Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,501
- 9,280
Baada ya watoto watatu kuuawa na fisi huku watano wakijeruhiwa vibaya wilayani Nyang'wale mkoani Geita mkuu wa wilaya hiyo Bw.Wilson Shimo ameanzisha operesheni ya nyumba kwa nyumba huku akiwaonya wananchi wanaofuga makundi makubwa ya fisi kwa shughuli usafiri.
Akizungumzia matukio ya vifo hivyo mkuu huyo wa wilaya anasema tayari fisi ishirini na nane wameuawa katika operesheni hiyo na msako unaendelea usiku na mchana.
Kaimu afisa mifugo na uvuvi wilaya ya Nyangwale Bw. Dickson Msumari anasema fisi hao ni tishio na wamekuwa wakiingia mpaka maeneo ya mjini nyakati za mchana na kuua watoto.
Aidha, Mbunge wa jimbo la nyangwale Hussein Nassoro anasema wameomba nguvu kutoka mkoa Shinyanga ili kuwawinda hao.
Chanzo: ITV
Akizungumzia matukio ya vifo hivyo mkuu huyo wa wilaya anasema tayari fisi ishirini na nane wameuawa katika operesheni hiyo na msako unaendelea usiku na mchana.
Kaimu afisa mifugo na uvuvi wilaya ya Nyangwale Bw. Dickson Msumari anasema fisi hao ni tishio na wamekuwa wakiingia mpaka maeneo ya mjini nyakati za mchana na kuua watoto.
Aidha, Mbunge wa jimbo la nyangwale Hussein Nassoro anasema wameomba nguvu kutoka mkoa Shinyanga ili kuwawinda hao.
Chanzo: ITV