Fursa kwa vijana njenje EAPOC

Fursa kwa vijana njenje EAPOC

semtawa

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2012
Posts
1,267
Reaction score
1,258
Rais Dk. Samia afungua
fursa kwa vijana EACOP

Na Mwandishi Wetu, Geita
Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan imezidi kuwajali vijana, baada ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko kuzindua Mpango wa Uwezeshaji wa Kiuchumi kwa Vijana (YEE), ambao unagusa maeneo yanayopitiwa na mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP).

Uzinduzi huo ni jitihada zinazoendelea kufanywa na Serikali katika kuhakikisha kuwa jamii zilizo karibu na miradi zinanufaika na miradi hiyo.

Akizindua mradi huo katika Kijiji cha Bukombe, wilayani Bukombe, Mkoa wa Geita leo, Dk. Biteko alisema mradi huo wa Uwezeshaji Vijana Kiuchumi ni moja ya miradi iliyopangwa kuwezeshwa na Kampuni ya EACOP, kwa kipindi cha ujenzi na baada ya ujenzi ikiwa ni sehemu ya Uwajibikaji wa Kampuni hiyo kwa jamii.

Alisema mradi huo umepangwa kuwafikia zaidi ya vijana 12,261 ambao miongoni mwao wanawake ni 6,130; wanaume 4,905 na makundi maalumu 1,226, katika awamu ya kwanza inayohusisha Mikoa ya Geita, Kagera, Tabora na Tanga.

"Tunapozindua mradi huu hatuna budi kuwashukuru Mheshimiwa Dk. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museveni, Rais wa Jamhuri ya Uganda.

Viongozi wetu hawa kwa nia yao ya dhati na moyo wa uzalendo wameuendeleza na kuusimamia kikamilifu mradi huu wa EACOP ambao umefikia asilimia 65, tumefikia hapa sababu ya msukumo wao wa kutekeleza mradi huu, "alisema Dk. Biteko.

WATANZANIA
WALIO NUFAIKA
Alifafanua, kuwa tangu kuanza kwa mradi wa EACOP mwaka 2022 hadi hivi sasa, jumla ya Watanzania 9,194 wamepata nafasi za kufanya kazi ndani ya mradi na hivyo kuwa fursa kwao ya kujipatia kipato, mwaka 2024 kampuni ilitoa mafunzo maalumu kwa vijana 170 na kuwapatia kazi kwenye mradi, vijana wengine 110 wapo katika masomo na wanatarajiwa kujumlishwa pia katika mradi huo.



-Ends
 

Attachments

  • IMG-20250818-WA1327-935x1536.jpg
    IMG-20250818-WA1327-935x1536.jpg
    340.6 KB · Views: 17
  • WhatsApp Image 2025-08-18 at 12.52.53 PM (1).jpeg
    WhatsApp Image 2025-08-18 at 12.52.53 PM (1).jpeg
    152.9 KB · Views: 20
  • IMG-20250818-WA1377.jpg
    IMG-20250818-WA1377.jpg
    140.2 KB · Views: 18
  • WhatsApp Image 2025-08-18 at 1.52.14 PM.jpeg
    WhatsApp Image 2025-08-18 at 1.52.14 PM.jpeg
    110.5 KB · Views: 15
  • 1002087821.jpg
    1002087821.jpg
    137.8 KB · Views: 19
Rais Dk. Samia kafungua fursa, tupunguze drama za siasa nchini
#Updates
Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan imezidi kuwajali vijana, baada ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko kuzindua Mpango wa Uwezeshaji wa Kiuchumi kwa Vijana (YEE), ambao unagusa maeneo yanayopitiwa na mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP).

Uzinduzi huo ni jitihada zinazoendelea kufanywa na Serikali katika kuhakikisha kuwa jamii zilizo karibu na miradi zinanufaika na miradi hiyo.

Akizindua mradi huo katika Kijiji cha Bukombe, wilayani Bukombe, Mkoa wa Geita leo, Dk. Biteko alisema mradi huo wa Uwezeshaji Vijana Kiuchumi ni moja ya miradi iliyopangwa kuwezeshwa na Kampuni ya EACOP, kwa kipindi cha ujenzi na baada ya ujenzi ikiwa ni sehemu ya Uwajibikaji wa Kampuni hiyo kwa jamii.

Alisema mradi huo umepangwa kuwafikia zaidi ya vijana 12,261 ambao miongoni mwao wanawake ni 6,130; wanaume 4,905 na makundi maalumu 1,226, katika awamu ya kwanza inayohusisha Mikoa ya Geita, Kagera, Tabora na Tanga.

"Tunapozindua mradi huu hatuna budi kuwashukuru Mheshimiwa Dk. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museveni, Rais wa Jamhuri ya Uganda.

Viongozi wetu hawa kwa nia yao ya dhati na moyo wa uzalendo wameuendeleza na kuusimamia kikamilifu mradi huu wa EACOP ambao umefikia asilimia 65, tumefikia hapa sababu ya msukumo wao wa kutekeleza mradi huu, "alisema Dk. Biteko.

WATANZANIA
WALIO NUFAIKA
Alifafanua, kuwa tangu kuanza kwa mradi wa EACOP mwaka 2022 hadi hivi sasa, jumla ya Watanzania 9,194 wamepata nafasi za kufanya kazi ndani ya mradi na hivyo kuwa fursa kwao ya kujipatia kipato, mwaka 2024 kampuni ilitoa mafunzo maalumu kwa vijana 170 na kuwapatia kazi kwenye mradi, vijana wengine 110 wapo katika masomo na wanatarajiwa kujumlishwa pia katika mradi huo.



-Ends
Wenzetu Uganda wanahamasisha vijana kuchangamkia fursa za bomba la mafuta ghafi. Je, sisi vyombo vyetu vya habari, wanasiasa na wanaharakati wanawajibika vya kutosha kuwajenga vijana wetu kuchangamkia fursa hii?

Ukisoma historia ya maendeleo duniani, miradi mikubwa kama huu wa bomba la mafuta kutoka Hoima, Uganda hadi Chongoleani, Tanga; ina mchango mkubwa wa kuleta mapinduzi ya maendeleo kwa nchi husika.

1. Kuonyesha nchi zinakopita mradi zina salama wa hali ya juu kwa uwekezaji wa miradi mikubwa, ikiwemo ya moja kwa moja kutoka nje (FDIs) au hata ya kuvuka mipaka.

2. Ajira kwa vijana ( kama Tanzania ilivyoanza).

3. Mapato.

4. Kuchechemua biashara na uchumi wa maeneo mradi unakopita.

5. Kuweka rekodi ya nchi, kama bomba la gesi la Nord stream kutoka Russia kwenda Europe. Hivyo, tupunguze kelele za siasa, ajenda nyepesi mahakamani, slfie nk
Tuwaelekeze vijana wachangamkie fursa.
 
Back
Top Bottom