Nyanda Banka
JF-Expert Member
- Mar 14, 2023
- 330
- 1,244
Gerezani ni mahala ambapo kila Mtu apendaye Uhuru anapaona bora uwe hospital umelazwa hata kama hujui ni lini utapa ahueni ila utakuwa na tumaini la Uhuru na kukutana na wapendwa wako kwa wakati.
JeLa ni mahala panapozima Furaha na Matumaini ya Mwanadamu hata wale Wategemezi wake au Maisha yake Binafsi huwa yanayumba kama sio kutawanyika kabisa
Gerezani ni mahala ambapo andazi moja linaweza kuliwa na watu kumi ni kwa sababu ya Upendo.
Gerezani ni mahala ambapo ujamaa na ubinafsi huishia kwenye lango la Gereza ila ukiingia Gerezani mnakuwa Ndugu wa Damu
Gerezani yupo Baba au Mama wa Mtoto au watoto baada ya kufungwa tu Watoto wake walipoteza tumaini la kesho yao njema bila uwepo wa baba au mama yao waliyeamini uwepo wake katika Maisha yao ungekuwa daraja na mafanikio ya Ndoto za hatma zao
Gerezani zipo Ndoto kubwa zimezimwa kama mshumaa ulioko juu ya kaburi ambao hauna mtu wa kuuzingatia tena kuuwasha ukizimika
Gerezani wapo watu wema sana ambao wapo hapo si kwa sababu walitenda ila mazingira tu yaliwatia hatiani. Waliotamani Mungu Baba afunue ushahidi kwa sababu wao walipojitetea hawakuaminika wakahukumiwa Kwa sababu ya Mazingira, Huruma zao, Wema au majitoleo yao
Gerezani wapo Watu ambao Maisha ya Uraiani hawana uhakika nayo tena Kwa sababu maisha yao yote yameshaamuriwa yataishia gerezani
Gereza limebeba sauti nyingi ambazo zina mengi sana.
Ukitaka ujue zipo sauti nyingi zinazohitaji huruma nenda ukawasalimie Wafungwa au ukamatwe uende Gerezani/Selo