Gwajima: Hakuna Sababu ya Kuteka Watu

Hamatan

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2020
Posts
7,424
Reaction score
17,204
Askofu Gwajima, mbunge wa CCM, na kiongozi wa Kanisa la Uzima na ufufuo amesema kuwa nchi haina haki, maisha ya mwanadamu hayathaminiwa. Akasema hakuna sababu ya kuteka watu. Akauliza ni kwa nini maisha ya mtanzania hayathaminiwi?

Ameendelea kusema kuwa mitungi yote ya gas tunayoiona, hakuna hata wa kampuni moja uliojazwa gas ya Tanzania. Akauliza, ni kwa nini?

Anasema kuwa nchi ina mapepo.

Najiuliza: hayo mapepo yapo kwa viongozi au watanzania wote? Hayo mapepo tutayaondoaje?

Hii nchi ni nani aliyeridhika na yanayoendelea? Maana wananchi wanalalamika (isipokuwa machawa), viongozi wa siasa wanalalamika (isipokuwa viongozi machawa), viongozi wa dini wanalalamika.

Kama sote tunalalamika, nani wa kuchukua hatua kuyaondoa tunayoyalalamikia?

Msikilize Gwajima:

Your browser is not able to display this video.
 
Mtu yeyote ambaye hajali Thamani ya Mtu usimwamini hata siku moja kwamba atachochea maendeleo kwenye nchi.
 
HAPANA usimwamini mwana CCM yyte yule.itakula kwako.
KAZI ni kipimo cha utu
 
Kumbe Wenzetu Mikocheni Mmeshaunganishwa Mabomba ya Gesi nyumba 480?

Mbona hamsemi?
 
Chaujanja. Wameanza leo kwani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…