Gharama halisi ya Affidavit.

Gharama halisi ya Affidavit.

bachelor sugu

JF-Expert Member
Joined
Jan 30, 2018
Posts
2,689
Reaction score
3,651
Habari za usiku wadau,

Jamani samahani naombeni kuuliza kwa wenye taarifa za sasa kuhusu gharama halali na halisi ya Affidavit kwa mtu asiye na cheti cha kuzaliwa maana kuna vijana wangu nimewaelekeza mahali flani waende kufuatilia Affidavit form nikifahamu ni gharama isiyozidi sh.3500 kama haijabadilika kama nilivyowahi kuichukua kwa ajili ya mtegemezi wangu mmoja 2017 ila kilichonishtusha ni kuwa leo hii 07/8/2019 vijana wangu wameenda Dodoma mahakama moja wakakutana na tapeli mmoja kawaambia kuwa Affidavit ni sh.30,000/= kitu kilichowakatisha tamaa na kuondoka.

Sasa kwa kweli nimesikitishwa na hawa watendaji wasio na hofu na pesa za wenzao sasa naomba ambaye anafahamu bei ya sasa kama kuna mabadiliko yoyote anijuze maana nataka niwarejeshe tena wamfuate huyohuyo tapeli na kumpa conditions awashughulikie swala lao kwa bei halisi na kama atakataa niwape maelekezo wampelekee hela ya moto maana naona hapo anataka Rushwa.

Karibuni.
 
Cheti cha kuzaliwa una kipata siku hiyo hiyo, kwanini uhangaike na affidavit.
Ni kweli mkuu nimesikia kuwa mtu anaweza kupata cheti cha kuzaliwa ila sasa shida ni pale unapokihitaji ukiwa ktk wilaya ambayo hujaziliwa hapo sasa ukipiga hesabu kurudi kwenu mbali kwenda Rita makao makuu napo mbali basi hapo kidogo shida inakuwa kubwa kupelekea uitafute hata affidavit.
 
WATIZED WAMNAPENDA RUSHWA BALAA

UNAWEZA KUTA NI GHARAMA NDOGO TU ILA MMMH
 
Kama ni aged over 10 yrs.... CHETI ni 20k
Ukiwa na clinic card unapata!

Km huna uwe na kimoja kati ya ID YA MPIGA KURA ama CHETI CHA LEAVING CHA SHULE.... plus AFFIDAVIT....

Sio kweli kwamba kinapatikana ndani ya siku 1..... Uwongo.... Km utaomba kama URGENTLY needed si chini ya siku 3!
Shngapi na kama kilipotea unafanyaje kupata kipya
 
Kama ni aged over 10 yrs.... CHETI ni 20k
Ukiwa na clinic card unapata!

Km huna uwe na kimoja kati ya ID YA MPIGA KURA ama CHETI CHA LEAVING CHA SHULE.... plus AFFIDAVIT....

Sio kweli kwamba kinapatikana ndani ya siku 1..... Uwongo.... Km utaomba kama URGENTLY needed si chini ya siku 3!

Kama nishawai pata nikakipoteza nataka nikakichukue tena?
 
Affidavit form inapatikana bure bila malipo,hao wanaoomba pesa ni rushwa ya wazi kabisa
 
Back
Top Bottom