Ghost phase kwenye maisha ya mwanaume

Sasa mfano umetokomea huko umerudi unakuta wale uliokuwa ukiwa-'ghost' hawakuhitaji tena. Itakuwaje?

Naona kama lengo la kuwa ghost ni kuja kuwatambia watu kimtindo.
Tengeneza circle yako , circle ya watu ambao watakuwa ni wepesi kuelewa hisia zako na Ambition zako

Shida ya sisi wa Africa tulio wengi Huwa tunazungukwa na watu ambao ni wepesi kuwa katisha wenzao tamaa , wengi wao hawana wanacho changia katika fikra zetu wapo negative sana bad enough ni watu ambao wanataka kusaidiwa nyakati zote kuliko wao kusaidia so mtu unakuwa upo katika circle na watu ambao Kila siku wao ndio wenye shida wanataka uwasaidie wao but siku wewe ukifeli Hakuna hata wa kukupa back up kati Yao ,, so hiyo ndio circle Gani !?
 

View: https://youtube.com/shorts/UlIaRtbLogc?si=HMN2c08clrI_jBsn
 
Hao watu walikuwa wanazuia mafanikio yako kivipi mpaka uamue kuwatenga? Nashindwa kuelewa...
Kuna mambo ambayo kuyafanya yanakuwia vigumu ukiwa kwenye circke yako, mfano umesoma mpaka degree halafu ajira haujapata. Akitokea mtu akakwambia fanya kazi yoyote inakua ngumu kidogo kumuelewa kwa sababu ya ile expectation ambayo jamii inakua nayo juu yako kama msomi. Lakini ukiamua kuondoka mahali unapoishi na kwenda sehemu ambapo hakuna anaekujua ni rahisi kufanya kufanyia kazi huo ushauri wa "fanya kazi yoyote"
 
Ila hii concept ya ukifanikiwa usianze kusaidia watu sijaielewa kabisa, labda kama inamaelezo zaidi.
hearly
 
Na vipi kama kuna fursa nzuri hapo unapoishi. Utaiacha kwa kuogopa watu?
 
Na vipi kama kuna fursa nzuri hapo unapoishi. Utaiacha kwa kuogopa watu?
Na vipi kuhusu usalama wako !? Fursa inaweza kuwa nzuri lakini usalama hakuna , Utachagua kipi kwanza !?

Fursa inapaswa kuendana na usalama pia , tunatafuta maisha but kitu Cha kwanza kuzingatia ni usalama wako first maana ukipatwa na tishio la usalama wa Mali zako na maisha yako Kwa ujumla then ukatokea ukapata Matatizo ya kugharimu uhai wako ,

Hayo maisha utayaendesha vipi Ukiwa mahututi au Ukiwa kaburini!?
 
Na vipi kama kuna fursa nzuri hapo unapoishi. Utaiacha kwa kuogopa watu?
Nimetolea mfano lakini sio kila situation inahitaji kuama sehemu ulipo. Msingi wa ghost mode ni kukata distractions ambazo unaona kuna namna zinazuia au zinachelewesha mafanikio yako, na hizi distractions sio watu tu hata ratiba, behaviors, habbit nazo zinaweza kuwa distributions. Ukisema uache ulevi automatically utawa-ghost unaokutana nao bar mara kwa mara
 
Tupunguze ushauri Maishani kila mtu anaishi maisha mapya kila siku

Hakuna legend wa Maisha
Uzoefu unamfanya mtu kuwa na busara, kwaiyo hakuna ubaya ukawaelekeza mapema uliowatangulia yale mambo ambayo wewe ulichelewa kujifunza.

Watu wengi tumekalili kwamba binadamu anajifunza kutokana na makosa, kwaiyo tunaamini mpaka mtu afanye maamuzi mabovu ndio anajifunza. Kitu ambacho sio kweli. Binadamu mwenye hekim anaweza kujifunza kwa kupewa miongozo na kuangalia walipokosea waliomtangulia then akachukua hatua sahihi mapema kabla hajapotea au hajapigwa na kitu kizito
 
Napenda kukaa peke yangu kwa utulivu huku naskiliza mzk mzto sn, napenda kutafakari, meditate mambo yng na namna nitakavyofanikiwa, sipendi kuonea wala kuonewa na mtu, napenda na nafurahia kuwatendea wengne haki au kuwapa haki zao, spendi kukopa au kudaiwa, naishi kulingana na kpato changu, wkt mwng spend ndugu, marafk wajue npo wp au nafanya nn, naskia amani sn nikiwa nmekaa mwnyw kwa utulivu mkuu kuliko nikiwa na watu hasa wanaoongeaongea sn, chumban nmebandka maneno ambayo nikiwemo tu nayaona na nayasoma kwa kujiambia mfano i prevail, a victor, a winner, a conqueror yapo chumban kwng, napenda kutimiza wajbu wng, nina huruma sn ila ninamsmamo usiyoyumba, niksema natoka eneo fulan na starud tena na hakika huwa sirud nyuma, nikmtema mtu nimemtema kweli ila akjrud huwa nasamehe tu, napenda sn kusaidia wenye uhitaji, napenda kushnda kiroho kuliko kmwili, mtu aktaka vita kwangu atapata, aktaka amani atapata sinaga shda na mtu, spendi kuwapa watu mambo ya kunijadili labda wajtungie ya uwongo ila yng hawayapati.
 
Mimi sio msoto tu mimi hata likitokea suala ambalo linavuluga ratiba zangu huwa naghadhibika sana, na nikiwa katika hali iyo solution yangu ni ghost mode mfano kama nipo home siongei na yoyote. Nawasha tv natulia tu naangalia mpira, na ghadhabu niliyokua nayo inaondoka taratibu mpaka nakua sawa.
 
Yeah binaadamu tuna tofautiana sana character zetu
 
Mada nzuri sana hii

Sometimes huwa nawaelewa sana watu wanaoamua kujilipua na kwenda kuishi mbali na jamii ya watu walipozaliwa au kukulia

Wakishajipata, ndio utawaoana wanarudi tena ile kiaina

Wanawasaidia wawili watatu, dhen wanarudi kwenye life ya kujitenga kidogo

Afrika kuna mambo mengi sana ya kukwamishana, ya kiroho, wivu, chuki, fitina, majungu, kupangiana maisha, uchawa, na kila aina ya sarakasi

Hasa ukiwa na ndoto za kufanikiwa ukiwa kijana mdogo na kuna ma legend wao hawajatoboa

Hii ya kujitenga kwa muda ni kitu muhimu sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…