mbayumbayu
Senior Member
- Jan 25, 2012
- 110
- 82
Mkuu siku ya kwenda kuchukua hiyo hundi yako nenda na kadi yako ya ATM kabisa maana wakikukata na kodi ya zuio (withholding tax) balance haikutoshi nauli na lunch ya siku hiyo. Hamna jinsi utaingia ATM tu. Labda ujiongeze uwe na hisa angalau 500,000Leo nimepewa taarifa kuwa katika kikao cha Wanahisa kilichokaa mjini Arusha imeamuliwa kuwa gawio la kila hisa iwe shs. 10. Haingii akilini kwangu kutokana na faida ya Tshs.75bn iliyopatikana gawio inakuwa shs.10 kwa hisa moja. Ninatarajia kuuza hisa zangu zipatapazo 3500 ili nichukue ustaarabu mwingine. Ina maana katika hisa zangu 3500 gawio langu ni shs.35,000 bado kodi. Kwangu naona kama tusi. Hata akaunti yangu nitahamisha kutoka CRDB.