edcv
Member
- Feb 22, 2012
- 48
- 23
Nimesikia sana usemi huu 'free is expensive' binafsi sijaufuatilia sana ila kwa uzoefu wangu huohuo mdogo nimeona kuna kaukweli. Ila sasa nikiangalia maisha yangu naona kama Mungu, wazazi, ndugu na marafiki wamenipa vingi sana vya bure ambavyo ndio haswa msingi wa maisha yangu. Kwa sababu hiyo nikiangali jinsi baadhi ya hawa walivyoteseka ili mimi nipate hivyo vitu, naamini kwamba Mungu ndiye ambaye anafanya tuweze kula kesho pamoja na kwamba tunaamini fedha zetu ndo kila kitu. Huwa najitahidi sana kuuendeleza huu msemo wa "Good things are always free". Sasa swali langu kwenu wanajamii, Ni kwanini mtu anafanya ngono, na kuanzia anaanza mpaka anamaliza yuko na akili zake. Mwanamke anapata mimba- wanasema ilikuwa accident kwa hiyo tuitoe. Kwa nini mtoto ndio alipe uzembe wenu kwa maisha yake? Na sisi wanajamii tunawashauri bila hata kuogopa dhamiri zetu zinavyotukataza! Why do we embrace these bloodthirsty murderers?