- Central Tanzania in Dodoma Region
Video hisani ya Hildebrandshayo wa Youtube
Habari za ziada kuhusu madini bwerere Tanzania toka Raiamwema Toleo namba 180 la tarehe 6-12 ,Aprili 2011:
Mahojiano ya Godfrey Dilunga wa gazeti la Raiamwema na Dr.Mselly Nzotta mtaalamu wa Metallurgy anayetamba kitaaluma Sweden anatoa data za ziada:
Dr. Nzotta: Kuna ramani niliyompa inayoonyesha kwamba kuna gold belt (mkondo/mkanda wa dhahabu) kutoka Ziwa Victoria umepitia katikati ya Tanzania, mkoani Dodoma mpaka kufika Afrika Kusini, lakini chimbuko lake ni Bukoba.
Nikamwuliza inakuwaje mwananchi wa Bukoba ana mali ya thamani kubwa chini ya ardhi kama hiyo, lakini hata kununua chumvi hawezi? Akanijibu kwamba; nimuandikie na akanipa anuani yake binafsi ili watu wengine wasinizubaishe katika ufuatiliaji wa mpango wangu.
Raia Mwema: Baada ya hapo nini kilifuata? Ulisaidiwa kuhamisha vifaa vya maabara kutoka Sweden?
Dk. Nzotta: Baada ya miaka kadhaa, wakaja (Kikwete) wakiwa na Mkapa (Rais) pale Sweden. Walivyokuja nikapata nafasi pia ya kujieleza kwa Mkapa. Tatizo lililokuwapo kwa wakati ule nilipokuwa najieleza nilimwita Mkapa "Mtukufu Rais". Sasa kumbe huku nyumbani alikuwa amekwishakataza kuitwa hivyo. Mimi sikuwa na hizo taarifa, kwa hiyo nilikuwa kila mara nikimwita hivyo.
Alichukia sana nilipomwita "Mtukufu Rais". Alikasirika kiasi cha maelezo yangu kutokuwa na maana tena kwake, na hakuna alichojibu zaidi ya kukasirika na kueleza kuwa watu wa Sweden "hatuna heshima". Nilimweleza tena Waziri (Kikwete) lakini naye akasema hana cha kufanya tofauti na msimamo wa mzee (Rais).
Raia Mwema: Je, ulikata tamaa?
Dk. Nzotta: Hapana, sikukata tamaa. Kuna siku moja tukiwa ubalozini (Ubalozi wa Tanzania nchini Sweden) nilishauri kwamba kwa nini ubalozi wa Tanzania usianzishe database (hifadhi ya taarifa) ya Watanzania watalaamu? Unajua India ndiyo wanavyofanya, wanayo database ya wataalamu wao wote walioko nje ya nchi.
Hiyo inasaidia sana kwa sababu serikali inapokuwa na uamuzi wa mradi au jambo fulani unaohitaji watalaamu wa aina fulani, basi, inakuwa rahisi kwao kujua nani yuko wapi, na kumuita kwa sababu huyo ni Mtanzania; hata kama amechukua uraia wa nchi za nje.
Sasa pale ubalozini kulikuwa na ofisa mmoja ambaye kwa sasa yuko Ikulu (Dar es Salaam). Balozi hakuonyesha kuvutiwa sana na wazo hilo la database lakini huyo ofisa ubalozini pale alivutiwa na kuthamini. Ofisa mwenye anaitwa Mwaipaja kwa wakati ule alikuwa katibu wa balozi wetu Sweden.
Sasa, nilisahau kukueleza kuwa baada ya kumaliza masomo mwaka 1999 niliajiriwa na kiwanda cha chuma kule kule Sweden kinaitwa Uddeholm Tooling AB. AB ni kama Limited kwa hapa Tanzania.
Sasa yule Ofisa wa Ubalozi Mwaipaja akaja kunitembelea pale kiwandani kwetu na kukagua shughuli zangu, na kwa kweli mpaka leo yeye ndiye anayenihimiza; vinginevyo ni kama nilianza kukata tamaa.
Mwaka 2004 nikaja kwa nauli yangu wakati ule kulikuwa na Wizara ya Sayansi na Teknolojia, nikapangiwa nikutane na watu wa DIT (Dar es Salaam Institute of Technology) ili tuzungumzie suala la kuanzisha Steel Complex Tanzania (SCT) kwa ajili ya kutoa taaluma ya metallurgy kwa vijana wetu ili tunufaike zaidi na raslimali zetu.
Tukazungumza na mkuu wa DIT akaandika barua ili tuombe msaada SIDA (Shirika la Maendeleo la Sweden) kwa ajili ya kutafuta watalaamu, lakini nasikitika kwamba hapakuwa na msukumo au dhamira ya kutosha ya kisiasa.
Baadaye tena safari ya pili binafsi nikaja mwaka 2008. Nilikuja kama mwakilishi wa kampuni yangu ya Sweden nilikoajiriwa. Nikazungumza na watu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Unajua katika tunachokusudia kuanzisha (SCT) tumepanga katika maeneo tofauti ya utekelezaji au uendeshaji. Tumeona kwamba ili Tanzania iendelee watu au wanafunzi wafundishwe katika makundi makuu mawili.
Soma nakala kamili: http://www.raiamwema.co.tz/news.php?d=3072 Dr.Mselly Nzotta mtaalamu anayetamba kitaaluma Sweden.
Last edited by a moderator: