Global Positioning System (kifupi: GPS) ni kitu gani?

Global Positioning System (kifupi: GPS) ni kitu gani?

Mwanamkiwi

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2019
Posts
2,023
Reaction score
2,402
Global Positioning System (kifupi: GPS, kwa maana: Mfumo wa mwongozo kote duniani) ni mfumo wa kupima na kutambua kimakini kila mahali duniani ukitumia satelaiti.

Misingi
Satelaiti kama 30 zinazunguka Dunia muda wote kwenye njia maalum. Zinakaa kilomita 20,000 - 25,000 juu ya uso wa ardhi na kutumia mnamo saa 12 kwa kuzunguka Dunia. Zinatuma muda wote ishara za redio duniani. Kipokezi duniani kinapokea ishara hizi. Majiranukta za mahali pa satelaiti hujulikana kwa kila dakika na kila sekunde, maana zinatembea kwenye njia thabiti. Kipokezi kikiwa na ishara redio za angalau satelaiti tatu kinaweza kukadiria majiranukta ya mahali pake penyewe kwa umakini. Kama kipokezi kinapata ishara ya satelaiti nyingi zaidi umakini huongezeka.

Hali halisi umakini wa GPS unategemea kifaa ulicho nacho. Kama si vizuri tofauti za mita 100 zinaweza kuonyeshwa. Matumizi katika mazingira ya majengo marefu, ndani ya majengo au penye milima mikali inaathiri umakini pia kwa sababu vizuizi hivi vinaweza kuzuia ishara ya satelaiti moja au zaidi.

Vifaa vya GPS havihitaji intaneti kwa sababu ishararedio za satelaiti zinapokelewa moja kwa moja. Hata hivyo vifaa vingi hutumia intaneti pia kwa kuborsha huduma.

Mwongozo wa safari
Kifaa cha GPS kwenye gari kinaonyesha ramani pamoja na njia ya kuelekea kwenye lengo

Vipokezi vya GPS vinapatikana katika simujanja na vifaa vingine vinavyotumiwa katika magari, eropleni na meli. Vifaa hivi ni kama kompyuta ndogo ambavyo vinatumia pia ramani ya nchi au Dunia pamoja na habari za barabara na hali zao. Kwa njia hii programu za GPS zinazounganishwa na kipokezi inaweza kukadiria muda unahitajika kufika kutoka mahali ulipo hadi mahali pengine ama kwa miguu au kwa gari kwa kutumia kasi ya wastani. Pale ambako ratiba za usafiri wa umma zinapatikana kifaa kinaonyesha pia muda wa usafiri kwa treni au basi. Ilhali majiranukta ya kifaa chenyewe kinajulikana muda wote, ni lazima kupata majiranukta za mahali unapolenga. Hapa mtumiaji anaweza kudokeza kwenye ramani anapoenda au kuingiza anwani kamili maana programu za GPS huwa na data nyingi zenye majina na majiranukta za barabara, mitaa na hata majengo maalumu.

Mifumo mbalimbali ya GPS
Marekani ilikuwa nchi ya kwanza iliyopeleka satelaiti za GPS angani na mwanzoni shabaha ilikuwa kijeshi. Baadaye makampuni ya kiraia yaliruhusiwa pia kutumia data na ishara za redio kutoka satelaiti zinapatikana sasa kwa kila mtu mwnye kifaa. Mfumo wa Marekani unaitwa "NAVSTAR GPS", upo tangu 1985 na tangu mwaka 2000 umepatikana pia kwa watumiaji raia. Lakini ishara zake hazipatikani kwa umakini mkuu kwa vifaa vya watu raia ambao huchezacheza kwa mita 10 hivi. Kwa vifaa vya kijeshi vya Marekani umakini unafikia sentimita ambao ni muhimu kwa kulenga silaha.

Nchi nyingine zimejenga pia mifumo yao kwa sababu hawataki kutegemea GPS ya Marekani inayoweza kuzimishwa muda wote. Hivyo kuna mifumo ifuatayo:
  • GLONASS ya Urusi
  • Galileo ya Umoja wa Ulaya (mfumo wa pekee usio chini ya usimamizi wa kijeshi)
  • Beidou ya China
Kila mfumo unatumia satelaiti zake za pekee angalau 24, hadi 32. Jina la Kiingereza kwa jumla ya mifumo hii ni "global navigation satellite system " (GNSS) lakini jina la GPS limekuwa kawaida katika nchi nyingi kwa zote.
1120641
Satelaiti za GPS zinazozunguka Dunia; rangi ya buluu inaonyesha kupatikana kwa satelaiti kwa kipokezi kwenye kaskazini y Dunia, rangi nyekundu inaonyesha satelaiti zinazopotea nyuma ya upeo ambako hazipokelewi tena na kipokezi
 

Attachments

  • 1559908391406.png
    1559908391406.png
    9.6 KB · Views: 46
Global Positioning System (kifupi: GPS, kwa maana: Mfumo wa mwongozo kote duniani) ni mfumo wa kupima na kutambua kimakini kila mahali duniani ukitumia satelaiti.

Misingi
Satelaiti kama 30 zinazunguka Dunia muda wote kwenye njia maalum. Zinakaa kilomita 20,000 - 25,000 juu ya uso wa ardhi na kutumia mnamo saa 12 kwa kuzunguka Dunia. Zinatuma muda wote ishara za redio duniani. Kipokezi duniani kinapokea ishara hizi. Majiranukta za mahali pa satelaiti hujulikana kwa kila dakika na kila sekunde, maana zinatembea kwenye njia thabiti. Kipokezi kikiwa na ishara redio za angalau satelaiti tatu kinaweza kukadiria majiranukta ya mahali pake penyewe kwa umakini. Kama kipokezi kinapata ishara ya satelaiti nyingi zaidi umakini huongezeka.

Hali halisi umakini wa GPS unategemea kifaa ulicho nacho. Kama si vizuri tofauti za mita 100 zinaweza kuonyeshwa. Matumizi katika mazingira ya majengo marefu, ndani ya majengo au penye milima mikali inaathiri umakini pia kwa sababu vizuizi hivi vinaweza kuzuia ishara ya satelaiti moja au zaidi.

Vifaa vya GPS havihitaji intaneti kwa sababu ishararedio za satelaiti zinapokelewa moja kwa moja. Hata hivyo vifaa vingi hutumia intaneti pia kwa kuborsha huduma.

Mwongozo wa safari
Kifaa cha GPS kwenye gari kinaonyesha ramani pamoja na njia ya kuelekea kwenye lengo

Vipokezi vya GPS vinapatikana katika simujanja na vifaa vingine vinavyotumiwa katika magari, eropleni na meli. Vifaa hivi ni kama kompyuta ndogo ambavyo vinatumia pia ramani ya nchi au Dunia pamoja na habari za barabara na hali zao. Kwa njia hii programu za GPS zinazounganishwa na kipokezi inaweza kukadiria muda unahitajika kufika kutoka mahali ulipo hadi mahali pengine ama kwa miguu au kwa gari kwa kutumia kasi ya wastani. Pale ambako ratiba za usafiri wa umma zinapatikana kifaa kinaonyesha pia muda wa usafiri kwa treni au basi. Ilhali majiranukta ya kifaa chenyewe kinajulikana muda wote, ni lazima kupata majiranukta za mahali unapolenga. Hapa mtumiaji anaweza kudokeza kwenye ramani anapoenda au kuingiza anwani kamili maana programu za GPS huwa na data nyingi zenye majina na majiranukta za barabara, mitaa na hata majengo maalumu.

Mifumo mbalimbali ya GPS
Marekani ilikuwa nchi ya kwanza iliyopeleka satelaiti za GPS angani na mwanzoni shabaha ilikuwa kijeshi. Baadaye makampuni ya kiraia yaliruhusiwa pia kutumia data na ishara za redio kutoka satelaiti zinapatikana sasa kwa kila mtu mwnye kifaa. Mfumo wa Marekani unaitwa "NAVSTAR GPS", upo tangu 1985 na tangu mwaka 2000 umepatikana pia kwa watumiaji raia. Lakini ishara zake hazipatikani kwa umakini mkuu kwa vifaa vya watu raia ambao huchezacheza kwa mita 10 hivi. Kwa vifaa vya kijeshi vya Marekani umakini unafikia sentimita ambao ni muhimu kwa kulenga silaha.

Nchi nyingine zimejenga pia mifumo yao kwa sababu hawataki kutegemea GPS ya Marekani inayoweza kuzimishwa muda wote. Hivyo kuna mifumo ifuatayo:
  • GLONASS ya Urusi
  • Galileo ya Umoja wa Ulaya (mfumo wa pekee usio chini ya usimamizi wa kijeshi)
  • Beidou ya China
Kila mfumo unatumia satelaiti zake za pekee angalau 24, hadi 32. Jina la Kiingereza kwa jumla ya mifumo hii ni "global navigation satellite system " (GNSS) lakini jina la GPS limekuwa kawaida katika nchi nyingi kwa zote.
View attachment 1120641Satelaiti za GPS zinazozunguka Dunia; rangi ya buluu inaonyesha kupatikana kwa satelaiti kwa kipokezi kwenye kaskazini y Dunia, rangi nyekundu inaonyesha satelaiti zinazopotea nyuma ya upeo ambako hazipokelewi tena na kipokezi
Naomba unifahamishe utaratibu wa kufungiwa hiyo GPS kwenye simu yangu ili ikiibiwa au kupotea niweze kuipata
 
Naomba unifahamishe utaratibu wa kufungiwa hiyo GPS kwenye simu yangu ili ikiibiwa au kupotea niweze kuipata
Ninavyojua ni tofauti kwa simu mbalimbali. Tumia google uitafute kwa simu yako.

Kwanza utambue namba ya IMEI ya simu yako (uifungue na andika mahali fulani kwenye karatasi unayoweka mahali utakapokumbuka - si "namba ya simu", ni namba ya simcard , kama mwizi si hodari sana polisi inaweza kujua mahali pake takriban , maana wataona iko katika seli gani ya mtandao wa kampuni yako..) --
Pili utumie akili ya kawaida kwa kufuata ushauri huu:
Tatu kama ni Android, ushauri huu:
Ushauri wa nyongeza:
Apps zinazoweza kusaidia (kama mwizi si hodari):
 
Naomba unifahamishe utaratibu wa kufungiwa hiyo GPS kwenye simu yangu ili ikiibiwa au kupotea niweze kuipata
Ninavyojua ni tofauti kwa simu mbalimbali. Tumia google uitafute kwa simu yako.

Kwanza utambue namba ya IMEI ya simu yako (uifungue na andika mahali fulani kwenye karatasi unayoweka mahali utakapokumbuka - si "namba ya simu", ni namba ya simcard , kama mwizi si hodari sana polisi inaweza kujua mahali pake takriban , maana wataona iko katika seli gani ya mtandao wa kampuni yako..) --
Pili utumie akili ya kawaida kwa kufuata ushuri huu:
Tatu kama ni Android, ushauri huu:
Ushauri wa nyongeza:
Apps zinazoweza kusaidia (kama mwizi si hodari):
 
Geographical Information System.. Nimefarijika kukutana nayo hapa jukwaani.
 
Global Positioning System (kifupi: GPS, kwa maana: Mfumo wa mwongozo kote duniani) ni mfumo wa kupima na kutambua kimakini kila mahali duniani ukitumia satelaiti.

Misingi
Satelaiti kama 30 zinazunguka Dunia muda wote kwenye njia maalum. Zinakaa kilomita 20,000 - 25,000 juu ya uso wa ardhi na kutumia mnamo saa 12 kwa kuzunguka Dunia. Zinatuma muda wote ishara za redio duniani. Kipokezi duniani kinapokea ishara hizi. Majiranukta za mahali pa satelaiti hujulikana kwa kila dakika na kila sekunde, maana zinatembea kwenye njia thabiti. Kipokezi kikiwa na ishara redio za angalau satelaiti tatu kinaweza kukadiria majiranukta ya mahali pake penyewe kwa umakini. Kama kipokezi kinapata ishara ya satelaiti nyingi zaidi umakini huongezeka.

Hali halisi umakini wa GPS unategemea kifaa ulicho nacho. Kama si vizuri tofauti za mita 100 zinaweza kuonyeshwa. Matumizi katika mazingira ya majengo marefu, ndani ya majengo au penye milima mikali inaathiri umakini pia kwa sababu vizuizi hivi vinaweza kuzuia ishara ya satelaiti moja au zaidi.

Vifaa vya GPS havihitaji intaneti kwa sababu ishararedio za satelaiti zinapokelewa moja kwa moja. Hata hivyo vifaa vingi hutumia intaneti pia kwa kuborsha huduma.

Mwongozo wa safari
Kifaa cha GPS kwenye gari kinaonyesha ramani pamoja na njia ya kuelekea kwenye lengo

Vipokezi vya GPS vinapatikana katika simujanja na vifaa vingine vinavyotumiwa katika magari, eropleni na meli. Vifaa hivi ni kama kompyuta ndogo ambavyo vinatumia pia ramani ya nchi au Dunia pamoja na habari za barabara na hali zao. Kwa njia hii programu za GPS zinazounganishwa na kipokezi inaweza kukadiria muda unahitajika kufika kutoka mahali ulipo hadi mahali pengine ama kwa miguu au kwa gari kwa kutumia kasi ya wastani. Pale ambako ratiba za usafiri wa umma zinapatikana kifaa kinaonyesha pia muda wa usafiri kwa treni au basi. Ilhali majiranukta ya kifaa chenyewe kinajulikana muda wote, ni lazima kupata majiranukta za mahali unapolenga. Hapa mtumiaji anaweza kudokeza kwenye ramani anapoenda au kuingiza anwani kamili maana programu za GPS huwa na data nyingi zenye majina na majiranukta za barabara, mitaa na hata majengo maalumu.

Mifumo mbalimbali ya GPS
Marekani ilikuwa nchi ya kwanza iliyopeleka satelaiti za GPS angani na mwanzoni shabaha ilikuwa kijeshi. Baadaye makampuni ya kiraia yaliruhusiwa pia kutumia data na ishara za redio kutoka satelaiti zinapatikana sasa kwa kila mtu mwnye kifaa. Mfumo wa Marekani unaitwa "NAVSTAR GPS", upo tangu 1985 na tangu mwaka 2000 umepatikana pia kwa watumiaji raia. Lakini ishara zake hazipatikani kwa umakini mkuu kwa vifaa vya watu raia ambao huchezacheza kwa mita 10 hivi. Kwa vifaa vya kijeshi vya Marekani umakini unafikia sentimita ambao ni muhimu kwa kulenga silaha.

Nchi nyingine zimejenga pia mifumo yao kwa sababu hawataki kutegemea GPS ya Marekani inayoweza kuzimishwa muda wote. Hivyo kuna mifumo ifuatayo:
  • GLONASS ya Urusi
  • Galileo ya Umoja wa Ulaya (mfumo wa pekee usio chini ya usimamizi wa kijeshi)
  • Beidou ya China
Kila mfumo unatumia satelaiti zake za pekee angalau 24, hadi 32. Jina la Kiingereza kwa jumla ya mifumo hii ni "global navigation satellite system " (GNSS) lakini jina la GPS limekuwa kawaida katika nchi nyingi kwa zote.
View attachment 1120641Satelaiti za GPS zinazozunguka Dunia; rangi ya buluu inaonyesha kupatikana kwa satelaiti kwa kipokezi kwenye kaskazini y Dunia, rangi nyekundu inaonyesha satelaiti zinazopotea nyuma ya upeo ambako hazipokelewi tena na kipokezi
Mkuu Naomba utuwekee na update za kuhama kwa North Magnetic Pole hivi karibuni kwani imehama kwa kiasi ambacho hakikutarajiwa na ina athari kwenye GPS

Km unataarifa zaidi
 
Mkuu Naomba utuwekee na update za kuhama kwa North Magnetic Pole hivi karibuni kwani imehama kwa kiasi ambacho hakikutarajiwa na ina athari kwenye GPS

Km unataarifa zaidi
Ncha sumaku kuhama kidogo ni kawaida. Kama ni zaidi sioni itatuhusu. Maana simu yako na GPS ndani yake hazitegemei ncha sumaku wala upimaji wa uga sumaku lakini ishara redio kutoka satelaiti za GPS. Naona ishara hizi (na umakini wa data zinazowasilishwa kwa GPS) kama zinaathiriwa na mabadiliko ya uga sumaku (na mahali pa ncha sumaku), basi sisi watumiaji wadogo na simujanja zetu ni shida dogo. Maana usafiri kwa ndege na kwa meli wote zinategemea GPS siku hizi.
Kwa hiyo wanaoendesha GPS watalazimishwa kunyosha data zao na kusambaza update.
Hapo sina wasiwasi.
 
Mkuu umenifurahisha na hichi kiswahili chako nyoofu kabisa.

Binafsi ningeapata shida sana kuizungumzia GNSS kwa lugha ya kiswahili.

Lakini pia naombo nisahihishe kitu kimoja kwamba katika utawala Wa George Bush aliruhusu rasmi GPS kutumika for civilian purposes pia censorship ya signals iliondolewa hapo baadae kidogo toka miaka ya 2000s kwahio sahizi tunapata usahihi Wa kimaeneo ( positional accuracy ) up to less than a centimetre kulingana na strength ya kifaa chako na muda Wa observation

Kwa hizi za simu siku hizi zimeimprove up to less than a metre mkuu

Kwa zile paid signals ( commercial). Kama ambazo zinapatikana kwenye specialized GNSS receivers kama za leica,ashtec,Trimble, Pentax na nyingine depending on time and other mitigating factors usahihi wao unaweza kwenda hadi less than a centimetre.
 
Back
Top Bottom