Habibu Mchange njiapanda

Habibu Mchange njiapanda

tenende

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2012
Posts
6,511
Reaction score
506
HABIBU MCHANGE aka Mdude ambaye pia alikuwa kiongozi mkuu wa kikundi haramu cha MASALIA aka PM7 yuko njiapanda kuhusu hatma yake ya kisiasa.

Tangu kundi hili liliposambaratishwa (mwezi desemba mwaka jana), na kufia mbali (januari mwaka huu), kundi hili liliangukia katika mgogoro wa kuchagua mahali sahihi pa kwenda wote kwa pamoja lakini hawakuafikiana. Mazungumzo yao ya kawaida, mawasiliano yao na Vikao vyao vilikuwa na maeneo matatu ya kwenda: 1. Kuanzisha CHAUMA; 2. Kuhamia CCM 3. Kuhamia NCCR mageuzi. Pendekezo la kurudi CHADEMA na kuomba radhi lilipingwa na wengi, hasa Eddo, Mtela na Shonza.

  • Wazo la kuanzisha chama cha siasa (CHAUMA) - lilionekana kuwatisha wengi kwa kuhisi kuna kazi kubwa ya kukijenga chama hicho ili kiaminiwe na watanzania wengi!.

  • Wazo la kuhamia NCCR lilitolewa na EDDO ambaye amekuwa akitoa sababu za kwamba angependa aendelee kuwa mpinzani na tena vijana wengi walioenda NCCR wengi wao wamefanikiwa sana kisiasa. Wenzake walilikataa wakihofia kwamba chama hicho kitawapa wakati mgumu saana kujiuza.

  • Wazo la kuhamia CCM lilionekana kuungwa mkono na BWANA fedha na bibi fedha (FEDHA MAALUMU) za kutoka CCM (kuibomoa CHADEMA) na wengine kusitasita.

Tangu mwanzo Shonza na Mtela wao walionekana kuchagua kwenda CCM wakiwa na sababu:

1. Kimewasaidia sana kuwaweka mjini kwa zaidi ya mwaka mmoja. Hela hii imekuwa ikiwafikia wengine hata kabla ya kufukuzwa CHADEMA kupitia MTELA na mara nyingine SHONZA.

Hela za kutoka MASWA (ambapo katika awamu zote mpaka jumapili ya tarehe 24/2/2013 nilipowasiliana na mtela zinawafikia kupitia MTELA). Mtela alikuwa anapewa hela za maswa na muda mwingine za LUMUMBA na kuwafikishia wengine. Kwa mfano EDDO amekuja DAR zaidi ya mara 5 mwezi januari na februari akiwa hajalipwa mshahara miezi mi 3. Hapa ndipo alikuwa anatokea;

2. Wote walikuwa wameahidiwa AJIRA, ambapo mpaka sasa taarifa za ndani zinaonyesha kuwa atafanya kazi LINDI au MTWARA (siyo ualimu aliousomea wala si ukuu wa wilaya-kulingana na makubaliano ya awali na ya sasa). Shonza ameahidiwa kubaki Dar!.. AJIRA hizo wameahidiwa kupewa rasmi baada mizunguko ya kisiasa kuibomoa CHADEMA.

3. Ndani ya CCM watatafuta namna ya kujisafisha na kujitofautisha na mafisadi papa ili wagombee ubunge na kushinda. Mtela anaona akiwa CCM anaweza kuwa na nguvu MBOZI MASHARIKI kuliko kuwa NCCR. Vivyo hivyo Shonza analenga viti maalumu, jimbo la ubungo na jimbo la MBEYA mjini.

HABIBU Mchange kwa upande wake alisita sana kuhamia mapema kwa kuhofia kuchuja ZAIDI. Alibaki kuongoza chama cha wanamuziki wa kigoma LEKA DUTIGITE na kueandelea kula kwa jasho lao!. Hivi sasa yupo tayari kujiunga na CCM lakini ANASEMA KUWA anahofia kuporomosha IMAGE yake mbele ya jamii. Washauri wake wamemuambia akiamua kwenda CDM kuoma radhi muda huu hatapokelewa!. Wamemshauri aende CCM akatumie majukwaa yake kuisakama CHADEMA na baadaye mwaka huu arudi na kuomba radhi kwenye mkutano mkubwa wa CHADEMA!.. Huyu bro anaonekana kuukubali ushauri huu!..

MTIZAMO WANGU: Ni heri aende kuomba msamaha sasa (kama kweli ana nia ya kurudi) kuliko kuitukana CHADEMA majukwaani na baadaye kuomba kurudi. Naona hataaminiwa kabisa kuliko sasa.

SOURCE: Mimi mwenyewe kwakuwa nipo nao katika mambo mengi.
 
Hawa vijana wazalendo kwanini wanasumbuliwa namna hii? Kwanini wasipewe fursa ya kuwatumikia Watanzania wenzao?
 
Mkuu,

Ulichosema chaweza kuwa ni ukweli. Ila kwa uhalisia wa sasa, hawa vijana walinyea kambi kabla mvua haijakatika, na wana wakati mgumu sana kurejesha imani ya Wananchi kwao. Hebu ona kama hawa Mtela na Shonza; wanamtukana Dr. Slaa kila siku wakifikiri kuwa huo ndio mtaji wao wa kufanikiwa kisiasa. Wanafanya hivyo wakitekeleza maagizo na ushauri wa majuha wengine kama Nape na Nchemba. Kumbukumbu za kihistoria zinaonyesha kuwa, kila aliyejaribu kumtukana Dr. Slaa kwa kumtumia kama ngazi ya umaarufu, mwishowe alipoteza hata umaarufu mdogo aliokuwa nao. Nadhani hili Mchange amelitambua ndio maana yeye sasa ametulia na kuanza kujitathmini kwanza.

Chadema ndicho chama kilichowapa hawa vijana umaarufu. Waliupata umaarufu huu baada ya awali kujipambanua kama wapiganaji, wasimamia ukweli. Watu waliwakubali, si wao kama wao, bali ukweli waliousimamia. Sasa leo wameuacha ule ukweli ambao uliwafanya watu wawakubali, tayari wameshakuwa maadui wa umma. Kumbuka Chadema ni nguvu ya umma. Mtu aisalitipo nguvu hii, kwa hakika anavuna upepo, anavuna kudharaulika, anavuna kutothaminika, kwa ufupi anavuna matusi. Namshauri Mchange atulie na afanye maamuzi sahihi, asikurupuke kama hawa Mtela na Shonza. Nguvu ya umma inaamua yote.
 
Nina imani HABIBU Mchange akiomba msamaha kwa dhati, atasamehewa! ni mwanasiasa mzuri akijiroga kuwa kada tegemezi, amekwisha kisiasa.
 
Habibu Mchange ni mwanasiasa kinda kwa maana upeo wake ni mdogo! Mwanasiasa mzuri aliyekomaa unafanya jambo moja lazima uwe na plan B ikiwa lile la kwanza litashindwa sasa kama alikuwa anatumika kuibomoa chadema halafu hakujua baadae afanye nini ni maajabu!!? Anyway naunga mkono wazo la mleta mada kuwa arudi chadema atubu makosa yake na kuomba radhi na kuahidi kutorudia tena kutumika atasamehewa huyu shosti anayesubiri Viti maalumu amepotea maana katiba mpya inaenda kuvifuta ila anaweza kukaa pale Lumumba na kuwaburudisha viongozi wa ccm bado analipa,. ila akishaanza kuchoka atafute hata pesa aanzishe kamradi tena mapema kabla ya kimbunga ya 2015!!
 
Siasa ni utumishi wenye uzalendo si ajira! Ujira wa siasa ni sawa na ujira wa viongozi wa dini!

Kwa maana ya siasa ya utumishi wa watu hawa masalia si wanasiasa bali job seeker tu kama vijana wetu wengine wanaoweza kudhalilisha utu wao ili wapate ajira!

CDM kama chama cha siasa lazima kijitenge na watu wa namna hii na uwepo utaratibu wa malezi ya vijana wakizalendo wenye nia njema.

Msamaha ni kwa anayejuta na kutambua makosa yake na kutotamani kurudia tena si kwa lengo la kufanikisha matamanio ya kisiasa tu.

Yetu macho kwa hawa vijana!
 
Ninahisi kama Habib alipotoshwa na watu fulani ili akisaliti chama hiki cha wazalendo, walijaribu kutumia ile style yao ya zamani ambayo kwasasa inaligharim taifa, hoja ya udini ili mbele za watu CDM kionekane hivyo walivyo kua wanataka, sasa Habibu amerudisha his senses na kugundua alikosea sana, namshauri, hawezi kurudi CCM akakaa salama cuase inaonekana hawezi kuishi kinafiki, akirudi ccm tu napata hisia pia kua anaweza kuacha kabisa siasa kwasababu ya hisia zake zinavyomtoka moyoni, kuishi na kuitumikia ccm kunamtaka mtu awe mnafiki wa hali ya juu sana, mtu ambaye anaongea asicho kiamini kabisa moyoni mwake, ndio sababu watu kama Nape na Shoza imebidi hata masuala ya Kanisani wayache kabisa, wameona warudie upagani wao why?

Cause wanajikuta watembea na kuhubiri tofauti na wanavyo amini, nini kinachowatokea sasa, Dhamiri zao zinawahukumu kila wanapotamka kitu kwenye mikutano.

Habibu, nakushauri, fanya kama alivyo fanya Ben Saanane, nenda CDM kaombe msamaha sasa na eleza kila kitu na kubali masharti yote utakayo pewa na viongozi wale makini, kurudi ccm ni kujipotezea muda, ukombozi wa nchi hii upo karibu mno kuliko unavyofikiri. Huo ushauri unaopewa na hao wahuni wa mjini ni kukupotosha tu, wanataka uendelee kuishi kihuni kihuni, muda huo umeisha kwisha mdogo wangu, tuliza akili.
 
Hawa vijana wazalendo kwanini wanasumbuliwa namna hii? Kwanini wasipewe fursa ya kuwatumikia watanzania wenzao?
Hawa Masalia wanatumikia MATUMBO yao. Hakuna Mtanzania mzalendo anayehitaji utumishi wa hawa watoto wasio na adabu hata kwa watu wazima...

Kwanza watatumikia katika idara gani maana hawataki kufanya kazi walizosomea na kuamua kuishi kiujanja ujanja. Ubaya wanaoufanya kwa sisi watanzania tunaolipa kodi lakini zinatafunwa na MaCCM na wao wamejiunga na watafuna kodi zetu, mwisho wake ni aibu. Na aibu inakaribia.

Kivuli cha Dr Slaa kinawafuata kila wanakoenda. Mwenzao Mwigulu Chemba alikimbia kinywaji alicholipia baada ya kumuona Dr Slaa kaingia hotelini. Long live Dr Slaa, wapigishe kwata magamba na masalia wao in full force hadi 2015 na sisi watanzania tutaendelea kuchangia harakati zako kupitita M4C
 
mchange huwa na chat naye sana na kumweleza mdogo wangu ulichemka sana
Cha msingi hapa ni ww kurudi chadema ukatubu dhambi zako jimbo la kibaha mjini bado ni lako na wana nchi wako badi wanakuamini sana utaingia bungeni kupitia kibaha mjini mchange rudi tubu dhambi zako utasamehewa
 
Na wewe ni masalia mdogo mdogo au ndio wakala wa kukabidhi mzigo toka kule?

Sinkala, mimi siyo masalia aka PM7, ila mchange, na Mtela ni watu ambao pamoja na kuasi wao ni kama kaka zangu. Wao pamoja na Shonza nimekuwa nao ktk shughuli za siasa kwa muda mrefu. Nawafahamu in and out!... Siwezi kuwatenga kwa itikadi waliyoichagua. Eddo na Deo pia nafahamiana nao muda mrefu.
 
Du kazi ipo. Yaani Mchange anataka kuitukana chadema kwanza halafu ndio arudi kuomba radhi. Mboni mambo.

Mi naona bora aendelee tu kuitukana chadema bila kukata tamaa kama wanavyofanya masalia shonza na mwampamba. Akiomba msamaha sasa haitasaidia....yaani baada ya kuona mambo magumu ndio akumbuke msamaha!!?
 
Hawa Masalia wanatumikia MATUMBO yao. Hakuna Mtanzania mzalendo anayehitaji utumishi wa hawa watoto wasio na adabu hata kwa watu wazima...

Kwanza watatumikia katika idara gani maana hawataki kufanya kazi walizosomea na kuamua kuishi kiujanja ujanja. Ubaya wanaoufanya kwa sisi watanzania tunaolipa kodi lakini zinatafunwa na MaCCM na wao wamejiunga na watafuna kodi zetu, mwisho wake ni aibu. Na aibu inakaribia.

Kivuli cha Dr Slaa kinawafuata kila wanakoenda. Mwenzao Mwigulu Chemba alikimbia kinywaji alicholipia baada ya kumuona Dr Slaa kaingia hotelini. Long live Dr Slaa, wapigishe kwata magamba na masalia wao in full force hadi 2015 na sisi watanzania tutaendelea kuchangia harakati zako kupitita M4C

Kaka ni kweli, hawapendi kufanya kazi walizosomea. MWAMPAMBA aligoma kabisa kufundisha alipofika kituo chake kanda ya ziwa kufundisha. Aliishia kutokomea na fedha za malipo ya awali alizopewa na serikali. Kwa ufupi hana usafi wa kuibeba CCM mbele za UMMA!.
 
Ninahisi kama Habib alipotoshwa na watu fulani ili akisaliti chama hiki cha wazalendo, walijaribu kutumia ile style yao ya zamani ambayo kwasasa inaligharim taifa, hoja ya udini ili mbele za watu CDM kionekane hivyo walivyo kua wanataka, sasa Habibu amerudisha his senses na kugundua alikosea sana, namshauri, hawezi kurudi CCM akakaa salama cuase inaonekana hawezi kuishi kinafiki, akirudi ccm tu napata hisia pia kua anaweza kuacha kabisa siasa kwasababu ya hisia zake zinavyomtoka moyoni, kuishi na kuitumikia ccm kunamtaka mtu awe mnafiki wa hali ya juu sana, mtu ambaye anaongea asicho kiamini kabisa moyoni mwake, ndio sababu watu kama Nape na Shoza imebidi hata masuala ya Kanisani wayache kabisa, wameona warudie upagani wao why?

Cause wanajikuta watembea na kuhubiri tofauti na wanavyo amini, nini kinachowatokea sasa, Dhamiri zao zinawahukumu kila wanapotamka kitu kwenye mikutano.

Habibu, nakushauri, fanya kama alivyo fanya Ben Saanane, nenda CDM kaombe msamaha sasa na eleza kila kitu na kubali masharti yote utakayo pewa na viongozi wale makini, kurudi ccm ni kujipotezea muda, ukombozi wa nchi hii upo karibu mno kuliko unavyofikiri. Huo ushauri unaopewa na hao wahuni wa mjini ni kukupotosha tu, wanataka uendelee kuishi kihuni kihuni, muda huo umeisha kwisha mdogo wangu, tuliza akili.

kweli umemshauri vizuri sana. Akatubu CDM, aeleze yote kama Ben, aanze upya! Ushauri mzuri
 
Mchange ajifunze kwa Zitto, waliyekuwa wanamwegemea!
 
Hawa vijana wazalendo kwanini wanasumbuliwa namna hii? Kwanini wasipewe fursa ya kuwatumikia watanzania wenzao?

Mkuu sijawasumbua!.. Kama huamini haya niyasemayo basi tafuta namba ya simu ya mchange au mtembelee TABATA, utagundua yupo ktk wakati mgumu sana kisiasa. Pamoja na kuongoza UASI, lakini hakujua madhara yake yatakuwa ni kufukuzwa!...
 
Hawa vijana wazalendo kwanini wanasumbuliwa namna hii? Kwanini wasipewe fursa ya kuwatumikia watanzania wenzao?
Mkuu, aina ya uzalendo wanaouonyesha vijana hawa si ile ambayo watu wengi wanaamini kuwa ni moja ya njia kuu za ukombozi.
Uzalendo wa kutumikia makundi ni lazima uwatie mashaka watu wenye lengo la kuijenga nchi


Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Japo simjui vizuri mchange ni vema atulie kama best yangu chacha okong na dada zaituni(ex-katibu wa cdm nyamagana)
 
Mh! Naamini kuteleza si kuanguka, kama anahisi alipotoka basi
aombe radhi kwa viongozi wake ili waanze upya, la kama anaona
alikuwa sahihi basi aende CCM ambako ataendelea na mikakati
yake kumchafua Dk. Slaa na Chadema. Sioni kitu cha kumuweka
njia panda muda wote huu..
 
Back
Top Bottom