Naomba kujua sababu ya gari kuchemsha (overheat)

Mkuu kuhusu hedi mpk kutoa moshi ndio exactly nilioexpirians hadi leo najaza maji tu na kuchapa mwendo naomba unielewshe solution ipoje na garama kwa makisio bcs sina uelewa kuhusu magari . Nitashkuru sm ukinijibu.
Inabidi utafute fundi aifumue injini aangalie kama hedi ipo/zipo flat kulingana na vipimo vilivyowekwa na waundaji (manufacturer).

La sivyo itabidi utumie gharama zaidi kuirudisha hedi kwenye ubora wake wa mwanzo. Gharama yake kwakweli sifahamu kwa kuwa nipo nje ya nchi.
 
Yap kunaweza kusababisha engine kuchemsha

Ngoja nikupe elimu kidogo

Maji hayapoozi engine moja kwa moja ila yanapooza kama ifuatavyo:-

Oil inakazi tatu nazo ni
1.kuleta mlainisho wa vyuma
2.kusafisha engine
3.kupooza engine

Hapo kwenye kupooza engine ipo ivi:-

Oil inapozunguka kwenye engine inakutana na joto na ukisoma theory ya tempature inasema iv:-
Joto husafiri kutoka sehem yenye joto kubwa kuelekea kwenye sehem au chombo chenye joto dogo(heat transfer)

Kwaiyo oil inagain heat kutoka kwenye engine

Oil hiyo hupoozwa na maji au coolant hali ambayo hupelekea kupungua kwa joto la engine kwasababu oil huingia katika engine ikiwa na joto kidogo na hutoka na joto jingi kitendo ambacho tunaweza kusema oil husafirisha joto kutoka kwenye engine.

Kwaiyo oil hiyo isipopoozwa vizuri jawabu lake ni engine kutopoozwa vizuri jambo ambalo hupelekea engine kupatwa na joto losilo la kawaida

Note. Maji hayaiingii kwenye engine moja kwa moja kwasababu ya tabia yake ya kuweza kusababisha kutu(corrosion) hivyo oil hutumika kama chambo tu


Kama hujaelewa uliza kipengele ambacho unahitaj maelezo zaid ili nikupatie
Mkuu hebu rudia kusoma reference zako, kazi ya cooling ni ya maji au coolant. Jaribu kukagua engine uone pipes za maji kutoka kwenye rejeta zinaingia wapi. Check water pump thermostat nk. Kwa kifupi kwenye engine kuna njia za maji kama wengine walivyoeleza. Cylinder head gasket ina njia za maji na oil na ndiyo maana gasket ikiungua maji na oil vinachanganyika. Pia tatizo la gasket husababisha compression inayopotea kutokea njia za maji hivyo inapush maji nje yanakuwa hayakai mwenye rejeta
 
Sababu kubwa ni kutu kutokana na kutumia maji ya bomba. Baada ya hapo inakuwa ni ama water pump au thermostat failure ambazo pia husababishwa na hiyo kutu. Zaidi ya hapo labda itakuwa ni serpentine belt kuchakaa kiasi kuwa haizungushi pump sawasawa.
 
Mkuu hebu rudia kusoma reference zako, kazi ya cooling ni ya maji au coolant. Jaribu kukagua engine uone pipes za maji kutoka kwenye rejeta zinaingia wapi. Check water pump thermostat nk. Kwa kifupi kwenye engine kuna njia za maji kama wengine walivyoeleza. Cylinder head gasket ina njia za maji na oil na ndiyo maana gasket ikiungua maji na oil vinachanganyika. Pia tatizo la gasket husababisha compression inayopotea kutokea njia za maji hivyo inapush maji nje yanakuwa hayakai mwenye rejeta
Mi gar yangu naona kama Coolant inaisha haraka kuliko kawaida. Shida inaweza kuwa ni nini??
Gari ni Carina Ti.
 
Radiator yako ni ya njia ngapi kuna 3 na 4, hii njia nne hainaga headache. Kwa masafa ya mbali kulinganisha na Engine yako utasahau lakini kuna kitu inaitwa gasket cylinder head kama haipo poa inapitisha maji au hewa hapo dili na engine kwanza hususani kwa engine ambayo ilishafunguliwa
Mimi Gari yangu ni Vitz 2001.Ilikuwa inachemsha nikabadili radiator nikaweka used radiator, ikawa inachemsha Kwa umbali mfupi zaidi.Ikasafishwa ikafungwa Tena.Kwasasa Nina uwezo wa kwenda kutoka airport paka Magomeni Na kurudi hila Maji yanapungua.Natumia maji ya kawaida Na Thermostat ilitolewa.
Nini shida?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na kuondoa Thermostat kwenye gari mfano Vitz vvti engine.haiwezi kuwa shida ya kufanya Maji kupotea Na hatimae Engine kuchemsha?
Gari aina gani? Angalia mfuniko wa redetor unaweza kua unavuja afu kuna kitu inaitwa themostart kama aifungui gari inachemsha sehemu zenye joto uwa zinatolewabkabisa ili maji yazunguke free

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hebu rudia kusoma reference zako, kazi ya cooling ni ya maji au coolant. Jaribu kukagua engine uone pipes za maji kutoka kwenye rejeta zinaingia wapi. Check water pump thermostat nk. Kwa kifupi kwenye engine kuna njia za maji kama wengine walivyoeleza. Cylinder head gasket ina njia za maji na oil na ndiyo maana gasket ikiungua maji na oil vinachanganyika. Pia tatizo la gasket husababisha compression inayopotea kutokea njia za maji hivyo inapush maji nje yanakuwa hayakai mwenye rejeta
Mimi nashauriwa nibadili cylinder head gasket lakini Kwa utaalamu wako kuwa kama ikiungua Maji Na oil ujichanganya nafikiri haijaungua.Maana Maji yapo meupe kabisa.Labda nianze kutumia coolant Na pia nirudishe Thermostat.Maana Nina uwezo wa kutola airport paka kinondoni bila gari kuchemsha hila maji yanapungua.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
.
Hii ni basis ya cooling system ambayo inafanywa na thermostat.

.
Naelewa kuhusu heater ya engine block, na hii siyo magari yote yapo 'equipped'. Ni kwa magari yanayouzwa kwenye 'coldest regions' kama Alaska. Na hii unachomeka cable kutoka kwenye gari kwenda kwenye outlet ya garage (nyumbani) na ku 'heat engine block' kwa muda kabla ya kuiwasha gari. kama haupo karibu na 'electric outlet' kuwezi kufanya hivyo.

Ila usibishe ndugu, maji yanaganda yakifikia 'freezing point' majimaji yaliyoko kwenye radiator yanaganda joto la nje likifika 0°C. Na maji yakiganda yanatanuka (anomalous expansion of water). Kwahiyo raidator inaweza kupasuka pembeni (radiator nyingi zina plastic pembeni) kama maji yakiganda, ndiyo maana kwenye nchi za baridi coolant inashauriwa wakati wa winter.


.
Hii inategemea na engine design, kwa upande wa magari (4 stroke engine), 'coolant' hutumika zaidi (effectively) kupoza , ndiyo maana wakaiita COOL-ant (kipozeo), inayozungukakwenye 'waterjackets'. Hizi huwa zinajaa maji wakati wote ili 'ku transfer excess heat' (moja kwa moja) kutoka kwenye block kwenda kwenye maji.

Oil kazi yake kubwa ni kulainisha 'rod bearings' na 'crankshaft' kwasababu hapa ndo kuna 'maximum turning effect (torque)'. Ndiyo maana kama oil ni kidogo sana, utaanza kusikia 'rod knock'. Pia oil inalainisha 'camshaft' na lifters' kwenye 'cylinder head'.

Oil ni 'viscous' kuliko maji, haiwezi ika 'tranfer heat efficiently' kama maji.

Oil kweli inaweza inapoza engine lakini siyo kiivyo, njia inayopita oil ndani ya engine ni nyembamba kwahiyo ufanisi wake wa kupoza ni mdogo.

kuna magari yenye 'oil cooler', hii yanasaidia kupoza oil kwa kuitoa nje ya engine na kuipoza kwa 'heat exchanger' aidha kwa kutumia upepo (mbele ya gari) au kwa kutumia 'coolant' na kuirudisha kwenye engine ikiwa imepoa. kawaida hii ni kwa 'performance vehicles' (BMW) ambazo zina 'run at high temperatures' (105°C). Oil ikiwa kwenye joto kali huanza kupungua uwezo wake wa kulainisha (viscosity decrease with temperature).

Kwahiyo upozwaji wa oil siyo kwaajili ya kupoze engine bali kuhakikisha oil ina-'maintain it's molecular structure'.

Mkuu samahani kdg..
Rod nock unaiskiaje kama oil ni kidogo.. yaani mlio gani unasikia?


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inabidi utafute fundi aifumue injini aangalie kama hedi ipo/zipo flat kulingana na vipimo vilivyowekwa na waundaji (manufacturer).

La sivyo itabidi utumie gharama zaidi kuirudisha hedi kwenye ubora wake wa mwanzo. Gharama yake kwakweli sifahamu kwa kuwa nipo nje ya nchi.

Bado upo nje ya nchi?
 
Sababu kubwa ni kutu kutokana na kutumia maji ya bomba. Baada ya hapo inakuwa ni ama water pump au thermostat failure ambazo pia husababishwa na hiyo kutu. Zaidi ya hapo labda itakuwa ni serpentine belt kuchakaa kiasi kuwa haizungushi pump sawasawa.

Mie mbona siku zote natumia maji ya bomba mwendo mdundo na engine ipo fiti kalikiti?
 
Mie mbona siku zote natumia maji ya bombs mwendo mdundo na engine ipo fiti kalikiti?
injini haiko fiti hito; itakufa haraka kabla ya muda wake. Pole pole itajaa kutu na baadaye matundu ya kupoozea yataanza kuziba na injini kuwa ya spana mkononi. Kuna wakati utakuwa unatakiwa kuongezea maji mara kwa mara badala ya kujaza mara moja na kusahahu hadi wakati wa serive nyingine. Ndiyo hiyo ilivyokuwa kwa madereva wa daladala kutembea na geleni la maji!!
 
injini haiko fiti hito; itakufa haraka kabla ya muda wake. Pole pole itajaa kutu na baadaye matundu ya kupoozea yataanza kuziba na injini kuwa ya spana mkononi. Kuna wakati utakuwa unatakiwa kuongezea maji mara kwa mara badala ya kujaza mara moja na kusahahu hadi wakati wa serive nyingine. Ndiyo hiyo ilivyokuwa kwa madereva wa daladala kutembea na geleni la maji!!
Mkuu habari.
Nimechunguza pale nikifungua mfuniko wa Radiator kutu imejaa. Natumia maji ya bomba kwa muda mrefu.

Je inawezekana maji yote yakaondolewa na system nzima ikasafishwa kutu yote inaondoka? Nataka nianze kutumia Coolant ama nishachelewa/haiwezekan
 
Back
Top Bottom