Gari la Lema lashambuliwa na UVCCM - Arusha

Gari la Lema lashambuliwa na UVCCM - Arusha

Crashwise

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2007
Posts
22,227
Reaction score
8,760
Akiwa anaekekea nyumbani kwake Mbunge Wa Arusha Mjini Mhe. Godbles Lema ameshambuliea na vijana wa uvccm maeneo ya clock Tower,..kuna watu wameumia katika tukio hilo ambalo vijana wa ccm walimvamia lema wakiwa na mashoka, panga na mipini..
===============

Lema: Machokoraa waliotumwa na CCM walitaka kuniua

Siku moja kabla ya uchaguzi wa wenyeviti wa Serikali za Mitaa, Mbunge wa Arusha, Godbless Lema, amesema amenusurika kuuawa baada ya kuvamiwa na vijana wa mitaani waliokuwa na mapanga, marungu na mafyekeo.

Alisema tukio hilo lilitokea jirani na kituo kimoja cha mafuta kilichopo eneo la mzunguko wa Mnara wa Saa majira ya saa 1:30 jioni, wakati kundi hilo alilodai kuwa ni machokora linalotumiwa na CCM kutaka kuvuruga uchaguzi.

Alisema alipofika maeneo hayo alishuka kwenye gari lake kwa lengo la kumsaidia mtu aliyekuwa amevamiwa akipigwa na vibaka hao na ndipo walipomgeukia na kusema kuwa ndiye waliyekuwa wamkitafuta.

"Mimi nimekuwa mhanga wa uvamizi wa kundi hili na polisi walishuhudia kundi hili likiwa na mapanga, marungu na silaha mbalimbali zinazoweza kutumika kwa kudhuru na kuharibu mali na maisha ya binadamu.

"Ni watoto wa mitaani, wanaolala kwenye takataka, pembeni mwa uwanja wa mpira na maeneo mengine…hao ndio wanaotumiwa na CCM sasa hivi ili kuleta vurugu.

"Nililazimika kupiga risasi tatu hewani lakini bado walikuwa wakinifuata, nikajitahidi kujinusuru lakini walifanikiwa kuharibu gari langu kwa kuvunja kioo cha nyuma," alisema na kuongeza alitoa taarifa ya tukio hilo polisi na kufunguliwa faili namba AR/RB/16/681/14.

Alisema vijana hawa wasipodhibitiwa uchaguzi huo utakuwa na vurugu.
"Mimi mbunge naomba kutoa tahadhari kwamba genge hili lisipodhibitiwa sasa, ninaona mashaka na hatari kubwa itakayoweza kutokea 14/Desemba/2014 na kusababisha mauaji makubwa," alisema.

Alisema maeneo yote ya Arusha yanahitaji ulinzi wa hali ya juu lakini maeneo kama Sekei, Ngarenaro, Sombetini, Elerai, Unga Ltd, Daraja Mbili, Olasiti, Sokoni 1, Murriet, Kaloleni na Kata ya Kati yanahitaji uangalizi maalum wa kiulinzi juu ya tetesi na mipango mibaya inayopangwa huko.

Akizungumzia tuhuma za Lema, Katibu wa CCM Wilaya ya Arusha, Feruzi Bano, alisema chama chake katu hakiwezi kuwatumia vijana machokoraa kumdhuru mbunge huyo.

"Huyu ni mbunge wetu hatuna shida naye, huu ni uchaguzi wa Serikali za Mitaa, sasa kwa nini tuwe na nia ya kumdhuru…unajua huyo kila unapokuja uchaguzi anazua mambo na tuhuma hizi sio za kweli kabisa," alisema.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Daud Felix Ntibenda, alisema suala la madai ya kuvamiwa kwa mbunge Lema, linashughulikiwa na vyombo vya usalama.
Chanzo: Nipashe
 
Akiwa anaekekea nyumbani kwake Mbunge Wa Arusha Mjini Mhe. Godbles Lema ameshambuliea na vijana wa uvccm maeneo ya clock Tower,..kuna watu wameumia katika tukio hilo ambalo vijana wa ccm walimvamia lema wakiwa na mashoka, panga na mipini..

Naona wamechokoza sehemu isiyo sahihi ole wao naona wamebep ngoja tuwapigie.
 
Akiwa anaekekea nyumbani kwake Mbunge Wa Arusha Mjini Mhe. Godbles Lema ameshambuliea na vijana wa uvccm maeneo ya clock Tower,..kuna watu wameumia katika tukio hilo ambalo vijana wa ccm walimvamia lema wakiwa na mashoka, panga na mipini..
Tafadhali sana mkuu. Taarifa yako haijakamilika ipasavyo. Hebu toa taarifa kwa kina na mapana yake mkuu ili tuelewe kwa nini wapuuzi hao wamefanya hivyo.
 
Hii inaonyesha CCM hawako tayari kukubali kushindwa. Itabidi tujiandae vilivyo mwakani.
 
Wakuu,

Taarifa za muda huu ni kwamba CCM wamevamia gari la Mh. Mbunge wa Arusha mjini maeneo ya Clock Tower wakati anaelekea nyumbani kwake njiro.
Wakati anapita Mnara wa saa, ghafla wakatokea maccm yakiwa na watu wenye sura ngumu kama banyamulenge, wakaanza kushambulia gari la mbunge huku wakimweleza kwamba wewe ndiye nuksi hapa Arusha, lazima tukukomeshe. Bahati nzuri wakatokea wananchi wazalendo wakaanza kuwashambulia hao banyamulenge wakakimbia zao.

Hivi sasa Mh Lema anaandika maelezo polisi
 
Akiwa anaekekea nyumbani kwake Mbunge Wa Arusha Mjini Mhe. Godbles Lema ameshambuliea na vijana wa uvccm maeneo ya clock Tower,..kuna watu wameumia katika tukio hilo ambalo vijana wa ccm walimvamia lema wakiwa na mashoka, panga na mipini..

Nani amshambulie jambazi mkongwe kiasi hicho! hao ni wezi wenzake amewa stage ili kujipa promo baada ya kugundua wana A.Town wamemstukia na wanataka kumtosa ubunge kwa kuwadanganya mambo mengi na yote kuishia kwenye maandamano yanayokosesha wananchi vipato kwa vurugu na kupora mali.
 
Akiwa anaekekea nyumbani kwake Mbunge Wa Arusha Mjini Mhe. Godbles Lema ameshambuliea na vijana wa uvccm maeneo ya clock Tower,..kuna watu wameumia katika tukio hilo ambalo vijana wa ccm walimvamia lema wakiwa na mashoka, panga na mipini..
Kwanini usingetumia kichwa kufikiri ili uandike kitu cha kueleweka. Hebu proof read ujikosoe kabla hatujakukosoa mana tutakupopoa mawe
 
Hao ccm wametoka wapi?si mlisema ccm imefutwa kabisa arusha,nyie muulizeni vizuri amemdhulumu nani.
 
nikiwa ofisini karibu na kitu cha mafuta cha oryx clock tower nimesikia milio ya risasi waliokuwepo ni mbunge lema na wafusi wa ccm,watu hawa wa ccm walikua na marungu, kama kuna mwenye taarifa zaidi atusaidie!!
 
Back
Top Bottom