Fundisho kwa mnaopenda kuchati chati hovyo

Fundisho kwa mnaopenda kuchati chati hovyo

Kuna jamaa walifanyaga tukio kama hilo wakiwa na pikipiki maeneo ya savei hapo darajani kabla hujafika Chuo kikuu cha Ardhi,wamekwapua kwa mama mmoja na kukimbia lkn hawakufika mbali baada ya kuitiwa mwizi.Jamaa walikimbia kupitia njia za uchochoroni,dereva aliamua kuacha usukani na kukimbia akimwacha yule aliyeiba akijaribu kukimbia bila mafanikio na kutiwa mikononi mwa wananchi wenye hasira kali na kumtia moto.
In fact haya matukio ya kuiba na kukimbia na pikipiki yamekuwa mengi sana maeneo ya Savei hasa nyakati za usiku.
 
Hiyo ndiyo dar. Huku kwetu haufiki mbali, ushakuwa majivu.
Watu wa mikoani huwa hatulei upumbafu. Huku kwetu iba hata karanga tu za 100 utachezea kichapo cha kufa binadamu
Wewe kweli wa mkoani. Hao wezi wako kwenye bodaboda wanakuvizia kwenye foleni unafikiri utawapata vipi?
 
Hapo mataa ya keko/Karume hovyoo Sana,ukiona Bodaboda pembeni ujue wanasubiri watu wawapige,magari yakisimama tu yakisubiri Taa,vijana wanapita pembeni ya magari Ili kuwaibia watu,na akikwapua fasta anadandia bora wanakimbia..
 
Hiyo ndiyo dar. Huku kwetu haufiki mbali, ushakuwa majivu.
Watu wa mikoani huwa hatulei upumbafu. Huku kwetu iba hata karanga tu za 100 utachezea kichapo cha kufa binadamu
Acha hizo na wewe , huko kwenu yatatokeaje, wakati magari yenyewe hayazidi kumi, mpaka yaweke foleni mkwapuliwe, huko foleni yenu ni ya mashine ya kusaga makopa ya mihogo tu. Mmezidi kuwaonea donge watu wa bandar salam.
 
Acha hizo na wewe , huko kwenu yatatokeaje, wakati magari yenyewe hayazidi kumi, mpaka yaweke foleni mkwapuliwe, huko foleni yenu ni ya mashine ya kusaga makopa ya mihogo tu. Mmezidi kuwaonea donge watu wa bandar salam.
Tunawaonea donge? Mwizi anaiba unamwangalia? Hiyo ndiyo dar
Njoo uibe huku kwetu uone.
 
Wewe kweli wa mkoani. Hao wezi wako kwenye bodaboda wanakuvizia kwenye foleni unafikiri utawapata vipi?
Huu ujinga haupo huku kwetu. Tunachoma mpaka pikipiki. Njoo ujaribu.
Yaani mwizi anashuka kwenye pikipiki, mwenzake anamsubiria kwenye pikipiki, anaenda anakwapua simu, anarudi, anapanda. Wanaondoka.
Wananchi wanaangalia tu. Hiyo ndiyo dar. Njoo huku kwetu mwanza ujionee.
Wakina scorpion, rambo, vikundi vya ajabu ajabu. Havipo huku
 
Wamikoani mnavyojipaisha utafikiri wa huku dar wote ni wazaramo kumbe sisi pia tumetoka huko huko mikoani
Wamefuata tabia zenu. Siku zote mtu akikaa na mvuta shisha lazima naye aanze kuvuta shisha
 
Mfiwa hana pa kulala popote analala.

Mtoa post ametoa angalizo. Na mimi natoa yangu...................,
Wanaochat wasifunge vioo mnatia joto kwenye daladala.
 
kwasababu uko Lisbon. njoo keko ukione cha moto!! wa ureno😉
Tena keko ndio balaa mida yajioni nilishuhudia katika dala dala jamaa aliekaa siti yambele yangu simu ikichukuliwa kiulain tena jamaa hakua naboda boda wala nini
 
Kama nusu saa zilizopita nilikuwa kwenye basi la Goms-Masaki nikirudi zangu kitaa.

Tukiwa kwenye foleni maeneo ya ngozi ,pale kwenye makutano ya keko,karume na ngozi.kiukweli palikuwepo na foleni cha kizushi.

Mimi nikiwa siti ya mbele kabisa karibu na dereva nikishuhudia tukio la mzembe akilizwa na mjanja A-z.

mara kidogo bodaboda iliyokuwa na watu 2. Dereva na mwenzake nyuma walipita katikati ya lanes 2,sasa gari Fulani hv ukilitizama linavutia sana jamaa wa lile gari alikuwa peruzi simu yake akivutia foleni itembee tembee sijui masikini ya mungu alikuwa anachati whatsap,ana peruzi JF,fb au instagram

Mara paap yule jamaa aliyepakizwa nyuma kwenye bodaboda akashuka na kwenda kuchukua simu ya yule jamaa kiulaini bila bughudha yeyote kama vile chatu akimla mbuzi

Baada ya tukio jamaa akatembea hatua 3 na kupanda bodaboda hao wakatembea na kutokomea pasikojulikana

Jamaa kustuka anafungua mlango na kushuka ikawa too late kwa kihindi tunasema marighaya ,ikabidi ashike kichwa na kuwatizama tu kama vile mfiwa akisindikiza jeneza,jamaa kwa unyonge akaingia kwenye gari lake akisubiri foleni itembee arudi zake kwake.

Fundisho

1.kwann uchati ilhali dirisha umeacha wazi tena huna wasiwasi wowote
Kila anayetumia simu akiwa ndani ya gari anachati? Fikiria nje ya box
 
Huyo nae joto lote la Dar kwanini kioo kiwe chini,ubahili wa mafuta na IOS imeenda na waporaji
 
Tena keko ndio balaa mida yajioni nilishuhudia katika dala dala jamaa aliekaa siti yambele yangu simu ikichukuliwa kiulain tena jamaa hakua naboda boda wala nini
mleta mada karipoti tukio jingine. actually haipiti siku!
 
Wewe kweli wa mkoani. Hao wezi wako kwenye bodaboda wanakuvizia kwenye foleni unafikiri utawapata vipi?
Unabishana na mtu ambaye kwao hakuna hata traffic light. Hajawahi kuona foleni akiwa shuhuda zaid ya taarifa za habar
 
Mwengine nyakati za jion hujifanya kam anapanda daladala hasa walio jirani ya sit za mlangoni, tabia hiyo ipo pale mission mbagara
 
Back
Top Bottom