Fursa za biashara Zanzibar

Mi nadhani tatizo lipo kwenye kupata habari na uwoga wa ku take risk.Wengi hatupendi kuumiza kichwa katika kuwekeza that's way tunakuwa na excuse nyingi.John Rockefeller àliwahi Judea"I always try to change Avery disester into oppunities. Kitu ambacho hatuna uwezo huo
 
Mambo mengine au ukitaka kujua fursa za kibiashara Zenji muwe mnauliza wenyeji msiende kichwa ngumu na kufanya Survey zenu pekee na kujiridhisha tu, ohoo mtakuja kupoteza mitaji yenu na kujutia baadae
 
Kuna wakati nilikuwa z'bar nikaenda kwenye hoteli moja ya kitalii, nilikuta watu wakishusha mizigo kwenye gari moja kubwa hapo hotelini, moja ya mizigo hiyo ilikuwa ni mayai na vinywaji vikali (mvinyo).
Nilijaribu kumdadisi mhudumu mmoja pale akaniambia vitu vile vinatoka nje ya nchi, nikashangaa sana, yani hata mayai ya kisasa wanaagiza toka nje ya nchi?
Nilipodadisi zaidi niligundua 90% ya bidhaa zinazotumiwa pale hotelini zinatoka nje ya nchi, sio kwamba hapa tz hazipo hapana! ni kwasababu wabongo wengi ni 'wababaishaji' yan kama amepewa tenda ya mayai 1000 kila wiki, basi atapeleka kwa wiki mbili then wiki ya tatu atakuwa ameishiwa au ataanza kusuasua, hii ndio shida(commitment).
Ukweli ni kwamba kuna fursa za biashara ni nyingi kwenye mahoteli makubwa z'bar wanahitaji bidhaa nyingi mfano vinywaji, matunda,nyama,mayai,
mbogamboga tena kwa bei nzuri sana ila wanahitaji watu committed mf;kuna jamaa alikuwa anawauzia nyama ya
'mbuzi katoliki' sh 17,000@kg
Pia kipindi cha Ramadhan watu wanopeleka nyama ya Kuku,mbuzi ng'ombe wanapiga sana pesa(hii sio hotelini hata mtaani tu).
Tatizo watz tumelala
mpaka toothpick zinaingizwa kutoka nje, hii ni aibu!!
Magogo yanazalishwa Iringa mpaka yanasafirishwa nje tunashindwaje kutafuta/kuagiza mashine ya kutengeneza toothpick? tuamke tuchangamkie fursa wakuu.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
thanks ila tunasafari ndefu
 
Vipi kuhusu lile zuio la ku-export mazao nje si utahitaji vibali na mambo ya urasimu yanajaa.
 
Ni kweli kuna fursa lakini pia kuna ubabaishaji mkubwa sana wa kuingiza mzigo kutoka bara ...sio hizi za hotel hata biashara ya mbao ngumu inalipa sana Zanzibar.... Kuna mitumbwi inapitia Bandar ya mtwara na tanga ni karibu sana but mchakato wa vibali inabidi uwe mtu wa mtaji mkubwa embu fanya reserch na wewe kujua kwann watu hawachangamkii hiyo fursa...hakuna fursa mpya hapa tz kwa biashara za namna hiyo
 
Hata bangi inalimwa hapahapa halafu watu wengine wanaingiza kutoka nje. Tatizo commitment.
 
Tumejaa ulaghai, uongo, utapeli, maneno mengi yasiyo na maana, uzinguaji, no commitment, porojo, visingizio, karaha na kila hila. Hayo yote hayatakiwi kwenye biashara ya leo.
 
Hawataki fursa,

Wanataka kumjadili wema katengeneza sha au laa,

Wana-interviews zao kule na muosha rungu,

Mapenzi ndio mijadal yai( sio mbaya mapenzi yana run dunia),

Wameajiriwa yes hawataki kabisa kwenda nje ya box(in kingwangala articles),

Wanajadili makinikia kwanza mkuu jana si umesikia tumelipwa Au hujui

Mijadala ya kuhegedana ndo tunaipenda mkuu
Kuna tatizo pia kuhusu elimu ya jinsi ya kuanza biashara. Masoko ya mitaji, mifumo ya kodi, changamoto sokoni. Mfano: wanaotoa elimu kuhusu fursa za kilimo Hakuna anayezungumzia changamoto kubwa Kwa mkulima mwenye mtaji mdogo: source of sustainable labour(wafanyakazi WA uhakika) mifumo ya masoko yetu(changamoto za madalali na ushuru usioangalia Hali ya soko) na kadhalika. Hivyo basi na Huku watu waelimishwe. Watu wanaogopa changamoto za kuanguka kimitaji pia.
 
Thread ambayo haina kichwa cha habari chenye haya maneno huwezi kupata wachangiaji

-Mbowe kufanya press
-Magufuli atumbua
-Dawa ya kuongeza nguvu za kiume kwa bei chee
-Njia ya kuacha punyeto
-Makonda
-Ccm kuhonga madiwana wa Chadema
-Natafuta jimama
etc....

Yaani shida tupu.... Zanzibar wana uhitaji mkubwa sana wa Nyanya na wale wanao lima Mpunga kipindi cha sikuku na kipindi cha kawaida kuna uhitaji wa Mchele
Tatizo kodi..yaani jinsi ya kupitisha mzigo kuupeleka mpaka zanzbr...TRA
 
Back
Top Bottom