kazuramimba
Senior Member
- Jun 14, 2011
- 126
- 57
Wakuu mliopo hapa mkiwemo wanasheria bobezi hivi ni kweli mmeshindwa kumsaidia bwana kubenea kupambana ili gazeti letu pendwa lirudi uwanjani?Ni jambo la kusikitisha sana kuona hata wanasiasa wakubwa wa upinzani ambao wamejengwa na kutukuzwa na lile gazeti hadi kufika walipo sasa bado wapo kimya.Wapi dk Slaa,Zitto kabwe,Mnyika na Mdee.Ilikwisha tamkwa mara nyingi kuwa ile sheria iliyo tumika si sahihi na ni sheria onevu sasa kinacho shindikana ni kipi? Kama Dowans walifanikiwa kuiburuta hii serikali dhaifu na wakashinda kwani ishindikane kwa mwanahalisi? Mi nadhani muda umefika kwa vyombo vya habari kugoma kwa makusudi hadi kieleweke kwamba mwanahalisi lirudi mtaani na sheria hii kandamizi ifutwe.