Nilipotaka kuchimba kisima changu na kuona haya makampuni yanavyochimba mikwara ya utafiti tu nilichoka na kuishiwa nguvu. Nikakumbuka jana yake jirani yangu aliponiambia kuna kikundi cha vijana wajasiri mali wanachimba kisima kwa gharama nafuu na wana uzoefu wa kujua kama maji yanapatikana au laa katika eneo hilo. Nikaamua kurudi niwatafute hao vijana, na kweli walipofika eneo hilo wakafanya utafiti kutokana na visima vilivyochimwa awali na wakasema 90% maji yapo chini ya ardhi Ft 80 - 100.
Ingwawa ilikuwa risk nilijilazimisha kuwaamini kutokana na majirani wa hapo kuwa na visima vingi tu vya maji. Bila ajizi vijana wali-drill kisima cha maji kwa zana zao za kimachinga na walipofikia Ft 55 dalili za maji zilianza na wakanihakikishia wanataka wafikishi ft 80 ili kupata maji baridi bila chumvi.
Nikuhakikishie hadi leo napata maji safi baridiii toka Ft 80 chini ya ardhi kwa gharama nafuu sana, kwani gharama zote za kuchimba kisima na kukamilika kuweka pump ilinigharibu Tz Shs 1,200,000. Gharama hii ni tofauti na ile waliyoniambia wataalamu maana wao utafiti tu zaidi ya laki tatu zingenitoka.
Maelezo hayo ni kwa kisima ambacho ni drilled ambacho pia ni salama kwa familia yako tofauti na kisima chenye shimo kubwa la kuchimbwa ambalo pia si salama kwa famili na huweza sababisha mmommonyoko wa ardhi.
- Mambo ya msingi yanayotakiwa uyaandae ni kujaribu kuangalia waliokutangulia maeneo hayo kama wana maji ya visima na pia kujirishisha kwamba eneo lako haliko kwenye mwinuko zaidi ya wenzako walio na visima eneo lako.
- Ukubwa wa kisima chako ni diameter ngapi kulingana na mabomba mengi yanayopatikana ambyo kwa kawaida ni mabomba magumu ya Plastic yatakayozamisha ili kuhifadhi maji ndani ya kisima chako.
- Kuna mchanga wa pekee wa kutiwa kwenye basement ya kisima chako na kando ya bomba ili kuchuja maji yawe maangavu zaidi, wachimbaji wa visima wanajua wapi kwa kupata mchanga huo hasa kandokando ya vijito vya maji, na kuna wauzaji mitaani wa mchanga huo ila hakikisha umehakikiwa na wazoefu wa visima vya maji usijechukua mchanga unaotoa vumbi k uchafua tena maji yako zaidi.
- Mabomba yatakayounganishwa hadi chini ambayo ni ya plastic ya kuhifadhi maji tokana na chemchemi.
- Kifuniko cha juu kwenye kisima chako ili kulinda na kuhifahdi kisima kisiharibiwe na maji machafu yasiingie tena.
- Pump ya maji na tank la maji.
Kama nafasi inakuruhusu kuwatumia wataalamu zaidi ni bora tu ila ujue gharama nazo zinaendana na kiwango cha ukubwa na elimu ya mtu.
Kwanza kabisa nawashukuru wote kwa mchango wenu.Mwenzetu wewe uliyechimbiwa na wajasilimali
ullichimbiwa maeneo gani? je unaweza kutuunganisha na hao wajasilimali ?tutawapataje?
Mimi ninavyoelewa kuchimba kisima chini ili kupata maji ni lazima uwe na kibali,haina tofauti sana na kuchimba madini.
Na katika kibali hicho kitakua kimeandikwa full details ya utaratibu wa uchimbaji.
Mimi nakushauri kama unataka kuchimba maji ardhini ni lazima utumie wataalamu ambao wanavifaa vya kisasa vitakavyoeleza kama kweli maji yako chini na yako umbali gani na kama yanafaa kwa matumizi ya binadamu.
Wakishakuchimbia kisima na maji kutoka sio kwamba utaanza kuyatumia hayo maji moja kwa moja,itabidi wayachukue wayapeleke labolatory kwa ajili ya kupima contents ya madini yaliopo kama yako kwenye normal range ya matumizi ya binadamu.Wakati mwingine maji yanaweza kupatikana kumbe yana madini fulani ambayo ni sumu ndani ya mwili wa binadamu,kwa hiyo kwa upande wa maji ni lazima ukubali kuingia gharama kwa kutumia wataalamu kwa ajili ya maisha yako na familia yako.
Pia wataalamu wataweza kukuambia una maji kiasi gani ardhini,hivyo utaweza kupanga mipango yako,kama kuyatumia kwa biashara au matumizi ya nyumbani.
Nawasilisha.
Sipingani nawe, hilo ni jambo la msingi, ila kumbuka mtu anapochimba kisima ndani ya kiwanja chake ni tofauti na anapochimba sehemu ambayo haimiliki. Kwa usalama zaidi inafaa kusajili kisima na kuhakikiwa maji kwa usalama, lakini wengi wanakwepa hilokutokana na kwamba huwezi kuhakikiwa usalama wa maji bila kuwa na ownership certificate ambayo itakulazimu kulipia kodi kila mwaka. Sidhani kama ni big issue maji kama yatatumika na familia, lakini kama ni kwa ajili ya biashara kuongeza kipato hapo hakuna ujanja, taratibu za kisheria hapana budi zifuatwe.
Kwa usalama wa afya ya watumiaji wa maji hata kama ni familia ni bora kupima usalama wa maji.
Naomba anuani au contacts zao.
Nami naomba nipate contact zao....jamani hao vijana ni assets sana!!
Wachangiaji hapo juu wote wako right, huyu wa kwanza ni kuhusu gharama, huyu Wa pili alichosema ni kweli kabisa usalama wa Maji huwa lazima upimwe na kisima kinapewa certificate ambayo unalipia si hela nyingi niliambiwa lkn nimesahau. Kama sikosei unalipa hiyo hela kila mwaka. Hiyo ndio sheria unaweza kufanya bila kufuata sheria na mambo yakawa sawa miaka yote ILA kikitokea cha kutokea labda mtu amekunywa gongo zake huko akaja akanywa Maji then akafa. Hapo shughuli zako zitasimama Kama unavyojua hata forensic hamna utaambiwa umeua. Unaweza watumia hao wachimbaji then ukakisajili Kama kawaida. Mchangiaji Wa kwanza tupatie contact za wachimbaji maana mimi pale Samora wameniambia mara Tatu ya hiyo hela ya kuchimbia. Na Kama unajua aina ya PUMP tafadhali nipatie pia.Asante.
Aina nzuri ya pump ni ile inayovuta maji badala ya ile inayosukuma maji.
Pump ya kusukuma maji huzamishwa ndani ya kisima na husukuma maji yaje juu, aina hii ya pump ina matatizo mengi utahitaji kubadilisha vipuli kila kukicha na pengine kama kisima hakikuwekewa mchanga wa kutosha utashtukia tobe limeingia kwenye tank lako la maji.
Pump ya kufuta maji ni nzuri zaidi kwa vile huwekwa nje ya kisima hivyo haikumbani na dhoruba ya maji kama ilivyo kwa ile ya kusukuma maji inayozamiswa ndani ya maji.
Pumb hizi ziko nyingi tu Kariakoo na ule mtaa wa bei mbaya kule Samora Ave. Lakini fanya utafiti wa kutosha kupata pump inayofaa maana siku hizi zipo nyingi ambazo ni fake.
Naomba mnipe muda niwape maelekezo namna ya kuwapata. Walichimba kisima eleno la Ukonga. Najua gharama zitakuwa zimepanda maana ni miaka 4 iliyopita, ndo maana nahitaji kuwapa maelekezo maana wakati huo hawakuwa na namba za simu. Na bila shaka mtawapata kwa urahisi tu kwa vile wanajulikana sana. Maskani yao yalikuwa Mbagala. Cha msingi utakapowapata andaa sembe la nguvu maana kazi hiyo inahitaji sana shibe na ni motisha kwa kazi yao.