Gigy Money amponda Alberto Msando kuhusu video iliyovuja akimpima oil

Status
Not open for further replies.

instagram

JF-Expert Member
May 27, 2014
2,091
4,716
ALBERTO MSANDO GIGY MONEY
A to Z ya Video Chafu ya Gigy Money na Wakili Msando...Msando Adai Gigy Amelipiza Kisasi

Aibu! Siri nzito imevuja baada ya video chafu iliyomhusisha wakili maarufu hapa nchini ambaye pia aliwahi kusimamia kesi ya Wema Sepetu, Albert Msando na muuza sura katika video za wasanii wa Bongo Fleva, Gift Stanford ‘Gigy Money’.

Video hiyo inamuonyesha Msando akimshikashika sehemu nyeti msichana huyo ambaye naye anajibu kwa kumkatikia mauno mwanasheria huyo msomi. Wakati wadau mbalimbali wakimlaumu Msando kwa kile walichosema amejishushia heshima, Risasi Mchanganyiko limebaini kuwa ishu hiyo haikutokea kwa bahati mbaya, bali ni kisasi kilichopangiliwa kwa ustadi.

MWANZO WA MCHEZO

Gigy Money alikuwa katika ziara ya kimuziki katika Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro akiwa na rafiki yake mmoja ambaye jina lake halikufahamika, aliyekuwa akifanya mawasiliano na mwanasheria huyo maarufu nchini, ambaye wakati huo alikuwa Arusha.

HUYU HAPA GIGY AKIMWAGA MBOGA…

Akizungumza baada ya video hiyo kuvuja, Gigy alisema wiki iliyopita alikuwa na shoo maeneo ya Boma, Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro ambako akiwa huko alipata mwaliko kutoka kwa Msando wa kwenda kumtembelea katika klabu yake iitwayo The Don, iliyopo Arusha.

“Kweli Msando nilikuwa sijawahi kuonana naye live, ila aliposikia nipo Hai akanipa mwaliko, nikamwambia siwezi kwenda kwa kuwa nilikuwa bize na shoo, pia sikuona umuhimu sana wa kumuona maana sicho kilichonipeleka. “Baada ya kusema atanitumia usafiri, nikakubali, nilipomaliza kazi alikuja na gari akiwa na watu wanne, wanaume wawili na wanawake wawili, tulifika Arusha tukaenda club, nikalewa sana na baada ya hapo wakanipa tena lifti kwenye gari yao kwenda hotelini.

“Tukiwa kwenye gari huku nimelewa, nilisikia Msando akimwambia mmoja wa wale watu aturekodi nami sikuelewa ana maana gani, wakanishusha nikaenda kulala peke yangu, sijalala na mtu yeyote, kesho yake nikaiona kwenye mitandao, kiukweli kitendo hicho hakijanifurahisha hata kidogo, kimeniudhi mno maana kimenidhalilisha,” alisema Gigy.

MSIKIE MSANDO SASA

Risasi Mchanganyiko lilijaribu mara kadhaa kumpigia simu yake ya mkononi bila kupokelewa, lakini baada ya kutumiwa ujumbe mfupi wa simu, likijitambulisha na kuomba kupata ufafanuzi kuhusu video iliyopo mtandaoni, Msando alipiga simu na kuzungumza.

Risasi: Mambo vipi kaka!

Msando: Safi aisee.

Risasi: Pole kwa kilichotokea mzee.

Msando: Aaah ndiyo imeshatokea tena haina jinsi.

Risasi: Kwani ilikuwaje kaka?

Msando: Aaah, unajua kilichotokea ni kama huyu dada amenilipizia hivi!

Risasi: Kivipi? Msando: Si unajua huyu dada aliwahi kusema kuwa hakumbuki ame-date na watu wangapi? Sasa mimi kuna siku nilipost (kuandika katika mitandao ya kijamii) nikishangaa kama kwa miaka miwili tu ameshawasahau, basi kuna tabu.

Sasa najua kuanzia pale akawa na hasira na mimi.

Risasi: Kwani mnafahamiana kabla ya leo?

Msando: Sijawahi kuwa na mawasiliano naye hata mara moja.

Risasi: Khaa, sasa kama hamjawahi kuwasiliana ilikuwaje ikawa kama vile ilivyokuwa?

Msando: Mimi nilikuwa nawasiliana na dada mmoja ambaye alikuwa anatumia simu ya Gigy, aliniambia wanataka sana kuja kupaona klabu kwangu, nikaona isiwe tabu, nikawakaribisha.

Risasi: Kwani wewe una klabu?

Msando: Ndiyo, inaitwa The Don, ipo Njiro.

Risasi: Aisee, safi kaka, uko vizuri. Enhee, ikawaje sasa?

Msando: Basi wakaja ile usiku sana, tukawa pamoja tunapata mambo, hadi kunakaribia kucha tukaondoka.
Risasi: Sasa ile video ilirekodiwa wapi?

Msando: Ndani ya gari wakati tunarudi, aliyekuwa anatupiga picha ni rafiki yake. Risasi: Hukuelewa kama unarekodiwa au uliruhusu jambo hilo lifanyike?


d945206858c768026ea234c63568059e.jpg

15f21aad69c5bc5f9f89a436ac1222c8.jpg

bcd0414fdcbaf146dfacfbea6ef84eb5.jpg
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom