Geofrey Maseta
JF-Expert Member
- Nov 24, 2015
- 1,115
- 916
yuda ni yuda tu.. huwezi kumwita Petro..mchange.. punguza njaa.. 2010 si uliuza ww na 2015 umeuza tena? ndoroooobo we
GENGE LA WANAFIKI WA CHADEMA NA WAFUASI WAO WAKAPIMWE AKILI?.
-------------------------------------------------
Tangu asubuhi Leo vijana wa CHADEMA wametokwa na mishipa ya shingo Kumshambulia Zitto eti ni Mnafiki kwa kuwa aliwahi kuisifu kazi Ya kamishina mstaafu wa TRA Kitilya.
Hii ni baada ya kamishna huyo kuonekana sehemu ya kampuni ya EGM inayohusishwa na Utapeli wa bilioni 16 za mkopo.
Hivi nyie CHADEMA mlifikiri Zitto anaweza kujua yaliyo moyoni mwa Kitilya?.. Zitto alisifu utendaji kazi wa Kitilya ambao kila mtanzania aliuona na sio makando kando yake. Ni Kitilya na wenzake ndio wa kujieleza kwanini wameshiriki udanganyifu huo (kama wameshiriki). Na kumuacha Zitto aendelee na majukumu yake..
Eti Zitto Mnafiki.
Hivi unaweza Kumlinganisha Zitto Na Mbowe kwa unafiki?...Mbowe aliyesimama kidete Kumtukana LOWASSA na baadae kumsafisha?.
Mmesahau Mbowe alivyorudisha gari la BUNGE (KUB) kwa mbwembwe na bashasha akijidai anaunga mkono kubana matumizi na kulichukua tena kimyakimya
Hivi unaweza kumlinganisha Zitto na Lissu wa CHADEMA kwa unafiki?...Lissu aliyeshirikiana na Slaa kusoma Orodha ya Mafisadi na Kumtukana Lowassa mpaka matusi ya Nguoni?.
Hivi unaweza kumlinganisha Zitto Na Mnyika wa CHADEMA kwa unafiki?..mnyika aliyetamba kuwa na Ushahidi wa UFISADI wa Lowassa na kuishia kumnadi kama Rais?..
Hivi unaweza kumlinganisha Zitto na MSIGWA wa CHADEMA kwa Unafiki?..Msigwa aliyetaka wanaomuunga Mkono Lowassa wapimwe akili na yeye mwenyewe akaishia kumnadi bila aibu.
Unaweza kumlinganisha Zitto na Lema wa CHADEMA kwa unafiki?.
Lema aliyesema ni Heshima kubwa kwa Mungu kumzomea Lowassa kwa maana ni FISADI na baadae yeye mwenyewe kunadiwa na FISADI namba 9 katika orodha ya chadema?..
Umaweza kumlinganisha Zitto na CHADEMA kwa unafiki, CHADEMA walioweka orodha ya MAFISADI katika mtandao wao kwa miaka 8 na kuiondoa ghafla baada ya chama kununuliwa na Fisadi namba 9?...
CHADEMA waliogoma kuacha kupokea posho za vikao na kumuacha zitto peke yake aendelee kutokuzipokea na wao kuramba pesa za walipa kodi.
CHADEMA kwa sasa ndio kisima cha Wanafiki waliojificha kwenye wimbi la ukamanda.
Achaneni na Zitto fanyeni yenu na wanafiki wenzenu pamoja na mafisadi wenu mliowatoa CCM.
Habibu Mchange
0762178678
Dar es salaam.
Zito alisema ana majina ya walioficha pesa uswisi wako wapi?
Mchange amemtuma Kala Pina....
Huwezi kupata kura 1000 ukose msongo wa mawazo!
yuda ni yuda tu.. huwezi kumwita Petro..mchange.. punguza njaa.. 2010 si uliuza ww na 2015 umeuza tena? ndoroooobo we
Huyu jamaa...sijui anapata wap ujasiri wakuandika haya wakati alipata kura buku tatu ...tu.....ingekuwa mm wala nisingetoka ndan
Wahaya wana usemi usemao:
MWANAUME ANABADILIKA KITANDANI TU LAKINI SIO KWENYE KAULI
Hao uliowasema walijitahidi kukipulizia marashi kinyesi Ili kinukie vizuri.
Nalog off