Gari la msafara wa IGP Sirro laua Morogoro

Gari la msafara wa IGP Sirro laua Morogoro

Jackline Samwel (9), amefariki dunia leo Alhamisi Desemba 12, 2019 baada ya kugongwa na gari lililokuwa katika msafara wa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro mkoani Morogoro.

Akizungumza na Mwananchi leo kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Mugabo Wekwe amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, “ni kweli ajali imetokea leo saa 4 asubuhi eneo la Kwa Makunganya.” Amesema Jackline ni mwanafunzi wa darasa la tatu shule ya Msingi Mbwanga mkoani Dodoma, kwamba amegongwa na gari la msafara huo wakati akivuka barabara eneo la Kwa Makunganya manispaa ya Morogoro.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema mwanafunzi huyo aligongwa na gari wakati akivuka barabara baada ya kutoka kununua maji akiwa na mama yake mdogo na ndugu zake wengine watatu.

Wanaeleza kuwa baada ya wenzake kuvuka kurejea katika basi la kampuni ya ABC walilokuwa wakisafiria kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam, yeye alikuwa wa mwisho kuvuka ndipo alipogongwa na gari hilo na kufariki dunia.

Kaimu kamanda huyo amesema mwili wa mwanafunzi huyo umehifadhiwa Hospitali ya rufaa Mkoa wa Morogoro.

Nimekutana na hiyo ajali maeneo ya makunganya kwa matraffick pale ni seme tu traffic pia hawakuwa makini kwani imetokea mbele yao hawakutoa taadhari abiria walioshuka kwenye gari.

Mtoto alirushwa juu dah RIP binti, inaonekana mama alikuwa naye ni mlezi na ndiyo alikuwa anamsomesha alimuwa analia sijui atamwambia nini mwenye mtoto.
 
Sad! Kwani lazima IGP akimbie kwa kasi bila kuchukuwa tahadhari? Driver aliyegonga hakuona basi na watu? Kwanini hakuchukuwa tahadhari kwa kupuunguza mwendo???????
Jackline Samwel (9), amefariki dunia leo Alhamisi Desemba 12, 2019 baada ya kugongwa na gari lililokuwa katika msafara wa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro mkoani Morogoro.

Akizungumza na Mwananchi leo kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Mugabo Wekwe amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, “ni kweli ajali imetokea leo saa 4 asubuhi eneo la Kwa Makunganya.” Amesema Jackline ni mwanafunzi wa darasa la tatu shule ya Msingi Mbwanga mkoani Dodoma, kwamba amegongwa na gari la msafara huo wakati akivuka barabara eneo la Kwa Makunganya manispaa ya Morogoro.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema mwanafunzi huyo aligongwa na gari wakati akivuka barabara baada ya kutoka kununua maji akiwa na mama yake mdogo na ndugu zake wengine watatu.

Wanaeleza kuwa baada ya wenzake kuvuka kurejea katika basi la kampuni ya ABC walilokuwa wakisafiria kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam, yeye alikuwa wa mwisho kuvuka ndipo alipogongwa na gari hilo na kufariki dunia.

Kaimu kamanda huyo amesema mwili wa mwanafunzi huyo umehifadhiwa Hospitali ya rufaa Mkoa wa Morogoro.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
*pole wafiwa

*meona basi la modern kwenda mombasa yamegongana na vifo vimetokea (mabasi ya kampuni moja yanagongana ...waeza waza na kukosa majibu)

mwaka unayoyoma ...19 days
 
Mtoto haachwi nyuma jamanii dah mnanikumbusha machungu ya mwangu
 
Mkuu Sirro sheria ni msumeno , nenda kituo cha polisi cha karibu ukaandike maelezo
 
Igp ashtakiwe kwa kusababisha ajali. Kwani hakuwaelekeza madereva wa msafara wake waendeshe kwa kuzingatia alama za barabarani? Awajibike!
Kwani IGP ndo alikuwa anaendesha hilo gari? Hadi ashtakiwe? Halafu toka lini IGP akawa muongoza magari ya msafara wake?
 
Ingekua ni dereva mwingine wa kawaida tu taarifa hiyo ya ajali ingeendelea kwa kusema "Dereva wa gari lililosababisha ajali anashikiliwa na polisi". Lakini hapo nadhani protokali itavunjwa
 
Kwani IGP ndo alikuwa anaendesha hilo gari? Hadi ashtakiwe? Halafu toka lini IGP akawa muongoza magari ya msafara wake?
Yeye ndiye msababishaji mkuu kwani bila yeye kupita hapo na msafara wake binti yule angekuwa salama! Na kwani atembee na convoy kana kwamba yupo Somalia? Gari mbili- zinamtosha kwenye msafara wake na siyo gari 10!
Wanasheria mnakwama wapi kupata kick kwa kumfungulia kesi huyu igp?
 
Back
Top Bottom