Yakobo 1:17 Kwake hakuna kubadilika wala kivuli cha kugeuka-geuka.
Malaki 3:6 Kwa kuwa mimi, BWANA, sina kigeugeu; ndio maana nyinyi hamkuangamizwa.
Zaburi 102:27 Lakini wewe U Yule yule, Na miaka yako haita koma.
Waraka Kwa Waebrania 6:17 - 18 Katika neno hilo Mungu, akitaka kuwaonyesha zaidi sana wairithio ile ahadi, jinsi mashauri yake yasivyoweza kubadilika, alitia kiapo katikati; ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo, tupate faraja iliyo imara, sisi tuliokimbilia kuyashika matumaini yale yawekwayo mbele yetu.