Gazeti la MwanaHalisi lafungiwa kwa muda usiojulikana!

nimejitahidi kuangalia post hii kama aimeshareportiwa lakin sijaona.. kama ipo mtanisamehe..mwanahalisi imefungiwa kwa mda usiojulikana kwa kua limekua likiandika habari za kichochezi.

source wapo radio
 
Safi sana Serikali,

Mwalimu Nyerere aliisha sema UHURU BILA MIPAKA NI SAWA SAWA NA WENDAWAZIMU. Hakuna serikali duniani ingeweza kukubali uchonganishi na uzushi wa habari za MWANAHALISI. Na wameisha onywa zaidi ya mara 10 hawasikii, hiyo ndio dawa yao. Sasa Kubenea atafute kazi nyingine, hii ya uandishi amekiuka maadili yake

You are not serious!!
 
Naam, Prof amenena ukweli mchana kweupe. Wwengi tutakuwa wapweke kila jumatano kwa kulikosa. Hata wasio na uwezo wa kulinunua, walizoea kukodolea macho meza za wauza magazeti siku hiyo
 
Banning out Mwanahalisi doesnot make them safe. Their deyz are numbered, it iz just a matter of time.
 
Kubenea tengeneza ID humu JF uwe unatuletea humu,au kama vipi anzisha lingine,maana wamefungia mwanahalisi hajamfungia kubenea,ila wamenikomesha maana tulishatenga bajeti ya mwanahalisi kila jumatano sasa imekula kwangu,mijitu hii ya ajabu sana,ila kubenea fikiria kusajili gazeti lingine,maana spirit ya kuandika ukweli bado ingalipo na kubenea mwenyewe hawajamfungia.tuko pamoja sana
 
nimesiliza bunge muda sio mrefu na Mh. Lissu kajaribu 'kulichomekea' hili suala.

kuna data zimetolewa bungeni juu ya madaktari kwa Afrika Mashariki:
daktari kenya 1:watu 7000; uganda 1:watu 8000; tz 1: watu 50,000.
so, kwa maamuzi ya serikari, hapa hakuna tatizo bali tatizo ni MWANAHALISI!!!!!!
 
Ninachukizwa sana kwa michango ya baadhi ya wanajf

1. Kubenea amefanya kazi yake ya kiuchunguzi. Ametoa data, vielelezo, reference, mazingira nk.

2. Serikali kwa kushindwa na haina pa kuificha aibu wanalifungia mwanahalisi.

Yanayonikera na na kuniuudhi:-

1. Ujinga wa watanzania wengi hum jf kuchangia wakimponda shujaa kubenea.

Tumetamani kwa mda mrefu kupata waandishi wa uchunguzi, amepatikana jasili Kubenea tena kwa ushahidi wanatoke watu wanaponda ....?

2. Nina wasiwasi mkubwa na uwezo wa kufikiri, kutafakari, kutambua na pia uelewa wa baadhi ya wachangiaji hapa jf.
a) Umri pengine ni watoto na kama watu wazima hawajitambui.
b) wamenunuliwa kuchafua mijadala hasa inayolenga kuikosoa serikali.

Ombi langu, ni aibu kubwa sana kwa watu kupinga kila kitu kwa kudhan wanaitetea serikali.

i) wanaoteseka ni wtz.
ii) wanaokufa mahospitalin kwa uzembe wa serikali ni wtz

Watanzania ni kaka, dada, wajomba, bibi na babu zetu.

Kuitetea serikali hii ni kuendeleza mateso na dhiki kwawtz.
 
Sasa sina shaka tena na nadharia ya uhusika wa dola kwa kila kilichompata Uli,kitakachompata kama akipona au asipopona na kitakachompata mbishi yoyote anayethubutu kuhoji KWA NINI? au kutamka neno HAPANA!ama kuulizia HAPO ILIKUWAJE?
wana JF hii inaitwa baptism by fire!Yapo mengi siku zijazo!
 
kweli kabisa mkuu Taharir square ni muhimu sana tena kwa kupigania haki na ukombozi wa nchi wameona hawana jinsi, sasa wanatumia mbavu. Lakini wanacho ni shangaza wamesema gazeti limechapishaa habari zinazo hatarisha amani ya nchi wakashindwa kueleza ni habari gani, kwakweli hapa naona serikali ya mwabepande inazidi kujichanganya yenyewe na kuwafanya watu wafungue macho.

Walisema tuzipuuze mbn gafla wamechange
 

Yaani nyie mmekuwa kama mimi vile.

Nimemchukia sana Kubenea toka ile makala ya tarehe 18/07/2012 kani anapenda sana sifa kwa kusema ukweli kuhusu Serikali.

Anajifanya anajua sana upelelezi sasa si angelienda kuomba kazi Usalama wa Taifa tujue moja kuwa ni mpelelezi.

Kisha upelelezi wake siku zote ni kuivua nguo hadi ya ndani Serikali ya CCM tu, kwanini asipelelezi Majambazi????

SIMPENDI HUYu!!!!!!!!



MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!

gazeti lenu lina chuki,husuda,gubu,na kila aina ya uchafu.linasomwa na watu wanaotumia vichwa kufuga nywele tu badala ya kufikiria.
 
Tuache utani!katika jambo ambalo kikwete angeweza kujivunia na kukumbukwa nalo ni uhuru wa habari.
Uhuru wa watu kutoa maoni umeongezeka sana katika miaka hii ya utawala wa kikwete.
Inawezekana ni kweli jk alidhamiria kuachia uhuru wa habari au alilazimishwa na nguvu za mabadiliko ya upashanaji habari duniani.

Hii ni sifa pekee iliyobakia kuuelezea utawala wa jk kama mwinyi na mkapa walivyoacha sifa za 'ruksa' na 'utandawazi' kila mmojawao.

Ninahuzunishwa sana kuona sifa hii ikianza kutokomezwa taratibu kwa kuangalia mifano mingi ikiwemo hii miwili ya muhimu.

Moja;vyombo cha taifa vya uhabarishaji kama vile TBC na magazeti ya serikali kutoa,kuficha au kupotosha habari kwa manufaa ya watawala na kushindwa kuenenda kama taaluma zao zinavyowataka.wananchi wamepoteza imani na vyombo hivi.

Pili;kufungia au kuonya vyombo vya habari vinavyoandika ukweli dhidi ya matakwa ya serikali huku tukiviacha vyombo vinzvyoandika uongo kwa maslahi ya serikali au chama.

Jk unaipoteza au unapotezewa alama yako muhimu.
Kama una masikio utanisikia!

KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
 
Dah,nashukuru nna nakala ya mwisho ya Mwanahalisi,ila sasa naanza kuamin kuhusu tiss na dr uli
 
Duuuuh profesa kanena! Hapo serikali imejipalia kaa la moto.

Serikali ya visasi.
 
jamani mwenye makala za uchunguzi ziivyoandikwa na gazeti hili juu ya Dr Ulimboka anitumie kwenye PM maana akiziweka hapa mods hawakawiikuzifuta hata kama kuna blog ambayo imeweka naomba link tafadhali...
Nitakutumia
 
Serikali inadai kuwa Mwanahilisi limekuwa "linachapisha habari na makala zenye kueneza na kujenga hofu kwa jamii".
Hivi nini kimeeneza na kujenga hogu kwa jamii, kutekwa na kuteswa kwa Dr Ulimboka na baadae movie ya Kova au taarifa za kichunguzi za gazeti la mwanahilisi?

Jamii imeingia hofu baada ya kuona serikali waliyoipa dhamana ya kuwaongoza imegeuka watekaji wa raia wake ! Mwanahalisi halijawahi kuitia jamii hofu yoyote !
 
mbona radio imani inayohubiri chuki za kidini kila siku haifungiwi?? kuna double standards kwenye media???


Usishangae, double std serikalini kitu cha kawaida sana. Magazeti ya SHigongo yamejaa picha za ajabu ajabu na habari za uzushi lakini yanapeta tu, wanafungia magazeti makini. SHame on this lame government
 
Baada ya serikali kulifungia gazeti la Mwanahalisi leo kwa kile inachosema ni uchochezi na kwamba
Mhariri, mara zote katika utetezi wake amekuwa akinukuu kifungu cha 18 cha Katiba ya nchi yetu ambacho kinatoa uhuru wa kutoa maoni na kwa makusudi kutonukuu kifungu cha 30 cha Katiba hiyo kinachoweka ukomo wa uhuru.


SASA KATIKA KUIPITIA KATIBA KATIKA KIFUNGU HICHO KINASEMA:

The Freedom of Expression

18.- (1) Without prejudice to expression the laws of
of the land, every person has the right to freedom of expression, opinion and expression, and to seek, receive and impart or disseminate information and ideas through any media regardless of national frontiers, and also has the right of freedom from interference with his communications.

(2) Every citizen has the right to be informed at all times of various events in the country and m the world at large which are of importance to the lives and activities of the people and also of issues of importance to society:



MY OPINION:

Kubenea amejaribu kutumia haki yake hiyo, na kuhakikisha mwananchi mmojammoja anapata haki yake ya kupata habari inayohusu Taifa lake au matukio yanayojiri.

UKOMO WA HAKI HIYO KATIKA KATIBA:

Limitations

30.-(1) The human rights and freedoms, the principles of which are set out in this Constitution, shall not be exercised by a person in a manner that causes interference with or curtailment of the rights and freedoms of other persons or of the public interest
.

TUJIULIZE:

Kwa kuzingatia kwamba hakuna mtu aliye juu ya sheria, Hivi swala la kujua kilichomtokea Dr. Ulimboka sio interest of the public? Vyombo vya serikali hapa hofu yao ni nini? kama sio kweli basi si afadhali habari au taarifa za kweli zitolewe kukanusha habari ya gazeti la Mwanahalisi kabla ya kulifungia gazeti?
What is the public interest in this matter?

Naomba kuwasilisha.
 
Back
Top Bottom