Ukiwa mfanya biashara kama huwezi kukabiliana na vitu kama hivyo kwa busara basi utagombana na watu kila siku na wateja watakuona kama unataka kuwalalia! Mwenzako anajua biashara na ndiyo maana ametoa sababu ya bei yake kuwa kubwa... ie quality. Angeamua kukasirika kama wewe na kumwita tu mchawi na mshirikina potential customers wangeona kama alitaka ''kuwapiga'' ndiyo maana baada ya kuumbuliwa akakasirika na kutukana. Njia yako ya ku-handle tatizo bado inatumiwa sana na wafanyabiashara wengi wa Bongo wasijue kuwa wanajiangusha wenyewe.
Narudia tena;
Mteja kuhoji si dhambi.
Ila namna Mtu anavyohoji inakupa picha ni Mteja au Mfanya vurugu.
Hapa JF usipojua namna ya ku-deal na watu hawa utapata sonona.
Ieleweke sikusema muuzaji asihojiwe,
Ila hili la kuparamia Uzi wawatu na kuweka hadi Bei nyingine.
Eti,'Sehemu fulani utapata kwa Bei fulani' -Nini hii?
Unania kweli mwenzako afanye Biashara?
After all, BIASHARA si-ni huria?
Shida yako wewe nini?
Au tuseme wewe Mzuri sana kwa mnunuzi na unawapenda,
Kwanini usifungue Uzi wako uweke hizo Bei zako?
Muungwana hawezi kufanya 'ujinga' huu.
Umegusia swala la Ujuvi wa ufahamu wa Biashara:
Hewala, Nami nikiri kuwa ni maamuma,
Ila nisaidie kidogo,
Unadhani kwanini masharti ya kumiliki Majokofu ya kuhifadhia Vinywaji baridi vya Makampuni kama Coca na Pepsi hairuhusiwi kuhifadhi kinywaji tofauti kwenye jokofu lisiloendana na kinywaji husika?
Jua tu kuwa haukuwa uamuzi wa bahati mbaya huo?
Rahisi tu,
Unaweza kumbadilisha uamuzi Mteja kwa kitu kidogo sana.
Na kwa mambo ya kijinga kama yanayofanywa na baadhi ya watu wa JF Utadhani wametumwa.
NASEMAJE;
Uchawi ni hadhi ya staha zaidi kuwaita baadhi ya watu.