Jethro
JF-Expert Member
- Mar 23, 2009
- 2,219
- 371
Gazeti la RAI toleo la leo limejaa makala za kuiponda Chadema na mgombea wake wa urais, na upande mwingine kuifagilia CCM na mgombea wake.
Ni rahisi sana ku-confuse gazeti hili na UHURU au MZALENDO, magazeti ya CCM. Nini kimelisibu gazeti hili pamoja na MTANZANIA? Au ni hofu ya mmiliki wake ROSTAM AZIZ kuwa iwapo mzalendo Dk SLAA ataingia madarakani basi safari yake yake ya kurejea kwao Iran itakuwa imewadia?
Huyu anatuhuma nyingi za kutisha ambazo swahiba wake KIKWETE amekuwa akizifumbia macho. Ni wazi kuwa anawaagiza wanahabari wake kukiuka maadili na kuwa chombo cha propaganda cha CCM badala ya kuwa fair katika kuripoti habari za uchaguzi.
Lakini ethics zinataka chombo cha namna hii kutangaza wazi kwamba kinamuunga mkono mgombea fulani ili wasomaji watambue wanasoma gazeti la aina fulani, badala ya kuwaacha wasomaji wadhanie kwamba ni gazeti huru. Kwa kweli RAI na MTANZANIA yanatia kichefuchefu.
Hii yote ni aibu kwao pia makamba kutangaza kuwa wagombea Ubunge (CCM) wasi shiriki mdahalo wa TBC1 sasa sielewi nini kimewasibu. kwani kutaka kujua strength yako ni muhimu ujipime na competitors wenzako ndipo utajua na pia wananchi wa majimbo mengine nao watatoa maoni. sasa mkikimbia ndio hivyo hivyo mkishinda ubunge hamtokuja wasikiliza wananchi wenu amini hilo na lina ukweli ndani yake.
Kama kweli wagombea kupitia CCM wakimsikiliza katibu-makamba imekula kwao mbaya sana uchaguzi ujao 2015. unajua kampeni hizi ni kutizama 5,10yrs in future sio hapa karibu for 2 yrs tuu jamani, twahitaji viongozi wasio pelekwa pelekwa tuu ati kufuata maaadili ya chama. kumbukeni kuna vijana wanaosoma sasa na wanaiona hii hali na baadae CCM itakuwa sio hii tunayoiona sasa, kuna viongozi au vijana wapya wa CCM watakao kuja watakuwa na challenge kwa waliopo na waliopo watashindwa kabisa kwani wakati huo am sure katiba ya nchi itakuwa mbioni na hata uongozi mzima wa CCM utakuwa tofauti kabisa sijui hatusomi alama za nyakati jamani hii polotics ya sasa itatuletea shida baaadae ati.