Fursa ya ujinga na matrix katika mfumo wa maisha ya kisasa

Fursa ya ujinga na matrix katika mfumo wa maisha ya kisasa

Bob Manson

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2021
Posts
4,543
Reaction score
8,754
Habarini waungwana,

Ni ukweli usio na shaka kwamba asilimia kubwa ya watu duniani wana ujinga, ndiyo, ni wajinga.

Ndoto zangu siku nitengeneze pesa kwa kutumia huu ujinga, au nitumie matrix kama fursa.

Wengi mnafahamu matrix ni nini, kwa ufupi ni mfumo ambao binadamu wanauishi katika maisha yao ya kila siku, yani gereza huru.

Addictions, uvivu, kupenda mteremko ni sifa kuu ya walimwengu wa sasa, pamoja na kupenda kutumia pesa kwenye mambo ya kufurahisha macho na masikio.

Sasa ndoto yangu ni kwamba, ipo siku nitatumia fursa hii kutengeneza pesa nyingi, na naamini nitafanikiwa kikubwa Mungu anipe Uzima.

Naona wengi wanatengeneza pesa kwa kutumia ujinga wa watu, na mimi sitakubali fursa hii iniptie, pia kila siku wajinga wanaongezeka na hawatoisha kamwe.

Hili ni wazo tu nililo nalo, bado natafakari ni idara gani au njia gani nipite ili kuwanasa wajinga, na hii ndio ndoto yangu, hatakama sio leo wala kesho, lakini ipo siku itatimia.

NOTE: sitofanya utapeli, sitaonea au kudhulumu mtu, sitaiba au kurubuni watu, bali nitabuni njia ambayo najua wajinga wengi watanipa hela, hata kama ni kidogo kidogo lakini zitajaa.

Ujinga ni mtaji, ujinga ni pesa.
 
Hatuishi kwenye jela, tunaishi kwenye paradiso.

Dunia haijawahi kuwa sehemu salama kuishi kuliko hivi leo.

Kipindi cha nyuma ambapo hakukuwa na mifumo rasmi kama mahakama, uchumi watu waliishi vibaya sana.
Wachache walishika mamlaka na waliyatumia vibaya. Vita kila mahali. Haki za binadamu hazikuthaminiwa.

Isitoshe hakukuwa na teknolojia kama hivi sasa, afya, usalama vilikuwa kidogo.

Leo tunapata mahitaji kupitiliza mpaka tunakuwa waraibu na wavivu. Maendeleo yamekuja na changamoto zake.

Kuzitatua hizi changamoto ndo kutaleta tija zaidi, tusichukie huu mfumo wa maisha, soma historia zamani watu waliishi kama wannyama.
 
Ukiamini hivyo, tayari wewe ni mhanga namba moja wa gereza la Matrix
hii mifumo ya kijamii kiuchumi imewekwa kurahisisha maisha mkuu, dunia sio salama ikikosekana

uvivu, uraibu ni mambo binafsi tu unaweka jitihada kuyapunguza
 
Hakuna mfumo uliowekwa kurahisisha maisha, kila kitu kimekuwa more complex, wanapata utajiri kwa ubize na mihangaiko yetu.
sasa hapo unaongelea wealth inequqlity, mambo ya kisiasa zaidi

lakini mimi naheshimu sana mifumo kama shule, mahakama, bima nk, inahitaji maboresho tu
 
Back
Top Bottom