sababu ya mwanaume huyo kufika mahakamani, wengi walihisi kwamba inawezekana alikuwa na kesi kama watuhumiwa wengine ambao walikuwa wakifika hapo huku wakiwa wamejeruhiwa.
Baada ya dakika kadhaa, gari lilobeba watuhumiwa ambao walitakiwa kusimama kizimbani na kujibu mashtaka yao wakafika mahali hapo.
Haraka sana waandishi wa habari wakaanza kusogea na kuanza kupiga picha. Mtu waliyekuwa wakimtaka alikuwa mzee Todd, waliihitaji picha yake mno kwa kuwa ndiye mtu aliyekuwa akijulikana kuliko wote ambao walikuwa wakifikishwa mahakamani katika kipindi hicho.
Kwa kumwangalia tu isingekuwa vigumu kugundua kwamba moyo wake ulivunjika nguvu, mwili wake ulipungua kwa sababu ya kuwa na mawazo mengi. Alikuwa akiifikiria familia yake lakini pia aliifikiria kesi hiyo ambayo ilikuwa ikimuelemea.
Akaingia ndani, akawekwa katika kiti kimoja na kuambiwa kutulia hapo. Hakujua kama Bruno alikuwemo mahakamani, alichohisi ni kwamba alikuwa amesalitiwa na mwanaume huyo.
Wakili wake alikuwa mbele kabisa, yeye mwenyewe alionekana kuwa na hofu moyoni mwake, kila alivyokuwa akiiangalia kesi ile alikuwa na uhakika kwamba mteja wake angeshindwa kesi ile.
CIA walifanya kila kitu kwa siri kubwa, hakukuwa na mtu aliyetakiwa kujua kilichokuwa kikiendelea kuhusu mashahidi kwani walimficha Bruno kwa nguvu zote na ndiyo maana hata mzee Todd hakuambiwa kitu chochote kile, alitakiwa kumuona Bruno kwa kushtukiza mahakamani hapo.
Hakimu alipokuwa akiingia, watu wote wakasimama kama kumpa heshima na alipokaa, wakakaa na kutulia. Kesi ikaanza, kama kawaida ikaanza kusomwa kwa dakika chache, ilipoanzia mpaka siku hiyo ambapo mashahidi walitakiwa kusimama na kusema kile kilichokuwa kimetokea.
“Shahidi namba moja anaitwa Bruno,” alisema hakimu, mzee Todd akashtuka kulisikia jina hilo, alikuwa ameinama, akauinua uso wake.
Akamuona mwanaume mmoja akisimama na kuanza kuelekea kizimbani, kwa kumwangalia tu ilikuwa ni rahisi kugundua kwamba alikuwa kwenye maumivu makali, alitembea kwa msaada wa Gilbert ambaye alikuwa pembeni yake na kumpeleka mpaka kizimbani.
Kila mtu aliyekuwa mahali pale alikuwa akishangaa, hawakumjua mwanaume huyo, alikuwa amezungushiwa bandeji, na kwa usoni yalionekana macho tu kwani alikuwa amejeruhiwa vibaya.
Akanyoosha mkono wake wa kulia na kisha kujitambulisha na kuiambia mahakama kwamba kila kitu ambacho angekwenda kukizungumza mahali hapo kilikuwa cha kweli kabisa na asingezungumza uongo hata kidogo.
“Naitwa Bruno Mike Onyambe!” alijitambulisha na mahakama kuanza kusikiliza ushahidi wake.
Alianza kusimulia kila kitu baada ya yeye kutoswa ndani ya maji na baadaye kuokolewa na watu waliokuwa katika meli ambayo aliikumbuka kwa jina lake, iliitwa Britannian Cargo P56 kwani iliiandikwa ubavuni.
Mule ndani, akaepelekwa ndani ya chumba ambacho akakutana na mzee huyo akiwa amefungwa huko na hivyo kuanza kuzungumza.
Hakutaka kuishia hapo, alisimulia kila kitu mpaka mzee huyo alivyokuwa akitafutwa na vijana ambao walipokea maelekezo kutoka nchini Marekani na hata wakati familia yake ilipokuwa ikiuawa, walikuwa Afrika Kusini na waliiona taarifa hiyo kwenye televisheni.
“Hakukuwa na kipindi kigumu kwa mzee Todd kama kipindi hicho. Alilia sana, hakuamini alichokuwa akikiona, iliniumiza sana moyoni mwangu, kwa nilivyokuwa nikimwangalia, niliyaona mapenzi yake makubwa aliyokuwanayo kwa familia yake. Mara nyingi aliniambia kitu kimoja tu kwamba kuna mtu anaitwa Maxwell ndiye aliyekuwa amesababisha yote hayo, alitaka kumuona akiingia gerezani ili afanye biashara zake kwa uhuru zaidi,” alisema Bruno, mahakama nzima ilikuwa kimya.
Alitumia dakika arobaini na tano, alipomaliza, akashuka kizimbani. Mzee Bruno alikuwa akilia, hakuamini kilichokuwa kikitokea. Ushahidi wa Bruno ulimkumbusha mbali kabisa, ulimkumbusha familia yake na mateso makubwa aliyoyapata alivyokuwa ndani ya meli.
Alipomaliza, akanyamaza. Akaanza kuulizwa maswali kutoka upande wa jamhuri na kila alipokuwa akiulizwa, alijibu kama ilivyokuwa ikitakiwa.
Alipomaliza, akateremka na kisha hakimu kusema kwamba kulikuwa na ushahidi kutoka CIA ambao ulikuwa ni wa kina kwa kuwa ulifuatiliwa kwa hatua zote.
Akaanza kuusoma ushahidi huo ambao ulieleza mambo mengi kuhusu mchezo ulivyokuwa na moja kwa moja ulikuwa ukimuweka hatihani mzee Maxwell.
“Vijana walifuatilia kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Ni kweli mzee Maxwell alikwenda Afrika, alipofika huko, akatekwa na kuingizwa katika meli iitwayo Britannian Cargo P56 ambayo ina usajili wa jina la Maxwell anayemiliki kampuni kadhaa nchini Marekani,” ulisema sehemu ya ushahidi huo na kuendelea:
“Nchini Afrika Kusini kulikuwa na kijana aliyekuwa akishirikiana naye, huyu aliitwa Xuso ambaye aliuawa siku chache zilizopita. Pale bandarini, Pretoria ndipo alipotaka kumalizia kazi yake kwani aliamini kuwa endapo angemuua Todd pale ingekuwa ni rahisi kwao kuupoteza mwili huo kwa kuwa walikuwa na watu wengi.”
“Walifanikiwa kwa kila kitu. Baadaye baada ya kugundua kwamba mzee Todd amekamatwa, alichokitaka ni kupoteza mashahid, hapa tunapoongea, kijana ambaye alikuwa karibu na Todd, Innocent, ameuawa na tulivyofuatilia tukagundua kwamba kijana huyo alianza kuweka ukaribu na Maxwell na alihusika katika kuweka madawa ya kulevya ndani ya nyumba ya Todd.”
“Yeye alifanikisha kutekwa kwa familia ya Todd, alihakikisha anashirikiana nao kwa ukaribu lakini waliposikia kwamba naye alitakiwa kuwa shahidi, wakamuua na mwili wake kuutupa baharini.”
“Bruno ambaye ni raia wa Kenya alipitia vikwazo vingi. Kwanza hakutakiwa kufika Marekani kwa kuwa Maxwell alijua kwamba mtu huyu alikuwa mwiba hatari sana. Wakamteka mchumba wake ili baadaye atishwe kwamba angeuawa kama tu angekanyaga nchini Marekani, bahati nzuri baadaye msichana yule alitoroka walipofika nchini Tanzania.”
“Hiyo haikutosha, wakapanga mipango wamteke uwanjani, walifanikiwa ila kwa kuwa maofisa wetu ni watu hatari, walifanikiwa kumuokoa katika mikono yao na kuwaua vijana wawili na kumbakiza mmoja,” ulisema sehemu ya ushahidi huo.
***
Gilbert na wenzake walikuwa wakifuatilia kila kitu, waliteremka kutoka ndani ya ndege huku wakimwangalia Bruno, walikuwa makini naye na waliamini kwamba kwa namna moja ama nyingine ilikuwa ni lazima watu wamfuatilie kwa sababu kile alichokuwa akienda kukifanya nchini Marekani kilionekana kuwa kitu hatari.
Waliingia ndani ya jengo la uwanjani hapo huku wakiwa pamoja naye, walijifanya abiria na ilikuwa vigumu kwa watu wengine kugundua kwamba watu hao walikuwa pamoja kwani walijitenga naye kupita kawaida.
Walipofika nje, wakamuona akiongea na dereva teksi, kwa jinsi walivyoongea, walionekana kama watu waliokuwa wakifahamiana, akaambiwa aingie ndani ya gari, akafanya hivyo.
Gilbert na wenzake hawakutaka kuchelewa, walikuwa na uhakika kabisa kwamba dereva teksi yule alikuwa ametumwa hivyo kuanza kuifuatilia teksi ile.
Walikuwanayo kwa umakini kabisa, hawakutakiwa kuwa na presha yoyote ile, ila walitakiwa kuwa makini kwa kuwa kama wangekosea hatua moja basi Bruno angeweza kuuawa.
Waliifuatilia teksi ile mpaka ikafika mahali fulani, nje ya nyumba moja, kwa jinsi walivyoangalia huku na kule, haikuwa vigumu kugundua kwamba eneo hilo lilikuwa la hatari sana, wakazima taa za gari lao na kisha kulisimamisha kwa mbali kidogo huku macho yao yakiwa katika teksi ile iliyokuwa imesimama.
“Tufanye nini? Tupige risasi?” aliuliza Putt.
“Hapana! Subiri kwanza!” alisema Gilbert.
Hapohapo wakamuona Kelly akielekea ilipokuwa teksi ile, akaufungua mlango huku akiwa na kipande cha nondo. Hakuwa peke yake, alikuwa na Adson ambapo wakambeba Bruno na kuingia naye ndani ya jumba lile.
“Tuwafuate?” aliuliza Bull.
Wakati wakiwa wamejiandaa, wakashtuka kuliona gari jingine likifika mahali hapo, mlango ukafunguliwa na mwanaume mmoja kuteremka.
Alikuwa Tim ambaye alikwenda uwanja wa ndege kuhakikisha kwamba Bruno anakamatwa. Alipofika maeneo yale, akasimamisha gari na kuteremka, naye akaingia ndani ya jumba lile.
Haraka sana Gilbert na wenzake wakateremka na kuanza kuelekea lilipokuwa jumba lile. Walikuwa na bastola mikononi mwao ili kuhakikisha wanafanya mauaji pale ambapo ingewabidi kufanya hivyo.
Walipofika katika dirisha la jumba lile wakaanza kuchungulia ndani. Wakawaona vijana wale wakiwa wamemuweka Bruno chini tayari kwa kuanza kumpiga.
Hawakuwa na bunduki, kama kumuua ilikuwa ni lazima wafanye hivyo kwa kutumia vipande vya nondo walivyokuwanavyo.
Kilichotokea ni kuanza kumshambulia Bruno na vipande vya nondo walivyokuwanavyo. Gilbert na wenzake walikuwa wakiangalia na kila walipotaka kuingia, Gilbert alikuwa akiwazuia kwa kuwaambia kwamba hawakutakiwa kuwa na presha hata kidogo.
“Watamuua!” alisema Putt huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Tunakusanya ushahidi, subiri!”
“Tunakusanya ushahidi?”
“Ndiyo! Subiri!”
Bruno alizidi kupigwa na vipande vya nondo ile mpaka akawaida hoi. Wakati wakijiandaa kummalizia, haraka sana Gilbert akanyoosha mkono wake uliokuwa na bastola, zilitoka risasi tatu mfululizo, kila mtu akapigwa, wakaanguka chini.
Gilbert na wenzake wakatoka kule walipokuwa na kuingia ndani, wakawafuata wanaume wale, wote watatu walikuwa chini wakiugulia maumivu, Gilbert hakutaka kuchelewa, hapohapo akawapiga risasi za vichwa Adson na Tim kisha kumuacha Kelly akiwa peke yake huku akiugulia maumivu.
Wakamshika Bruno pale alipokuwa, alikuwa amepasuliwa, alipigwa vibaya, hawakutaka kumuacha, wakamchukua na kumpeleka ndani ya gari huku wakiwapigia simu polisi na kuwaambia kwamba walitakiwa kuelekea katika jumba lile kuchukua maiti za waharifu ambao waliwashambulia kwa risasi.
“Na huyu?” aliuliza Putt huku akimaanisha Kelly.
“Tunaondoka naye!”
Japokuwa alikuwa na maumivu makali, hawakutaka kujali, walimchukua kwa kumshika hovyohovyo mpaka ndani ya gari na kuliondoa mahali hapo.
Njiani Kelly alikuwa akilia, alisikia maumivu makali katika paja lake la kulia, damu zilikuwa zikimtoka lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyejali. Walimchukua mpaka hospitalini na kumtaka kutibiwa huku akiwa chini ya ulinzi mkali.
Kwanza risasi ikatolewa na kuendelea na matibabu mengine. Wakati huo, pia Bruno alichukuliwa na kupelekwa katika chumba kingine na madaktari kuambiwa kwamba walitakiwa kuhakikisha mwanaume huyo anapona haraka iwezekanavyo kwa kuwa walikuwa na kazi naye.
Wakati hayo yote yakiendelea, mzee Todd alikuwa selo, kama kawaida yake alikuwa akilia mno, moyo wake ulimuuma kwa kuwa aliona kama Bruno alimsaliti kwa kile kilichokuwa kikiendelea.
Hakupokea taarifa yoyote ile, moyo wake uliumia kwani miongoni mwa watu aliokuwa akiwaamini alikuwa Bruno, na yote hiyo ni kwa sababu alikuwa naye kwa kipindi kirefu na hata kumpa kiasi kikubwa cha pesa.
Siku zikaendelea kukatika, baada ya siku ya kusikiliza tena kesi hiyo kwa upande wa mashahidi ilipofika, Bruno akachukuliwa na kupelekwa mahakamani huku akiwa amefungwa bandeji katika sehemu kubwa kichwani mwake kwani alikuwa amejeruhiwa mno.
Watu wengi hawakujua sababu ya mwanaume huyo kufika mahakamani, wengi walihisi kwamba inawezekana alikuwa na kesi kama watuhumiwa wengine ambao walikuwa wakifika hapo huku wakiwa wamejeruhiwa.
Baada ya dakika kadhaa, gari lilobeba watuhumiwa ambao walitakiwa kusimama kizimbani na kujibu mashtaka yao wakafika mahali hapo.
Haraka sana waandishi wa habari wakaanza kusogea na kuanza kupiga picha. Mtu waliyekuwa wakimtaka alikuwa mzee Todd, waliihitaji picha yake mno kwa kuwa ndiye mtu aliyekuwa akijulikana kuliko wote ambao walikuwa wakifikishwa mahakamani katika kipindi hicho.
Kwa kumwangalia tu isingekuwa vigumu kugundua kwamba moyo wake ulivunjika nguvu, mwili wake ulipungua kwa sababu ya kuwa na mawazo mengi. Alikuwa akiifikiria familia yake lakini pia aliifikiria kesi hiyo ambayo ilikuwa ikimuelemea.
Akaingia ndani, akawekwa katika kiti kimoja na kuambiwa kutulia hapo. Hakujua kama Bruno alikuwemo mahakamani, alichohisi ni kwamba alikuwa amesalitiwa na mwanaume huyo.
Wakili wake alikuwa mbele kabisa, yeye mwenyewe alionekana kuwa na hofu moyoni mwake, kila alivyokuwa akiiangalia kesi ile alikuwa na uhakika kwamba mteja wake angeshindwa kesi ile.
CIA walifanya kila kitu kwa siri kubwa, hakukuwa na mtu aliyetakiwa kujua kilichokuwa kikiendelea kuhusu mashahidi kwani walimficha Bruno kwa nguvu zote na ndiyo maana hata mzee Todd hakuambiwa kitu chochote kile, alitakiwa kumuona Bruno kwa kushtukiza mahakamani hapo.
Hakimu alipokuwa akiingia, watu wote wakasimama kama kumpa heshima na alipokaa, wakakaa na kutulia. Kesi ikaanza, kama kawaida ikaanza kusomwa kwa dakika chache, ilipoanzia mpaka siku hiyo ambapo mashahidi walitakiwa kusimama na kusema kile kilichokuwa kimetokea.
“Shahidi namba moja anaitwa Bruno,” alisema hakimu, mzee Todd akashtuka kulisikia jina hilo, alikuwa ameinama, akauinua uso wake.
Akamuona mwanaume mmoja akisimama na kuanza kuelekea kizimbani, kwa kumwangalia tu ilikuwa ni rahisi kugundua kwamba alikuwa kwenye maumivu makali, alitembea kwa msaada wa Gilbert ambaye alikuwa pembeni yake na kumpeleka mpaka kizimbani.
Kila mtu aliyekuwa mahali pale alikuwa akishangaa, hawakumjua mwanaume huyo, alikuwa amezungushiwa bandeji, na kwa usoni yalionekana macho tu kwani alikuwa amejeruhiwa vibaya.
Akanyoosha mkono wake wa kulia na kisha kujitambulisha na kuiambia mahakama kwamba kila kitu ambacho angekwenda kukizungumza mahali hapo kilikuwa cha kweli kabisa na asingezungumza uongo hata kidogo.
“Naitwa Bruno Mike Onyambe!” alijitambulisha na mahakama kuanza kusikiliza ushahidi wake.
Alianza kusimulia kila kitu baada ya yeye kutoswa ndani ya maji na baadaye kuokolewa na watu waliokuwa katika meli ambayo aliikumbuka kwa jina lake, iliitwa Britannian Cargo P56 kwani iliiandikwa ubavuni.
Mule ndani, akaepelekwa ndani ya chumba ambacho akakutana na mzee huyo akiwa amefungwa huko na hivyo kuanza kuzungumza.
Hakutaka kuishia hapo, alisimulia kila kitu mpaka mzee huyo alivyokuwa akitafutwa na vijana ambao walipokea maelekezo kutoka nchini Marekani na hata wakati familia yake ilipokuwa ikiuawa, walikuwa Afrika Kusini na waliiona taarifa hiyo kwenye televisheni.
“Hakukuwa na kipindi kigumu kwa mzee Todd kama kipindi hicho. Alilia sana, hakuamini alichokuwa akikiona, iliniumiza sana moyoni mwangu, kwa nilivyokuwa nikimwangalia, niliyaona mapenzi yake makubwa aliyokuwanayo kwa familia yake. Mara nyingi aliniambia kitu kimoja tu kwamba kuna mtu anaitwa Maxwell ndiye aliyekuwa amesababisha yote hayo, alitaka kumuona akiingia gerezani ili afanye biashara zake kwa uhuru zaidi,” alisema Bruno, mahakama nzima ilikuwa kimya.
Alitumia dakika arobaini na tano, alipomaliza, akashuka kizimbani. Mzee Bruno alikuwa akilia, hakuamini kilichokuwa kikitokea. Ushahidi wa Bruno ulimkumbusha mbali kabisa, ulimkumbusha familia yake na mateso makubwa aliyoyapata alivyokuwa ndani ya meli.
Alipomaliza, akanyamaza. Akaanza kuulizwa maswali kutoka upande wa jamhuri na kila alipokuwa akiulizwa, alijibu kama ilivyokuwa ikitakiwa.
Alipomaliza, akateremka na kisha hakimu kusema kwamba kulikuwa na ushahidi kutoka CIA ambao ulikuwa ni wa kina kwa kuwa ulifuatiliwa kwa hatua zote.
Akaanza kuusoma ushahidi huo ambao ulieleza mambo mengi kuhusu mchezo ulivyokuwa na moja kwa moja ulikuwa ukimuweka hatihani mzee Maxwell.
“Vijana walifuatilia kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Ni kweli mzee Maxwell alikwenda Afrika, alipofika huko, akatekwa na kuingizwa katika meli iitwayo Britannian Cargo P56 ambayo ina usajili wa jina la Maxwell anayemiliki kampuni kadhaa nchini Marekani,” ulisema sehemu ya ushahidi huo na kuendelea:
“Nchini Afrika Kusini kulikuwa na kijana aliyekuwa akishirikiana naye, huyu aliitwa Xuso ambaye aliuawa siku chache zilizopita. Pale bandarini, Pretoria ndipo alipotaka kumalizia kazi yake kwani aliamini kuwa endapo angemuua Todd pale ingekuwa ni rahisi kwao kuupoteza mwili huo kwa kuwa walikuwa na watu wengi.”
“Walifanikiwa kwa kila kitu. Baadaye baada ya kugundua kwamba mzee Todd amekamatwa, alichokitaka ni kupoteza mashahid, hapa tunapoongea, kijana ambaye alikuwa karibu na Todd, Innocent, ameuawa na tulivyofuatilia tukagundua kwamba kijana huyo alianza kuweka ukaribu na Maxwell na alihusika katika kuweka madawa ya kulevya ndani ya nyumba ya Todd.”
“Yeye alifanikisha kutekwa kwa familia ya Todd, alihakikisha anashirikiana nao kwa ukaribu lakini waliposikia kwamba naye alitakiwa kuwa shahidi, wakamuua na mwili wake kuutupa baharini.”
“Bruno ambaye ni raia wa Kenya alipitia vikwazo vingi. Kwanza hakutakiwa kufika Marekani kwa kuwa Maxwell alijua kwamba mtu huyu alikuwa mwiba hatari sana. Wakamteka mchumba wake ili baadaye atishwe kwamba angeuawa kama tu angekanyaga nchini Marekani, bahati nzuri baadaye msichana yule alitoroka walipofika nchini Tanzania.”
“Hiyo haikutosha, wakapanga mipango wamteke uwanjani, walifanikiwa ila kwa kuwa maofisa wetu ni watu hatari, walifanikiwa kumuokoa katika mikono yao na kuwaua vijana wawili na kumbakiza mmoja,” ulisema sehemu ya ushahidi huo.
***
Mahakama nzima ilikuwa kimya ikisikiliza ushahidi uliotolewa na Shirika la Kijasusi la CIA. Kila mtu alikuwa makini kusikiliza, kile ambacho kilizungumzwa mahali hapo kilionekana kumshangaza kila mmoja.
Baada ya kutolewa kwa ushahidi huo mrefu ambao ulichukua saa moja, ndipo mahakama ikasimamishwa kwa muda kwani baraza la wazee lilitakiwa kulizungumzia jambo hilo kabla ya kutoa uamuzi wa kukamatwa kwa Maxwell.
Muda huo mzee Todd alikuwa akitokwa na machozi ya uchungu, hakuamini kile alichokiona kikiendelea, mbali na Bruno, hata CIA walikuwa upande wake kumtetea kwa kila kitu kilichokuwa kimetokea.
Alitamani kusimama na kumfuata Bruno na kumkumbatia kwani kwake, alikuwa mwanaume shujaa ambaye alimtetea mpaka pumzi ya mwisho kabisa.
Baraza hilo la wazee lilikaa kwa nusu saa nzima ndipo likatoka na mahakama kuendelea. Kitu cha kwanza kabisa kilichoamuriwa na mahakama ni kuachwa huru kwa mzee Todd lakini vilevile Maxwell alitakiwa kukamatwa na kufikishwa mahakamani huku akitakiwa kusomewa mashtaka ya kushiriki katika mauaji ya familia ya mzee Todd na hata kifo cha Innocent.
Kesi ilipofungwa, mzee Todd akamsogelea Bruno na kumkumbatia, hakuamini kama alishinda kesi hiyo ambayo iliibua chuki kubwa mioyoni mwa Wamarekani kwa kuwa waliamini kwamba aliua na kukimbia nchini humo.
Akamshukuru sana kiasi cha kutokwa na machozi, walizungumza kidogo na kisha kuondoka ndani ya mahakama hiyo huku Bruno akiwa chini ya ulinzi mkali kwani hakukutakiwa kuachwa hata kidogo kwa ajili ya usalama wake.
Siku hiyohiyo Maxwell akakamatwa na siku iliyofuata kupelekwa mahakamani. Kesi yake ilikuwa nzito na iliyonguruma kwa miezi miwili na mwisho wa siku kukutwa na hatia na kuhukumiwa kifo kwa kuchomwa sindano ya sumu ya cynaide.
Kwa Bruno, aliendelea kutibiwa hospitalini nchini Marekani huku akiwa chini ya ulinzi mkali. Hakukutakiwa mtu yeyote kuingia ndani ya chumba chake zaidi ya daktari, mzee Todd na Sharifa ambaye alisafirishwa mpaka Marekani kwa ajili ya kumuona mpenzi wake.
Mzee Todd hakuacha kumshukuru Bruno, kwake, mwanaume huyo alionekana kuwa mkombozi aliyemuokoa katika mdomo wa kifo, hakutaka kumuacha hivi hivi kwani hata alipopona, akamuingizia kiasi cha dola bilioni moja kwenye akaunti yake ambapo kwa pesa za Kitanzania ilikuwa ni zaidi ya shilingi trilioni mbili.
Maisha ya Bruno yakabadilika, alikuwa masikini, aliyedharauliwa lakini mwisho wa siku alikuwa bilionea aliyeheshimika sana nchini Kenya.
Hakuacha kuwasiliana na mzee huyo, kwake, alikuwa kama baba yake kwani ndiye mzee ambaye alikaa naye kwa kipindi kirefu na kumfundisha maisha kuhusu umiliki wa pesa, biashara na mambo mengine mengi.
Baada ya miezi tisa kutimia, hatimaye Sharifa akajifungua mtoto wa kike na kumpa jina la Grace, yaani Rehema akiwa na maana kwamba kwa kile alichokuwa nacho, maisha aliyokuwa akiishi ni kama alipewa rehema tu kutoka kwa Mungu wa mbinguni.
Kutoka katika maisha ya dhiki, kuishi katika kijumba kibovu alichoachiwa na wazazi wake mpaka kuishi kwenye bangaloo kubwa, hakika ilikuwa ni ndoto moja ya kusisimua kupita kawaida.
“Kila kitu kilipangwa na Mungu. Mtu wa kwanza kumshukuru ni baba yako, bila yeye, nisingekutana na mzee Todd, bila yeye nisingekuwa hapa nilipokuwa,” alisema.
Aliendelea kufungua kampuni nyingi, kwa kuwa aliamua kuwekeza kwenye uvuvi pia, akanunua meli kubwa iliyokuwa ikisafiri mbali kwenda kuvua huku akimuweka Abdul kuwa kiongozi lakini pia hakuangalia ubaya, akamchagua James na mwenzake ambao ndiyo waliomtosa baharini na kuwapa vyeo kwa kuamini kwamba pia watu hao wawili walichangia kuyabadilisha maisha yake.
Hakuangalia kisasi, alisahau kila kitu, nguvu ya upendo ilikuwa na uwezo wa kubadilisha kila kitu, hicho ndicho alichokikumbuka ambacho alihubiriwa mara kwa mara kanisa.
“Upendo unapozidi, kisasi kinakufa, namshukuru Mungu kwa kuyabadilisha maisha yangu na kuniweka hapa. Tulimuomba Mungu sana siku moja tuishi pamoja, na hapa tunaishi pamoja, siku si nyingi kuanzia leo tutafunga ndoa,” alisema Bruno huku akimwangalia Sharifa.
“Nakupenda sana, nakupenda zaidi kwa kuwa umekuwa mtu wa msamaha kwa kila aliyekutendea ubaya,” alisema Sharifa.
“Hilo ndilo ambalo Mungu anatuagiza kila siku. Tunatakiwa kusamehe hata kama tulikasirishwa na kupata maumivu makubwa kiasi gani,” alisema Bruno, hapohapo akamkumbatia mpenzi wake huyo na kujifunika shuka, kilichoendelea, hakifai kuandikwa mahali hapa.
MWISHO.