econonist
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 22,138
- 32,716
Gabriel Mwita wa CHADEMA unataka Nini?
Nina swali moja Kwa huyu kada wa CHADEMA Gabriel Mwita , Je Gabriel Mwita unataka Nini?.
Kwanza, nakuuliza Gabriel Mwita unataka nini kwa sababu maamuzi ya kupitishwa kwa tamko la no reforms no election yalifanywa na vikao vyote halali vya Chama. Kuanzia Kamati kuu, Baraza Kuu na hatimaye Mkutano Mkuu wa Chama. Leo mnataka Chama kubadilisha maamuzi yake kisa wanachama 55 wanataka kugombea ubunge na udiwani?. Yani shida yako ni kugombea ubunge bila kuangalia mapungufu ya kwenye mfumo wetu wa uchaguzi. Haya bwana.
pili, nakuuliza Gabriel Mwita unataka nini kwa sababu uligombea ubunge Musoma mjini mwaka 2020 na unajua ulichofanyiwa kwenye ule uchaguzi ukaanguka. Ikumbukwe Musoma mjini ndio Jimbo pekee Tanzania Bara ambapo Rais Magufuli alipata kura chache zaidi kuliko majimbo mengine yani asilimia 55 tu ya kura na hapo ni baada ya kuiba Sana.
Wewe mwenyewe Gabriel ulilalamika kuchezewa faulo na CCM, lakini leo nashangaa unataka kugombea ubunge kwenye mazingira yale yale. Najiuliza shida ni nini?. Ni kweli unataka kugombea ubunge au una jambo lako mwenyewe moyoni baada ya kuwekwa pembeni na chama? Maana watu wanakupigania upate nafasi nzuri ya kushiriki uchaguzi katika mazingira bora yenye haki ila wewe una wakebehi na kuwaona hawafai.
Haya bwana.
Tatu, nakuuliza wewe Gabriel Mwita unataka nini maana mwaka 2024 kulikuwa na shinikizo la CHADEMA kutoshiriki uchaguzi wa serikali za mitaa, ila baadae Kamati Kuu chini ya Mh Mbowe ikapitisha azimio la kushiriki uchaguzi ule. Wewe mwenyewe ni shahidi kwa yaliyotokea, sina haja ya kuongea maana yalikuwa wazi. Je mnataka turudi huko?
Na nikuambie tu mkishiriki uchaguzi huu, dola itawabamiza hakuna na hakuna atakayewaonea huruma mkisiginwa na dola maana mnashiriki uchaguzi huku mkijua matokeo yake ni yepi. Sasa hiyo ni akili au matope? Unaenda kushiriki uchaguzi ambao unajua kushinda ni ndoto kutokana na mazingira mabovu.Kama unashiriki uchaguzi ilimradi ushiriki na sio kushinda kazi kwako bwana Gabriel Mwita.
Mwisho naomba nikushauri mambo matau yafuatayo Ndugu Gabriel Mwita:
1. Kama unataka kukijenga chama na kuwa kiongozi mkubwa wa chama huko mbeleni, Jenga tabia ya kuheshimu vikao vya chama. Vikao vyote halali vimekubali chama kisishiriki uchaguzi mkuu kama hakuna mabadiliko kwenye madhaifu yaliyopo kwenye sheria na mfumo wa uchaguzi Tanzania. Inakuaje leo unalazimisha chama kubadilisha mwelekeo ghafla baada ya Mkutano Mkuu kuridhia?. Huo ni utovu wa nidhamu na kiburi.
2. Kama unataka kugombea ubunge na unaona una ushawishi wa kushinda , tafuta chama kinachokubalika hata CCM , NCCR kagombee, maana kugombea ni haki yako siyo lazima iwe CHADEMA. Kuendelea kulazimisha unataka ugombeee kupitia CHADEMA huku ukijua kwa Sasa chama kinapambania mabadiliko kwenye mfumo wa uchaguzi inaonesha wewe una lako jambo kama sio kirusi ndani ya chama.
3. Kama unaona Chama kilifanya maamuzi yasiyo sahihi , nafasi uliyonayo ni kuomba mkutako mkuu wa dharura kupitia njia ya kikatiba ambapo Jambo lako litajadiliwa na likionekana ni la msingi chama kitabadilsha msimamo na kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Soma Pia: CHADEMA yamng'oa Katibu wa Sekretarieti wa chama, Julius Mwita baada ya kuibuka mzozano kwenye kundi sogozi
kwa kukuaga tu, nakushauri ya kwamba usiongee yote ukamaliza maana kwenye siasa hujui litatokea nini kesho. Leo waweza kuona sifa kwa kumshambulia Mh. Lissu ila kesho mamlaka yaweza kukubaliana na hoja za Lissu na kukaa meza moja kubadilisha mfumo wote wa uchaguzi, mtafanyaje?
Kesho nitajibu hoja zako zote ulizitoa kwenye press ya leo.
Asante
Nina swali moja Kwa huyu kada wa CHADEMA Gabriel Mwita , Je Gabriel Mwita unataka Nini?.
Kwanza, nakuuliza Gabriel Mwita unataka nini kwa sababu maamuzi ya kupitishwa kwa tamko la no reforms no election yalifanywa na vikao vyote halali vya Chama. Kuanzia Kamati kuu, Baraza Kuu na hatimaye Mkutano Mkuu wa Chama. Leo mnataka Chama kubadilisha maamuzi yake kisa wanachama 55 wanataka kugombea ubunge na udiwani?. Yani shida yako ni kugombea ubunge bila kuangalia mapungufu ya kwenye mfumo wetu wa uchaguzi. Haya bwana.
pili, nakuuliza Gabriel Mwita unataka nini kwa sababu uligombea ubunge Musoma mjini mwaka 2020 na unajua ulichofanyiwa kwenye ule uchaguzi ukaanguka. Ikumbukwe Musoma mjini ndio Jimbo pekee Tanzania Bara ambapo Rais Magufuli alipata kura chache zaidi kuliko majimbo mengine yani asilimia 55 tu ya kura na hapo ni baada ya kuiba Sana.
Wewe mwenyewe Gabriel ulilalamika kuchezewa faulo na CCM, lakini leo nashangaa unataka kugombea ubunge kwenye mazingira yale yale. Najiuliza shida ni nini?. Ni kweli unataka kugombea ubunge au una jambo lako mwenyewe moyoni baada ya kuwekwa pembeni na chama? Maana watu wanakupigania upate nafasi nzuri ya kushiriki uchaguzi katika mazingira bora yenye haki ila wewe una wakebehi na kuwaona hawafai.
Haya bwana.
Tatu, nakuuliza wewe Gabriel Mwita unataka nini maana mwaka 2024 kulikuwa na shinikizo la CHADEMA kutoshiriki uchaguzi wa serikali za mitaa, ila baadae Kamati Kuu chini ya Mh Mbowe ikapitisha azimio la kushiriki uchaguzi ule. Wewe mwenyewe ni shahidi kwa yaliyotokea, sina haja ya kuongea maana yalikuwa wazi. Je mnataka turudi huko?
Na nikuambie tu mkishiriki uchaguzi huu, dola itawabamiza hakuna na hakuna atakayewaonea huruma mkisiginwa na dola maana mnashiriki uchaguzi huku mkijua matokeo yake ni yepi. Sasa hiyo ni akili au matope? Unaenda kushiriki uchaguzi ambao unajua kushinda ni ndoto kutokana na mazingira mabovu.Kama unashiriki uchaguzi ilimradi ushiriki na sio kushinda kazi kwako bwana Gabriel Mwita.
Mwisho naomba nikushauri mambo matau yafuatayo Ndugu Gabriel Mwita:
1. Kama unataka kukijenga chama na kuwa kiongozi mkubwa wa chama huko mbeleni, Jenga tabia ya kuheshimu vikao vya chama. Vikao vyote halali vimekubali chama kisishiriki uchaguzi mkuu kama hakuna mabadiliko kwenye madhaifu yaliyopo kwenye sheria na mfumo wa uchaguzi Tanzania. Inakuaje leo unalazimisha chama kubadilisha mwelekeo ghafla baada ya Mkutano Mkuu kuridhia?. Huo ni utovu wa nidhamu na kiburi.
2. Kama unataka kugombea ubunge na unaona una ushawishi wa kushinda , tafuta chama kinachokubalika hata CCM , NCCR kagombee, maana kugombea ni haki yako siyo lazima iwe CHADEMA. Kuendelea kulazimisha unataka ugombeee kupitia CHADEMA huku ukijua kwa Sasa chama kinapambania mabadiliko kwenye mfumo wa uchaguzi inaonesha wewe una lako jambo kama sio kirusi ndani ya chama.
3. Kama unaona Chama kilifanya maamuzi yasiyo sahihi , nafasi uliyonayo ni kuomba mkutako mkuu wa dharura kupitia njia ya kikatiba ambapo Jambo lako litajadiliwa na likionekana ni la msingi chama kitabadilsha msimamo na kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Soma Pia: CHADEMA yamng'oa Katibu wa Sekretarieti wa chama, Julius Mwita baada ya kuibuka mzozano kwenye kundi sogozi
kwa kukuaga tu, nakushauri ya kwamba usiongee yote ukamaliza maana kwenye siasa hujui litatokea nini kesho. Leo waweza kuona sifa kwa kumshambulia Mh. Lissu ila kesho mamlaka yaweza kukubaliana na hoja za Lissu na kukaa meza moja kubadilisha mfumo wote wa uchaguzi, mtafanyaje?
Kesho nitajibu hoja zako zote ulizitoa kwenye press ya leo.
Asante