Global Imperialism on the rise!

Global Imperialism on the rise!

Kama hukuwa unajua basi ujue kuwa Marekani hayupo kwa sasa kwenye mashambulizi ya Libya, alishajitoa upo hapo?

Mkuu tazama mlolongo wa matukio yote.
Huu ukoloni mamboleo unarudi kwa kasi sana, na kuwepo au kutokuwepo na Marekani katika ACTUAL attacks hakuondoi dhamira ya nchi za magharibi kutaka kuitawala Libya na mafuta yake.
Naungana na only83 katika kuchambua suala zima.
Precedence iliyowekwa na nchi za magharibi ni mbaya sana kwa nchi za dunia ya 3.
 
Hali inayoendelea Libya ni kati ya vitu vinavyotakiwa kupingwa na kila mwafrika mpenda mapinduzi na anayelipenda bara hili kwa dhati.....Baada ya azimio la baraza la usalama la UN kupitisha kuilinda anga ya Libya ili Gaddafi asilitumie kufanya mashambulizi dhidi ya waasi wengi tulichukulia jambo hili kama ni sehemu ya kutafuta suluhu ya kudumu huko Libya.Chakushangaza kinachofanyika huko Libya ni mataifa ya magharibi yakiongozwa na Marekani kuitumia anga hiyo kumng'oa Gaddafi.Kuna nchi nyingi sana zinamatatizo ya kisiasa lakini sijwai sikia nchi hizi zikipeleka majeshi.Angalia Somalia,Ivory Coast nk kama sio agenda ya siri inaendelea ni nini? kama sio walikuwa wanamtafuta Gaddafi muda mrefu kwa hiyo kaingia kwenye anga zao na sasa wanamshughulikia ni nini? Najiuliza baada ya mapigano hayo kuisha na labda Gaddafi kutoka madarakani hawa wananchi watakuwa na ubavu wa kujisifu kuwa wamefanya mapinduzi ya NGUVU YA UMMA? Na je watamuweka madarakani mtu waliokuwa wanadhani hatawasaidia au NGUVU YA MABEBERU itawawekea mtu wanaomtaka ili wafyonze mafuta kwa raha zao kama inavyoendelea huko Iraq? Nalo liona sasa hapo utakuwa ushindi wa NGUVU YA MABEBERU.Kwa hakika mimi sikubaliani na Gaddafi kukaa madarakani kwa kipindi kirefu cha miaka takribani 40 kama sijakosea,ila njia ya kumtoa madarakani inayotumika sasa itawagharimu miaka yote watu wa Libya..mifano tunayo angalia Iraq na nchi nyingine ambapo NGUVU YA MABEBERU ilipotumika nchi kuzing'oa serikali zilizokuwa madarakani,hazitawaliki na hazitatawalika milele....Nawashangaa watu wanaoshangilia NATO kuvamia LIBYA,hawajui kuwa hawa watu hawana permanent enemy nor friend,utakuwa rafiki au adui kulingana na namna unavyokubaliana wakunyonye hawajui leo Libya kwa Gaddafi,kesho itakuwa nchi nyingine yoyote na hatujui ni ipi may be IRAN....wazo langu NGUVU YA UMMA iachwe ifanye kazi na tusiingiliwe na hawa watu weupe,ni wauhaji kabisa tuwaogope kama ukoma au HIV..........


mwenzake Mubarak hakuwa na ndege za kivita? Mbona hakuwaita raia wake mende? Mbona hakuamuru ndege za kijeshi zitumike Takhrir Square? Qaddafi na Mabeberu wote lao moja...hawana mapenzi mema na watu wa Libya. Qaddafi haamini kitu kinachoitwa demokrasia, ndiyo maana mpaka kesho anakataa kuitwa rais (anataka aitwe kiongozi).

mtu asiyeamini democrasia hawezi kuruhusu nguvu ya umma katika utawala wake. acha wamtwange.
 
Kama hukuwa unajua basi ujue kuwa Marekani hayupo kwa sasa kwenye mashambulizi ya Libya, alishajitoa upo hapo?
Mkuu.
US hajajitoa.

Yet Gates, asked whether the military operation might be over by year's end, said, "I don't think anybody knows the answer to that."
At least one of the five Navy ships and submarines that have launched dozens of Tomahawk cruise missiles at Libyan targets from positions in the Mediterranean Sea has left the area, three defense officials said. They spoke on condition of anonymity in order to discuss sensitive military movements.
That still leaves what officials believe is sufficient naval firepower off Libya's coast, and it coincides with NATO's decision Sunday to take over command and control of the entire Libya operation. Aided by international air power, Libyan rebels were reported to have made important gains by capturing two oil complexes along the coast.

Clinton, Gates: Libya Operation Could Last Months
 
mwenzake Mubarak hakuwa na ndege za kivita? Mbona hakuwaita raia wake mende? Mbona hakuamuru ndege za kijeshi zitumike Takhrir Square? Qaddafi na Mabeberu wote lao moja...hawana mapenzi mema na watu wa Libya. Qaddafi haamini kitu kinachoitwa demokrasia, ndiyo maana mpaka kesho anakataa kuitwa rais (anataka aitwe kiongozi).

mtu asiyeamini democrasia hawezi kuruhusu nguvu ya umma katika utawala wake. acha wamtwange.

kwanza si kweli kwamba Mubarak hakuua Waandamanaji, zaidi ya Wamisri 300 walikufa katika maandamano yale.
pili waandamanaji wa amani hawawi na silaha za kulipua vifaru, silaha za kulipua ndege, n.k

Tatu azimio la kulinda wananchi wa libya inaonekana Nchi za magharibi wanalitumia kusapoti waasi wakati hawatakiwi "kutake sides". hii inaonyesha malengo yao yanakwenda beyond kulinda civilians, bali kutoa air cover kwa waasi ili wamng'oe Gadafi. na hii kusema kweli ni precedence mbaya sana, next time watatumia excuse hiyo hiyo ya kulinda Civilians ili kutoa kipondo kwa nchi hasimu zao kama Iran na nyinginezo.

Kwa mtu yeyote mpenda Uhuru wa Kujitawala hana budi kulaani kitendo cha nchi hizi kuconspire kuipiga Libya. na ili kujua unafiki wa nchi hizi, hawataachia waasi kuichukua Tripoli kwa nguvu , watalazimisha mazungumzo baina yao na Gadafi, ili Gadafi asije akacollapse kienyeji kienyeji na hatimaye kusababisha Chaos ya Civil war ambayo lawama na Gharama zitawarudia wao. hii air operation wanayoifanya ni kujaribu kuwa na "upper hand" kwa wote, waasi na Gadafi, kwa waasi watahakikishiwa mikataba minono ya mafuta, na kwa gadafi atawahakikishia anaondoka salama, ili kuwapoza wafuasi wake wasiendeleze armed struggle, iwapo Gadafi atakamatwa na majeshi ya waasi au hata kuuawa. wewe Subiri uone.
 
kwanza si kweli kwamba Mubarak hakuua Waandamanaji, zaidi ya Wamisri 300 walikufa katika maandamano yale.
pili waandamanaji wa amani hawawi na silaha za kulipua vifaru, silaha za kulipua ndege, n.k

Tatu azimio la kulinda wananchi wa libya inaonekana Nchi za magharibi wanalitumia kusapoti waasi wakati hawatakiwi "kutake sides". hii inaonyesha malengo yao yanakwenda beyond kulinda civilians, bali kutoa air cover kwa waasi ili wamng'oe Gadafi. na hii kusema kweli ni precedence mbaya sana, next time watatumia excuse hiyo hiyo ya kulinda Civilians ili kutoa kipondo kwa nchi hasimu zao kama Iran na nyinginezo.

Kwa mtu yeyote mpenda Uhuru wa Kujitawala hana budi kulaani kitendo cha nchi hizi kuconspire kuipiga Libya. na ili kujua unafiki wa nchi hizi, hawataachia waasi kuichukua Tripoli kwa nguvu , watalazimisha mazungumzo baina yao na Gadafi, ili Gadafi asije akacollapse kienyeji kienyeji na hatimaye kusababisha Chaos ya Civil war ambayo lawama na Gharama zitawarudia wao. hii air operation wanayoifanya ni kujaribu kuwa na "upper hand" kwa wote, waasi na Gadafi, kwa waasi watahakikishiwa mikataba minono ya mafuta, na kwa gadafi atawahakikishia anaondoka salama, ili kuwapoza wafuasi wake wasiendeleze armed struggle, iwapo Gadafi atakamatwa na majeshi ya waasi au hata kuuawa. wewe Subiri uone.
umejaribu kuchambua ila unatia shaka pale unaposhindwa kuona tatizo la Gadaff kwa jinsi ambavyo alideal na hili tatizo la waandamaji,mara al qaeda then waasi.Yes US wanaonea lakini kwa nini unambeb Gadaff kama malaika wakati ana move kibao za kigaidi????????????
 
Back
Top Bottom