Giza ndio asili ndio chanzo....kwenye uumbaji

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,782
d60d8aa4221b47f652c60bef564a9499.jpg
Nayatafakari sana maneno yale kwenye Bible takatifu kwamba hapo mwanzo dunia ilikuwa kiza totoro na uso wake ukifunikwa na maji.

Kutoka hapo ndio uumbaji ukaanza, kwa kutenga kiza na nuru...kwahiyo ikawa usiku(kiza)siku ya Kwanza.

Ukiacha kiza kinachofuata ni maji lakini leo hatujadili maji tunajadili kiza
Ni Kutoka kwenye giza ndio utenganisho wa vitu ukaanza rasmi
Kiza ndio kimekuwa ndio chanzo na asili yetu huu ndio ulimwengu wenye nguvu kuliko ulimwengu mwingine wa nuru.

Bara la afrika linapoitwa bara la giza... Kwa mtazamo hasi watu hawajui tu kuwa ule si mtazamo hasi, kiroho ni kitu kingine tofauti chenye nguvu kubwa --achana na mambo ya ulimwengu wa nuru mambo ya sayansi tech madaraka na siasa.

Hata historia inathibitisha kwamba binadamu wa Kwanza kuishi duniani alitokea Africa Tanzania black continent.

Kwahiyo wandugu kiza ndio kila kitu na matendo ya kiza sio matendo ya hiari huja na kuondoka kwa wakati wake.

Unapotaka usione kitu kitendo cha Kwanza cha haraka kinachokuja automatically ni kufumba macho ama kuyaziba, tendo la hiari la kugeuka hufuata baadae kabisa.

Lakini mwili Unapotaka kupumzika hujikuta bila kutegemea macho huwa mazito na baadae kulala kabisa, na huwezi kulala umekodoa macho ni lazima urudi kwenye asili yako...! Kizani! Unaweza kuwa bingwa wa kukesha ama hata kuwasha mataa mengi ili kufukuza giza lakini huwezi asilani. Kiza ni kiza na hakuna mwanga uwezao kufunika kiza chote.

La mwisho na la muhimu kujua ni kwamba mwisho wetu (kufa) ni kurudi kwenye asili na ndio maana hata ukifa umekodoa macho waliopo hukusaidia kukufunika.

Tafsiri yake ni moja.... Unaaambiwa rudi kwenye asili yako
Shetani mwenye nguvu sana na matendo yake yanayovuta mamilioni ndio mungu wa ulimwengu wa kiza... Unavutwa bila hiari bila utashi, unafanya kisha unajuta sana lakini unarudia yale yale ya giza. Usijilaumu sana KIZA NDIO ASILI NA CHANZO CHA UUMBAJI

Jr.!
 
Ahsante sana kwa mada!

Huyu mungu unayemzungumzia ni yupi?.Huwezi kuandika MUNGU au Mungu?.Au siyo huyu Muumba wa Mbingu tunayemfahamu sisi?.Kama ni huyu basi anaandikwa kwa herufi kubwa, mfano Mungu,MUNGU nk kwa sababu ya sifa zake kuu ambazo sie binadamu hatuna na siyo kama ulivyomuandika.

Back to the topic.

Kuna masuala kadhaa umeyachanganya katika mada yako.Tuna black na Darkness,hizi ni terminology mbili tofauti na hata katika matumizi, wanaposema Dark Continent hawamaanishi Black Continent.
 
Ahsante sana kwa mada!

Huyu mungu unayemzungumzia ni yupi?.Huwezi kuandika MUNGU au Mungu?.Au siyo huyu Muumba wa Mbingu tunayemfahamu sisi?.Kama ni huyu basi anaandikwa kwa herufi kubwa, mfano Mungu,MUNGU nk kwa sababu ya sifa zake kuu ambazo sie binadamu hatuna na siyo kama ulivyomuandika.

Back to the topic.

Kuna masuala kadhaa umeyachanganya katika mada yako.Tuna black na Darkness,hizi ni terminology mbili tofauti na hata katika matumizi, wanaposema Dark Continent hawamaanishi Black Continent.
Asante kwa ufafanuzi wa dark na black japo mwishowe tafsiri inakuwa ni ile ile kiza ama nyeusi
Hapo kwenye mungu hebu rudia kusoma tena.... Naelewa vizuri sana matumizi ya herufi kubwa na ndogo... Sijammaanisha Mungu Mwenye enzi yote bali mungu shetani baba wa matendo ya giza
 
Back
Top Bottom