Hadhi na heshima ya Baba wa Taifa iko mashakani

Hadhi na heshima ya Baba wa Taifa iko mashakani

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,639
Reaction score
164,777
Ukifuatilia kwa makini kuhusu hili swala la muungano,utagundua kuwa limegubikwa na utata na inawezekana kabisa moja ya waasisi wa muungano huu(mwalimu Nyerere) alicheza "foul" na imekuwa ni siri ya mika nenda miaka rudi ila sasa wakati umefika hii siri lazima ijulikane tofauti na hapo ni kuvunja muungano.

Hapa sasa naanza kupata jibu ni kwanini siku zote mwalimu alikuwa mkali pale watu walipokuwa wakihoji uhalali wa muungano na muundo wake.Bila shaka alitambua kuna mengi yangefichuka ila sasa wakati umefika yaliyokuwa yakifichwa yatafichuka na hapa ndio naposema hata hadhi na heshima ya mwalimu katika hili taifa itakapochafuka.

Mbali na mapungufu ya juu ya uhalali wa huu muungano kama vile hati ya muungano n.k,kitendo cha siri za muungano kuwa hadharani ni doa kubwa kwa Baba wa taifa kwani siri hizo zitathibitisha kama muungano huu ni "haramu" au laa.

Time will tell.
 
muungano si haramu,kama kuna makosa ya ki bin adam basi ni yapo,tusing'ang'anie hivyo vijikosa kwa malengo ya kuuvunja.
 
muungano si haramu,kama kuna makosa ya ki bin adam basi ni yapo,tusing'ang'anie hivyo vijikosa kwa malengo ya kuuvunja.

Tatizo Nyerere alikuwa anachukuliwa kama kiongozi mwenye uadilifu wa hali ya juu lakini kwa hili la muungano linaweza kugeuka kuwa kashifa kubwa kwake.
 
Nyerere ana kashfa nyingi sana. Lakini huwezi kutaja upuuzi wa nyerere bila ya kuambiwa "mdini". Lakini kama inavyosemwa, uongo hupanda kwa lift na ukweli hupanda kwa ngazi. Kuna siku mtakubali tuu kama baba wenu wa taifa alikuwa mbulumundu mmoja tuu.
 
Nyerere ana kashfa nyingi sana. Lakini huwezi kutaja upuuzi wa nyerere bila ya kuambiwa "mdini". Lakini kama inavyosemwa, uongo hupanda kwa lift na ukweli hupanda kwa ngazi. Kuna siku mtakubali tuu kama baba wenu wa taifa alikuwa mbulumundu mmoja tuu.

Acha hizo Hakuna binadamu aliye kamili,kila mtu ana mapungufu yake,Nyerere mwenyewe kupitia zile hotuba zake alikiri kuwa Serikali yake kwa miaka 26 ilifanya mabaya na Mazuri,ikija Serikali mpya inachukua yale mazuri,hasa ya Msingi na kuyaendeleza,lakini wapo wajinga wanahoji hata yale mazuri ! Nyerere kwenye muungano ni kweli alimzidi akili Karume ndio maana ile Picha ya kuchanganya Udongo inaonyesha Nyerere akishika Vikombe viwili kushoto na kulia mwenyewe kisha akachanganya udongo huku karume akishuhudia,Tambua Nyerere alikuwa na Lengo la kuwa na Serikali 1 tu ili kupunguza Gharama ,baada ya kufariki tu,wakaacha kuchukua mazuri yake wakaamua kutengeneza Ulaji kwa kuzidisha Kero na kuanzisha wizara ya muungano ili kupitishia pesa zao humo kwa kisingizio cha kumaliza kero,pesa inaliwa na kero zipo zinazidi na sasa Zenji wamevunja Katiba wanajiita Nchi huku Mishahara na matumizi yao yote yanalipwa na Tanganyika. Nyerere alikuwa mjanja lakini kwa hili la muungano haliwezi kumvunjia heshima,kwani hakuna mahali alikataza muungano usikarabatiwe,alipenda mabadiliko ndio maana alikubali mfumo wa vyama vingi.
 
Nyerere ana kashfa nyingi sana. Lakini huwezi kutaja upuuzi wa nyerere bila ya kuambiwa "mdini". Lakini kama inavyosemwa, uongo hupanda kwa lift na ukweli hupanda kwa ngazi. Kuna siku mtakubali tuu kama baba wenu wa taifa alikuwa mbulumundu mmoja tuu.

Umetumia vyema uhuru wako wa kutoa mawazo, na busara ya hali ya juu...pole sana!
 
Tatizo Nyerere alikuwa anachukuliwa kama kiongozi mwenye uadilifu wa hali ya juu lakini kwa hili la muungano linaweza kugeuka kuwa kashifa kubwa kwake.
Hakuna kashifa pale Nyerere picha zinaonyesha anachanganya Udongo kwa mikono yake miwili huku karume akishuhudia hivyo kama nyerere alikuwa mjanja basi ni makosa ya akina Karume kukubali kuburuzwa ikiwa kashifa haitamgusa Nyerere peke yake itakuwa ni kashifa ya wote.
 
Nyerere hana pa kulaumiwa alifanya yake kwa kipindi kile tekinologia ikiwa chini,mfumo wa chama ulikuwa mmoja tu,katiba ilikuwa inaruhusu Zidumu Fikra za M/kiti nk alifanya mambo mengi kwa mujibu wa katiba ya kipindi hicho,hata yale mabadiliko ya katiba nyerere aliyalidhia,nyerere hukuwa Adui wa mabadiliko alipenda watu kwenda na wakati ,Tambua nyerere ni Rais pekee wa Tz ambaye alinusulika kupinduliwa mara kadha wa kadha hv ndio maana wakati mwingine aliamua kutawala kwa machale,hata mapungufu yake yalichangiwa na mazingira kama hayo.
 
Haiwezi shindwa kuwa mashakani kwa kuwa hadhi ya Tanzania na viongozi wake ilishashuka kitambo!
 
Aijalishi nini kilifanyika kipindi cha Nyerere, kinachotazamwa ni nia ya Nyerere kwa Tanzania ilikuwa nzuri au mbaya. Kama alifaulu jambo fulani lakini nia yake ilikuwa mbaya hapo heshima itashuka ila kama alifel mahali fulani lakini nia yake ilikuwa njema basi heshima yake itazizi ongezeka siku baada ya siku vizazi kwa vizazi.
 
Ndio maana maoni ya watanganyika wanataka muundo wa serikali tatu ili kutouvunja huo muungano,kwa sababu serikali moja haiwezekani hata kwa akili ya kawaida haikubali,huwezi ukabadilisha iliyokuwa nchi kuwa mkoa au jimbo.serikali mbili imeshindikana na ndiyo maana imekuwapo kiujanja ujanja kama tuanvyoishi kibongo bongo na maisha yanaendelea.ufumbuzi mzuri ni kuuvunja muungano tutafakari tunataka nini na wananchi waulizwe mawzo yao.sijui kwa nini hilo nalo halikubaliki?.
 
Ni binadamu so alikuwa na mapungufu pia tumkubali kwa mema na mazuri alofanya lakini pia tumsamehe kama alikosea na turekebishe huku tukumshukuru kwa kuonesha njia!!!!!

Na kama haufai muungano tuutawanyishe tu
 
Heshima ya Nyerere haitakaa ishuke hata siku moja, make mabaya ni machache na mazuri ni mengi. Isitoshe kila mmoja ana mikakati yake ya kuongoza kama uonavyo sasa waheshimiwa wetu kwani wao tutawakumbuka kwa lipi????????????:flypig:
 
Ukifuatilia kwa makini kuhusu hili swala la muungano,utagundua kuwa limegubikwa na utata na inawezekana kabisa moja ya waasisi wa muungano huu(mwalimu Nyerere) alicheza "foul" na imekuwa ni siri ya mika nenda miaka rudi ila sasa wakati umefika hii siri lazima ijulikane tofauti na hapo ni kuvunja muungano.

Hapa sasa naanza kupata jibu ni kwanini siku zote mwalimu alikuwa mkali pale watu walipokuwa wakihoji uhalali wa muungano na muundo wake.Bila shaka alitambua kuna mengi yangefichuka ila sasa wakati umefika yaliyokuwa yakifichwa yatafichuka na hapa ndio naposema hata hadhi na heshima ya mwalimu katika hili taifa itakapochafuka.

Mbali na mapungufu ya juu ya uhalali wa huu muungano kama vile hati ya muungano n.k,kitendo cha siri za muungano kuwa hadharani ni doa kubwa kwa Baba wa taifa kwani siri hizo zitathibitisha kama muungano huu ni "haramu" au laa.

Time will tell.

Huu sio Muungano ni Utapeli...
 
Kitendo cha Rais Mstaafu wa Zanzibar, wa Awamu ya Pili, Mheshimiwa Aboud Jumbe, kumwandikia barua Nyerere kumweleza kuwa kwa mujibu wa waraka wa makubaliano ya Muungano ya 1974, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ulikusudiwa uwe ni wa shirikisho lenye serikali tatu, na siyo mbili, au moja, kama inavyodaiwa na CCM -Bara, kilimsababishia Jumbe ajiuzulu nyadhifa zake zote, katika chama na serikali.

Na lile kundi la Wabunge 55 wa Bara, G55, walipotaka iwepo serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano, Nyerere wakati huo akiwa amekwisha ng’atuka Urais wa Tanzania na uenyekiti wa CCM, alisimama kidete kuwapinga wabunge hao na kulisambaratisha kundi lao. Aliandika na kitabu kuwasema na kuwakosoa aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamo Mwenyekiti wa CCM, Mzee Malecela na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Hayati Kolimba, kwa kile alichodai, kumshauri vibaya Rais Mstaafu, wa Awamu ya Pili, Mheshimiwa Al-Hajj Ali Hassan Mwinyi.
 
Nyerere aliamua kuacha Kazi yenye Heshima na Kupigania Uhuru wa Watanganyika.Hilo liliwashinda Wazee Wengi kabla yake hasa kutokana na Mapigo ya Wakoloni.Jiulize,Ni nani kati ya hawa Viongozi wa Leo wanaowaogopa Wawekezaji Wazungu wangeweza kumtimua Mkoloni?.Ukijipa Muda kidogo wa Kutafakari kwa Utulivu ndio utagundua Nyerere alikuwa Kiongozi wa aina yake.
 
Back
Top Bottom