Gaddafi.....the man!

Nachukizwa sana na viongozi wetu Africa. Ni wanafiki sana, hawana misimamo, wanauza uhuru kwa maslahi binafsi. Tumeona haya kwa Mugabe na sasa Gadafi. Congo wamarekani wanashabikia vita huku wakiiba utajiri wa wananchi wake. Libya kwa kutumia branketi la demakrasia wanaisambaratisha nchi, watu wake na uchumi wake ili waendelee kututawala na kutuibia. Na sishangai urafiki wao hata kwa nchi kama Tanzania utapelekea kupata mkong'oto tu siku moja ili wachukue mali zetu. Jamaa asili yake Kenya. Iweje aipende Tanzania zaidi kuliko aliko na nasaba? Ama kweli, wajinga ndio wali wao.
 
Eeh Mwenyezi Mungu usiyelala wala kusinzia tunakuomba uwape faraja Ndugu zetu wa Libya pamoja na Kiongozi wao katika wakati huu mgumu wa hujuma, uonevu na ufedhuli unaofanywa na wanaojiita wababe wa hii dunia. Wanadhani wana nguvu kuliko wewe. laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie wote wanaoendeleza hujuma hii kwani wanaoathirika ni kina mama na watoto wasio na hatia. Laana tu llahi...
 
Hamsini zake zimefika...aanze kujiandaa na lolote maana Sadam alinyolewa ndevu, Osama risasi ya jicho...huyu bwana atanyolewa nywele ili ajue uhuni dunia hii haulipi
 
Naafiki mkuu!
Japo kosa kubwa alilolifanya ni kukaa madarakani muda mrefu lakini tuache unafiki kidogo.
Malkia wa Uingereza kakaa madarakani toka 1953 na anataka kumuachia nchi mjukuu wake!!!
Mfalme Feisal wa Saudi Arabia mbona Marekani hawamgusi?
Leo jamaa wanafanya mazoezi ya mizinga na target practice nchi ya Libya na kuua watu wasio na hatia.
 

Mgogoro wake na wazungu ndio tupeleke wanajeshi wetu wakafe? Acha tusolve matatizo yetu ya ndani, kwanza hata Commoro hatukupaswa kupeleka wanajeshi wetu. Yote kwa yote acha wafu wazikane
 

Maslahi Mkuu ,Maslahi hamna chochote zaiiiiidi.
Pamoja na mabaya yake lakini yapo mazuri aliyoyafanya LIBYA, Kosa lako ni kugeuza Libya mali yake tu basi. Hawarudishie nchi wenye nayo,Kama anaitakia mazuri Libya aondoke kimya kimya, Akiondoka kwa nguvu atawapisha Washenzi watakuja kukomba kama IRAQ.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…