Kuna mjadala nimeusikia kutoka kwenye radio kuhusu ukosefu wa ajira kwa vijana wa elimu ya juu. Watanzania wengi hukimbilia kusema wajiajiri.Mimi mawazo yangu , nikianza na serikali ingefanya hivi, wale watumishi wanaostaafu kila mwaka nafasi zao wachukue hao vijana kulingana na walichosomea yani taaluma zao.Ila shida utakuta aliestaafu alikua mhudumu wa masijala nafasi IPO au fundi bomba amestaafu .na nyinginezo sasa hiyo degree ataziba hizo nafasi? Wakati ana degree! .sasa Maono yangu serikali iangalie mfano huyu ni fundi bomba mstaafu nafasi IPO wazi kama serikali ingemlipa huyu mwenye degree kwa kazi hiyo hiyo ya bomba au uhudumu wa masijala. Nadhani kwa MTU mwenye akili timamu atashika spaner kwa elimu yake hiyo hiyo ya degree na mshahara alipwe wa scale ya degree pia .nadhani italeta tija.