Dr Adam Francis
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 464
- 687
Kufuatia Press conference ya Askofu May 24, 2025 kuhusu utekaji, utesaji na mauaji, ambapo alidai huenda kipo kikundi kinachotenda mambo haya kwa maslahi ya mwanasiasa fulani, kumekuwa na mijadala mingi kitaifa yenye hisia mchanganyiko, huku chama chake kikimwona kuwa aliyepotoka.
Pamoja na mambo mengine, watanzania wataukumbuka mkutano mkuu wa CCM, May 30, 2025 kwa kutupatia msamiati mpya town, "Gwajimanization." uliopewa maana kutokukitenga chama na "majuzuhu" kwani "Mcheza ngoma si yake ataharibu." Bila shaka, hili lilikuwa ni jawabu kwa press ya bishop.
Kama tuijuavyo hulka ya bishop, June 1, 2025 kanisani kwake, miongoni mwa mengi aliyoyazungumza, mojawapo lilikuwa ni kutoa maana mpya ya "Gwajimanization" kuwa ni “Ujasiri wa kusema ukweli bila woga, hata kama ukweli huo unawaumiza walioko madarakani.” Maana ambayo kwakweli ndiyo inayoonekana kukubalika zaidi kwa sasa huku mtaani.
Kwaupande mwingine, Msajili wa asasi za kiraia kaona isiwe tabu, June 1, 2025, sio tu kalifutia usajili kanisa la bishop, bali pia polisi walilizingira kanisa la bishop, ikiwa ni hatua muhimu ya anti gwajimanization campaign, sio tu kukitenga chama na "majuzuhu", bali pia kuwatenga watanzania na "majuzuhu" chini ya falsafa ya "mcheza ngoma si yake, ataharibu"
Hapo ndipo tulipofika sasa! Kama gwajimanization ilikuwa popularity project, bishop kapata mileage, ila kama ilikuwa ni serious political agenda, ninawasiwasi bishop kapigwa ngwala. Watanzania wanasubiri kuona atafanya nini? Je, atakinukisha? Au ataufyata. Kwa hali ilivyo lolote laweza kutokea.
Hata hivyo namkumbusha bishop, "The skillful General subdues the enemy without fighting" Art of War by Sun Tzu, "It is dangerous to be right when the government is wrong.” Voltaire, French Enlightenment thinker of 18th century na "Never outshine you Master" The 48 Laws of Power by Robert Greene
Pamoja na mambo mengine, watanzania wataukumbuka mkutano mkuu wa CCM, May 30, 2025 kwa kutupatia msamiati mpya town, "Gwajimanization." uliopewa maana kutokukitenga chama na "majuzuhu" kwani "Mcheza ngoma si yake ataharibu." Bila shaka, hili lilikuwa ni jawabu kwa press ya bishop.
Kama tuijuavyo hulka ya bishop, June 1, 2025 kanisani kwake, miongoni mwa mengi aliyoyazungumza, mojawapo lilikuwa ni kutoa maana mpya ya "Gwajimanization" kuwa ni “Ujasiri wa kusema ukweli bila woga, hata kama ukweli huo unawaumiza walioko madarakani.” Maana ambayo kwakweli ndiyo inayoonekana kukubalika zaidi kwa sasa huku mtaani.
Kwaupande mwingine, Msajili wa asasi za kiraia kaona isiwe tabu, June 1, 2025, sio tu kalifutia usajili kanisa la bishop, bali pia polisi walilizingira kanisa la bishop, ikiwa ni hatua muhimu ya anti gwajimanization campaign, sio tu kukitenga chama na "majuzuhu", bali pia kuwatenga watanzania na "majuzuhu" chini ya falsafa ya "mcheza ngoma si yake, ataharibu"
Hapo ndipo tulipofika sasa! Kama gwajimanization ilikuwa popularity project, bishop kapata mileage, ila kama ilikuwa ni serious political agenda, ninawasiwasi bishop kapigwa ngwala. Watanzania wanasubiri kuona atafanya nini? Je, atakinukisha? Au ataufyata. Kwa hali ilivyo lolote laweza kutokea.
Hata hivyo namkumbusha bishop, "The skillful General subdues the enemy without fighting" Art of War by Sun Tzu, "It is dangerous to be right when the government is wrong.” Voltaire, French Enlightenment thinker of 18th century na "Never outshine you Master" The 48 Laws of Power by Robert Greene