Afisa Mteule Drj 2
JF-Expert Member
- Mar 21, 2017
- 3,961
- 4,663
Da yani wanakufa watu wa maana,kina gentamycine wanabaki tu,bora angetwaliwa gentamycine
Jackline Samwel (9), amefariki dunia leo Alhamisi Desemba 12, 2019 baada ya kugongwa na gari lililokuwa katika msafara wa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro mkoani Morogoro.
Akizungumza na Mwananchi leo kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Mugabo Wekwe amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, “ni kweli ajali imetokea leo saa 4 asubuhi eneo la Kwa Makunganya.” Amesema Jackline ni mwanafunzi wa darasa la tatu shule ya Msingi Mbwanga mkoani Dodoma, kwamba amegongwa na gari la msafara huo wakati akivuka barabara eneo la Kwa Makunganya manispaa ya Morogoro.
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema mwanafunzi huyo aligongwa na gari wakati akivuka barabara baada ya kutoka kununua maji akiwa na mama yake mdogo na ndugu zake wengine watatu.
Wanaeleza kuwa baada ya wenzake kuvuka kurejea katika basi la kampuni ya ABC walilokuwa wakisafiria kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam, yeye alikuwa wa mwisho kuvuka ndipo alipogongwa na gari hilo na kufariki dunia.
Kaimu kamanda huyo amesema mwili wa mwanafunzi huyo umehifadhiwa Hospitali ya rufaa Mkoa wa Morogoro.
Jackline Samwel (9), amefariki dunia leo Alhamisi Desemba 12, 2019 baada ya kugongwa na gari lililokuwa katika msafara wa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro mkoani Morogoro.
Akizungumza na Mwananchi leo kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Mugabo Wekwe amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, “ni kweli ajali imetokea leo saa 4 asubuhi eneo la Kwa Makunganya.” Amesema Jackline ni mwanafunzi wa darasa la tatu shule ya Msingi Mbwanga mkoani Dodoma, kwamba amegongwa na gari la msafara huo wakati akivuka barabara eneo la Kwa Makunganya manispaa ya Morogoro.
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema mwanafunzi huyo aligongwa na gari wakati akivuka barabara baada ya kutoka kununua maji akiwa na mama yake mdogo na ndugu zake wengine watatu.
Wanaeleza kuwa baada ya wenzake kuvuka kurejea katika basi la kampuni ya ABC walilokuwa wakisafiria kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam, yeye alikuwa wa mwisho kuvuka ndipo alipogongwa na gari hilo na kufariki dunia.
Kaimu kamanda huyo amesema mwili wa mwanafunzi huyo umehifadhiwa Hospitali ya rufaa Mkoa wa Morogoro.
haya magari ya msafara yana mwendo wa kasi sana sijui wanawahi wapi?
Kwani IGP ndo alikuwa anaendesha hilo gari? Hadi ashtakiwe? Halafu toka lini IGP akawa muongoza magari ya msafara wake?Igp ashtakiwe kwa kusababisha ajali. Kwani hakuwaelekeza madereva wa msafara wake waendeshe kwa kuzingatia alama za barabarani? Awajibike!
Yeye ndiye msababishaji mkuu kwani bila yeye kupita hapo na msafara wake binti yule angekuwa salama! Na kwani atembee na convoy kana kwamba yupo Somalia? Gari mbili- zinamtosha kwenye msafara wake na siyo gari 10!Kwani IGP ndo alikuwa anaendesha hilo gari? Hadi ashtakiwe? Halafu toka lini IGP akawa muongoza magari ya msafara wake?