Iran ndiyo iloyoomba bita ikome. Ujumbe ulioongozwa na waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ulienda Umoja wa Ulaya kuwataka wailazimishe Israel kukomesha vita. Nchi za Ulaya ziliwrka wazi kuwa ni Marekani pekee ndiyo yenye uwezo wa kuiambia Israel isimamishe vita, ikasikiliza. Umoha wa Ulaya waliongea na Trump. Trump akaongea na Iran, na kisha kuwataka Israel wasimamishe mashambulizi. Israel ilirudisha ndege zake zilizokuwa tayari angani kwenda kuishambulia Iran.
Ila wapo wajinga ambao hupenda kuongea yanayofurahisha nafsi zao, wanasema Marekani iliiomba Iran kusimamisha vita, wakati Trump hakuiomba Iran kusimamisha vita bali aliiamuru Iran kusimamisha vita mara moja, na akawaahidi kuwa atailazimisha Israel nayo kusimamisha mashambulizi. Iran ikakubali mara moja, na Israel ikaridhia. Kama Iran ingekuwa na ubavu wa kuipiga Israel isingekubali kusimamisha vita mara moja kwa sababu yenyewe ndiyo iliyokuwa imepigwa vibaya, na kuingia hasara kubwa, ikiwemo kupoteza karibia makamanda wote wa juu na wataalam wa nuclear. Mashambulizi ya Iran nchini Israel yaliua watu 28, lakini mashambulizi ya Israel nchini Iran yaliua watu 1,000+.