HabariLeo: Zitto hakamatiki urais 2015

HabariLeo: Zitto hakamatiki urais 2015

ibange

JF-Expert Member
Joined
Dec 31, 2010
Posts
1,543
Reaction score
553
Habari zinazoongoza gazeti la habari leo ni kwamba Zitto ndie mtanzania anayepewa nafasi kubwa zaidi kushinda urais 2015
Hili gazeti la wana CCM nimeshangaa kuandika habari hii ila nadhani wamepania kumpa kichwa ili ahame CHADEMA agawe chama. Sidhani kama Zitto anampita Dr Slaa hata kumkaribia
 
Non Sense...Habari Leo ni sawa na magazeti ya Udaku tu.
 
Habari zinazoongoza gazeti
la habari leo ni kwamba zitto ndie mtanzania anayepewa nafasi kubwa
zaidi kushinda urais 2015
Hili gazeti la wana ccm nimeshangaa kuandika habari hii ila nadhani
wamepania kumpa kichwa ili ahame chadema agawe chama. Sidhani kama zitto
anampita dr slaa hata kumkaribia

Hakuna jipya hapa... Mods fungeni huu uchafu wa ki-masalia...
 
Habari zinazoongoza gazeti la habari leo ni kwamba zitto ndie mtanzania anayepewa nafasi kubwa zaidi kushinda urais 2015
Hili gazeti la wana ccm nimeshangaa kuandika habari hii ila nadhani wamepania kumpa kichwa ili ahame chadema agawe chama. Sidhani kama zitto anampita dr slaa hata kumkaribia

propaganda zao hizo si umeona gazeti lenyewe Habari leo du
 
kwani Kigoma inajitenga ili iwe nchi? kama ni hivyo siwezi kupinga,
ni kweli Zitto ana nafasi kubwa ya kushinda urais wa Kigoma 2015...
 
gazeti hilo hilo lingemtaja bwana fulani kuwa hakamatiki kwa urais 2015 ungesikia baadh ya watu humu jamvini wakisema "habari leo wameanza kuona upepo wa mabadiliko" vigeu geu
 
Huu ndio mwanzo wa Zitto na masalia yake kutafuta namna ya kutafuta popularity ili baadaye ajitoe CHADEMA kwa kisingizio kuwa amenyimwa kugombea Urais ili apungu\ze kura za wapinzani. Akanushe habari haraka kama kweli hahusiki.

Habari leo sasa hivi halina tofauti na Gazeti la Uhuru linafanya kazi ya CCM wakati linaendeshwa kwa kodi zetu. Wanasheria mpo?
 
Hahahaha......unashindwa kuongoza jimbo unataka nchi?
Labda nchi ya mapanya.
kule Lushoto kulikuwa na mipanya inayotoa viroboto vinavyosababisha ugonjwa wa tauni miaka ya 1980s,
tumehangaika nayo hadi madokta toka ulaya walikuja wakaambulia mauti kumbe huku kulikuwa na mtaalamu wa kuangamiza panya... loh!
 
Habari zinazoongoza gazeti la habari leo ni kwamba zitto ndie mtanzania anayepewa nafasi kubwa zaidi kushinda urais 2015
Hili gazeti la wana ccm nimeshangaa kuandika habari hii ila nadhani wamepania kumpa kichwa ili ahame chadema agawe chama. Sidhani kama zitto anampita dr slaa hata kumkaribia
Sidhani kama nia yao ipo kwenye kumtaka ahame chadema. Bila shaka umewasikia akina Nape na Le Mutuz pia wakimsifia Zitto, lakini kwa imani yangu ni kwamba wanataka kuwachanganya CHADEMA ili wamteue Zitto kwenye nafasi ya Urais na kumwacha Slaa, na hilo litakuwa ni kosa la kiufundi litakalo iwezesha CCM kushinda kiurahisi. Hakuna lingine. CCM na washirika wake wote vikiwemo vyombo vyao vya habari vinamugwaya Slaa kwa sana. Kwa hiyo ni lazima watafute njia ya ziada ya kuiingiza CHADEMA mkenge ili wamuweke mtu ambaye ni rahisi kwao. Nilishasema hapo zamaini, ukiona mpinzani wako anakusifia, ujue wewe si lolote wala si chochote.
 
gazeti hilo hilo lingemtaja bwana fulani kuwa hakamatiki kwa urais 2015 ungesikia baadh ya watu humu jamvini wakisema "habari leo wameanza kuona upepo wa mabadiliko" vigeu geu

Laiti kama wangeandika hivyo wala kusingekucha kabla ya kupokea ya habari mpya kama si Mhariri wa gazeti hilo si raia basi amekutwa amevamiwa na majambazi usiku nyumbani kwake na wamemuua, na uchunguzi wa jambo hilo unaendelea. Chezea Ighondu weye!
 
Hizi ni propaganda,zitto achunguzwe coz yupo nyuma ya iyo habari
 
Back
Top Bottom