Wakuu mi kwangu mkaa wa 1500 kwa siku ya natosha kupika, kuchemshia maji ya kunywa na mapishi kwa siku nzima halafu ges ambayo huwa natumia hii ya 30kg inamaliza wki 3 na sehemu na inauzwa 58,000, transport 2000 jumla 59,000
Sasa wakuu mkaa 1500x31= 46,500/=TZS vs 59,000 ungekuwa wewe ungenunua gesi kweli?
Swali la pili ni kweli serikali hii ina mkakati madhubuti wa kupambana na mazingira?
Pamoja na kwamba hesabu yako ya gesi ilitakiwa kuwa Tsh. 60,000/=
Kuna mambo ambayo ukizingatia, bado gesi ina nafuu.
A: GESI
1: Gharama: hutegemea na mtumiaji.
Matumizi ya gesi: kuhakikisha wanaotumia wanaelewa kuwa moto wa gesi unaotakiwa kuwaka ni bluu, na si njano. Wengi hutegemea ile sauti ya uwakaji na kufungua kwa kiasi kikubwa ili kujiridhisha kisaikolojia kumbe gesi nyigi kwa wakati huo inatoka bila kuungua vyema na hivyo kunakuwa na poor heat. Ukifanya hivyo utaona unaitumia kwa muda mrefu na utashangaa.
2: Time factor for cooking: nzuri
3: Usafi: mzuri
4: Utunzaji mazingira: nzuri
5: Material ya kuwashia: nzuri
6: Material kusafishia vifaa: nzuri
7: Afya: ni njema zaidi
B: MKAA
1: Gharama: inategemea ulipo na matumizi kama kwa gesi.
2: Usafi: chini ya gesi
3: Time factor: zaidi ya gesi
4: Utunzaji mazingira: mbaya kuliko gesi
5: Material ya kuwashia: juu zaidi ya gesi
6: Material kusafishia vifaa: juu zaidi ya gesi
7: Afya: kuna tatizo
NB: Tujaribu kujifunza pia, kwa vitu vya kuchemsha kama nyama etc. Kuchemshwa kwa wakati mmoja na jioni kuwa ni kuunha tu. Kutokana na urahisi wa gesi, unaweza kukuta mtu anachemsha asubuhi na jioni.
Pia ishu ya maharage kulowekwa kwanza kama ilivyoshauriwa na wadau hapo juu.