Govt: No Foreign Terrorists in Ukerewe

Govt: No Foreign Terrorists in Ukerewe

nngu007

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2010
Posts
15,860
Reaction score
5,803
Tanzania Daily News (Dar es Salaam)


7 FEBRUARY 2013

Dodoma - THE government refuted claims that soldiers from neighbouring countries have entered the country and are terrorizing residents in Ukerewe.

The Minister for Defence and National Service, Mr Shamsi Vuai Nahodha, told the House yesterday that the said acts by alleged foreign soldiers are in fact a special joint operation against illegal fishermen on Lake Victoria conducted by fisheries officers from Tanzania, Kenya and Uganda.

Mr Nahodha was clarifying on allegations brought in Parliament by Ukerewe Member of Parliament, Mr Salvatory Machemli (Chadema) who said on Tuesday that soldiers from Kenya and Uganda were terrorizing people in his constituency. The minister cautioned Mr Machemli against such serious allegations that may harm neighbourly relations and even lead to confrontation between states.

"These are serious allegations and I advise that as human beings we should let wisdom prevail before we make such comments. Careless talk could be detrimental to the country's peace and security," he said. That prompted reaction from Mr Machemli who stood his ground and said that his allegations were true and that there are several people who have been injured following acts of violence by foreign soldiers.


Mr Nahodha told Parliament that Tanzania, Kenya and Uganda which share borders on Lake Victoria have agreed to conduct joint operations to combat environmental degradation including illegal fishing on the lake. The agreement was reached through the Lake Victoria Fisheries Organization and members are currently conducting joint operations in Mwanza Region which was preceded by training for officers.


"On January 31 fisheries officers launched an operation on Ukerewe Island that lasted for seven days. The operation was aimed at netting illegal fishermen and the officers used the assistance of the police force," he said.


He said that on February 4 this year a group of people in Buzegwe in the island wanted to block the operation which resulted in police officers using teargas to disperse people and the operation went on smoothly without affecting residents.

FEB 20, 2013
Hofu ya Al Qaeda Ukerewe

*Wananchi wakihusisha chuo na ugaidi
*Mbunge ataharuki, aandaa hoja binafsi
*Mkuu wa Mkoa, DC wakwepa kunena


HOFU ya kuwapo kwa magaidi wa mtandao wa Al- Qaeda, imetanda katika Wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza, baada ya kuvuja kwa taarifa za kuanzishwa kwa chuo kimoja cha kidini kinachohofiwa kutoa mafunzo yenye mwelekeo wa kigaidi visiwani humo.

Taarifa hizo zimeeleza kuwa chuo hicho kinajulikana kwa jina la Markaz, Aljazeera na kimeanzishwa kwa ufadhili wa raia wa kigeni ambao ni waumini wa dini ya Kiislamu.

Makundi yanayotajwa kufadhili uendeshaji wa chuo hicho ni Al-Qaeda na Al shabab yanayoaminika kuwa na mtandao mkubwa wa ugaidi duniani.

Uchunguzi uliofanywa na Mtanzania Jumatano wilayani Ukerewe, umebaini kuwa chuo cha Markaz kinatoa mafunzo kwa watu wa rika mbalimbali yenye mwelekeo wa kujihami na kushambulia kama Karate na Kung-fu.

Aidha, taarifa nyingine za kiuchunguzi ambazo gazeti hili lilidokezwa na wakazi wa kisiwani humo walioonyesha wasiwasi wa kuwepo kwa chuo hicho, zilidai kuwa, aina nyingine ya mafunzo yanayotolewa katika chuo hicho na kushambuliana kwa silaha aina ya jambia.

Uchunguzi ulibaini zaidi kuwa, wanafunzi katika chuo hicho ni watoto wenye umri wa kati ya miaka saba hadi 10 na pia kuna wanafunzi vijana na watu wazima.

Baadhi ya wakazi wa wilayani humo waliopata kufanya kazi katika chuo hicho, waliliambia gazeti hili kuwa chuo hicho kimekuwa kikipokea mizigo ya aina mbalimbali, ikiwa imefungwa kwenye maboksi ambayo katika udadisi wao walibaini kuwa, baadhi ya bidhaa zinazokuwa kwenye shehena hizo ni kanzu, seti za televisheni, vitabu na silaha za aina mbalimbali.

Walidai kuwa, walianza kukitilia mashaka chuo hicho baada ya kubaini kinapokea silaha katika baadhi ya mizigo yake.

Mbali ya hilo, wakazi hao walilieleza gazeti hili kwamba aina ya wageni wanaoingia na kutoka visiwani humo kwa minajili ya kukitembelea chuo hicho, ni jambo jingine ambalo limekuwa likiwafanya wazidi kukitilia shaka chuo hicho.

Kwa mujibu wa wakazi hao, wageni hao wamekuwa wakiingia kisiwani kwa njia ya mitumbwi wakipita katika njia za panya nyakati za usiku.

Wageni hao kwa mujibu wa wakazi wa eneo hilo la Nansio ni wale wanaodaiwa na kuaminika kutoka katika nchi jirani za Kenya na Uganda ambazo mipaka ya ziwa Victoria inapita.

Wafanyabiashara wanaojihusisha na usafirishaji abiria waliozungumza na gazeti la Mtanzania Jumatano walieleza kuwa, wageni wanaowapakia kuwapeleka chuo cha Markaz au maeneo mengine ya kisiwa hicho huwalazimisha kuondoa misalaba waliyoivaa shingoni au waliyotundika katika magari na pia huwataka wazime redio katika magari yao.

Hofu hiyo ya wakazi wa Nansio ilisababisha gazeti hili kumtafuta Mbunge wa Ukerewe, Salvatory Machemli (Chadema) ambaye naye alikiri kulifahamu jambo hilo.

Akizungumza kupitia simu yake ya kiganjani, Machemli alisema chuo hicho kinatoa mafunzo ambayo wakazi wake wanayahusisha na matendo ya kigaidi.

Mbunge huyo alisema hofu zaidi kuhusu chuo hicho ni kuwapo kwa taarifa zinazodai kwamba, baadhi ya wanachuo ambao wamewahi kupata mafunzo chuoni wanatajwa kuwa wanachama wa makundi ya kigaidi ya Al Qaeda na Al-Shabab.

Kwa mujibu wa mbunge huyo, miongoni mwa hatua ambazo amepata kuzichukua ili kutafuta majibu ya wasiwasi wa wananchi wa Ukerewe ni pamoja na kumsaka mmoja wa watu anayekijua chuo hicho.

"Ni kweli tuna wasiwasi na hatuoni kazi ya umma kinachojihusisha nacho. Niliwahi kumuuliza Diwani wa Kata ya Nansio, Sheikh Ramadhani Mazige (CCM) kuhusu uhalali wa kuwapo kwa chuo hicho kwa sababu alikuwa akisimamia ujenzi wake na nikashauri juu ya umuhimu wa kubadili aina ya mafunzo yanayofundishwa chuoni hapo na jibu lake lilikuwa wenye chuo hawataki.

Alipoulizwa iwapo anawafahamu wamiliki wa chuo hicho, alikana kuwatambua kwa kueleza kuwa, jitihada zake za kuwafahamu hazikufanikiwa baada ya Diwani Mazege kukataa kuwataja.

Machemli alisema kuwa, amepanga kulifikisha suala hilo kama hoja binafsi kwenye Baraza la Madiwani ili kuomba kibali cha kutembelea chuo hicho kuona shughuli zinazofanyika na kwamba iwapo atakwamishwa, atalifikisha suala hilo katika ngazi za juu.

Akizungumza kuhusu raia wa kigeni wanaopitia njia za panya kwa usafiri wa mitumbwi nyakati za usiku kufika chuoni hapo, Machemli alisema hilo hawezi kulipinga.

Kwa mujibu wa Machemli, jiografia ya visiwa vya Ukerewe inavifanya viwe wazi kuhusu mipaka yake na kwamba jambo hilo alipata kulizungumza bungeni ingawa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha alimpuuza.

"Nilizungumza katika mkutano uliopita wa Bunge kuhusu mipaka ya Ukerewe kuwa wazi sana, nililalamika kwamba, wanajeshi wa Kenya na Uganda wanakuja hadi katika kisiwa hicho kufanya mazoezi yake na kuondoka, lakini nashangaa waziri akanipuuza," alilalamika Machemli.

Alipotafutwa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ernest Mangu kwa ajili ya kuzungumzia juu ya hofu hiyo, alisema anaomba apewe muda kwa sababu yeye ni mgeni mkoani humo na huu mwezi wa pili akiwa katika kituo chake kipya cha kazi, hivyo yapo mengi ambayo hayafahamu.

Hata hivyo, Mangu aliliahidi gazeti hili kufuatilia juu ya suala hilo na kulitolea ufafanuzi baadaye.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Mary Tesha alikana kufahamu chochote na badala yake akahoji sababu za mwandishi kumtafuta wakati tayari suala hilo lilisharipotiwa katika gazeti hili hivi karibuni.

Kumekuwa na tetesi za kuwepo kwa vikundi vinavyojihusisha na utoaji mafunzo ya kigaidi hapa nchini, vikiwa vimejificha katika mwamvuli huku lengo halisi likiwa kuhatarisha amani ya kitaifa.

Tayari Rais Jakaya Kikwete amekwishaagiza kusakwa kwa makundi yenye mwelekeo huo yanayohisiwa kuhusika na machufuko na mauaji hapa nchini, wakati akitoa salamu za pole baada ya tukio la kuuawa kinyama kwa Padre wa Kanisa Katoliki Evaritus Mushi huko visiwani Zanzibar.


CHANZO: Mtanzania | Feb 20, 2013
 

This is SCARY if IT IS TRUE or GOING to HAPPEN... OUR Leaders Prefers TRIPS OVERSEAS never care what's HAPPENNING WITHING OUR BORDERS!!!!
 
Wakuu, nimeshtushwa sana na habari ya kiuchunguzi iliyoandikwa leo katika gazeti la Mtanzania, page 13, kuhusu kuwapo kwa chuo kinachofadhiliwa na Al-Shabab na kutoa mafunzo kwa wapigananji wao, kisiwani Ukerewe, mkoani Mwanza. Kwa maelezo ya mwandishi, Chuo kinafahamika hata kwa vyombo vya dola wilayani humo.

Habari hii ya kiuchunguzi ni ukurasa mzima imeandikwa na mwandishi anayetumia jina la Ratifa Baranyikwa. Stori ni ndefu na bado itaendelea kutolewa katika matoleo yajayo.

Iwapo jambo hili ni kweli, basi tuemefikia mahala pabaya mno.

Hii ni habari nzito, ni vema ikaachwa jamvini watu wajue na kuchangia.
 
Wakuu, nilipost hii habari muda mfupi uliopita, bahati mbaya sijaiona.

Kwa mujibu wa makala ya kiuchunguzi katika gazeti la leo, Mtanzania, page 13, kundi la kigaidi la Al- Shabab wanamiliki na kuendesha chuo chao cha mafunzo kwa mambo wanayoyafanya huko Ukerewe, Mkoani Mwanza. Baadhi ya viongozi Wilayani wametajwa kwa majina kushirikiana na hawa Al-Shabab.

Wanapokea wageni ambao inalelekea wanaingia kwa kificho kupitia ziwani kutokea Kenya, Somalia, etc.

Vyombo vya dola wilayani, ikiwamo polisi wanalifahamu hili. Hata wananchi wanakiri kuwapo kwa hawa jamaa.

Mwandishi wa makala amejitambulisha kwa jina la Ratifa Baranyikwa, amendika makala ya kiuchunguzi na kuweka picha ya chuo hicho.

Habari hii ni ukurasa mzima. Itaendelea kuwa inatolewa katika matoleo yajayo.

Iwapo habari hii ni kweli, basi tumefika mahala pabaya mno. Lazima vyombo vya dola viamke sasa au wanachi wendelee kujitetea wenyewe ili Nchi isiangamie.

Hope habari hii itaachwa ikae jamvini, wadau wafahamu na kuchangia.
 
Wakuu, katika gazeti la leo la Mtanzania, ukurasa wa 13, zipo za habari za kuwapo kwa chuo mafunzo cha Al- Shabab wilayani Ukerewe, Mkoani Mwanza.

Habari hizi za kiuchunguzi zimeandikwa na mwandishi anayejitambilisha kwa jina la Ratifa Baranyikwa. Ukurasa mzima unazungumzia habari hizi yakiwamo maelezo kutoka kwa watu kisiwani humo wakikiri kuwapo kwa jamaa hawa, viongozi wa Halmashauri kufahamu, picha na mengineyo.

Aidha, inaelezwa namna kambi hiyo ya mafunzo inavyopokea wageni kupitia njia za siri wakipitia ziwani, ziwa Victoria, wakitokea Nchi jirani, ambazo mwandishi amezitaja.

Al- Shabab ni kundi hatari linalojihusisha na mambo ya ugaidi duniani. Kundi hili hatari linawindwa duniani kote na Mataifa ya Magharibi, hususani Ulaya na Marekani, ambayo yako mstari wa mbele katika vita vya kuliwinda na kulitokomeza.

Wadau wa JF ambao, kanda ya ziwa na wengine wanaofahamu, habari hizi mnazifahamu?Ni kweli kundi hili limepata maficho yake Tanzania?
 
Pia hapa Dar es Salaam pale Vingunguti kuna Chuo ambacho kilisajiliwa kwa ajili ya kutunza WATOTO YATIMA nacho kimekuwa na mafunzo yasiyotia shaka ni kwa ajili ya kuwafunza watoto hao yatima masuala ya KIGAIDI.

Usalama wa Taifa acheni kudharau taarifa mnazopata kwa njia yoyote iwe Radio, TV, Magazeti, Taarifa toka wananchi, hata michoro MBONA MPO KAMA HAMPO au na nyie mna agenda za KIUDINI???
 
sasa kutumia kung fu na majambia ndio ugaidi mbona sehemu nyingi hivyo vitu vipo tena hasa kwenye misikiti ambayo ina vyuo wenyewe wanafanya mazoezi nyie mnasema ni ugaidi watu waache kuzusha mambo kama ni hivyo hata GIM zifungwe maana ni ugaidi..........magaidi wanatumia mabomu sio majambia
 
Matatizo ya kuondoa madaraka kwa nyumba kumi kumi ndio haya. Enzi za mwal haya yasingekuwepo kila mgeni anayeingia mtaani au katika jamii lazima aolozeshwe kwa tencell leader. Sasa hivi magaidi wanaingia hovyo hovyo nchini na tunaishi nao bila kuwagundua.
 
sasa kutumia kung fu na majambia ndio ugaidi mbona sehemu nyingi hivyo vitu vipo tena hasa kwenye misikiti ambayo ina vyuo wenyewe wanafanya mazoezi nyie mnasema ni ugaidi watu waache kuzusha mambo kama ni hivyo hata GIM zifungwe maana ni ugaidi..........magaidi wanatumia mabomu sio majambia

Kama jamaa anachosema ni kweli basi mwenzetu hujuiunaongea nini!!!

Hujawahi kuona video za al quaeda huko Pakstani?? Unafikiri ugaidi nizaidi ya kutengeneza mabomu. Kuna mafunzo mengine kama ya self defense na combat huwa yanatolewa!!!

 
Kwanini haya yanakuja hadharani na kila muhusika anakimbia kuelezea? wanapaswa kutuambia ipasavyo katika ukweli wake. hivi vyombo vya usalama havioni, wanaokagua mizigo wako wapi? uhamiaji wako? vitu vingine haviingii akilini hata kidogo...
 
Dah kweli Propaganda ni hatari Hainiingii akilini eti Mizigo(Maboksi) ya Silaha yanaingizwa Je Police Jeshi Usalama wako wapi ??
Halafu eti wageni huingia Usiku na Mitumbwi Je Kikosi cha Marine kinafanya kazi Gan
Choko choko Mchokoe Pweza.........,!!!!!!!!!!!!!
 
Idem, Kabwoba Islamic Centre, enroute to Mtukula.
 
Pia hapa Dar es Salaam pale Vingunguti kuna Chuo ambacho kilisajiliwa kwa ajili ya kutunza WATOTO YATIMA nacho kimekuwa na mafunzo yasiyotia shaka ni kwa ajili ya kuwafunza watoto hao yatima masuala ya KIGAIDI.

Usalama wa Taifa acheni kudharau taarifa mnazopata kwa njia yoyote iwe Radio, TV, Magazeti, Taarifa toka wananchi, hata michoro MBONA MPO KAMA HAMPO au na nyie mna agenda za KIUDINI???

Tuwasaidie hawa jamaa kufanya ka zao ( if they are not part of the deal any way). Kwa nyongeza tu, wale vijana kwa makundi wakisaidiwa na bakwata kwenda uarabuni kwa ' ajira' nao fuatilia nyendo zao. Of course si baya kutafuta kazi huko but always avoid hidden agenda.
 
Utawala wetu umepwaya na hawaitakii Tanzania, ikiwa waziri Nahodha anapuuza jambo hili wakati mbegu za udini zinastawi kwa kasi ya ajabu, watanzania kwa umoja wetu tuwakatae hawa watawala na hivyo vyuo vinavyotia shaka. Hivi Waziri Nahodha hajui hii kitu kweli, au kwa kuwa ni cha kidini ndiyo maana amekaa kimya? Aibu kwa Taifa langu Tz.
 
Back
Top Bottom