Fundi Ujenzi anahitajika

Fundi Ujenzi anahitajika

Bado naona watu wanatoa namba za simu tu badala ya kutoa taarifa ambazo zitanipa uelekeo wa kunishawishi niwape kazi au la.Nafikiri hii pia ni moja ya shida zinazofanya watanzania tushindwe kuwa na ushindani kimataifa.Kwa jinsi nilivytoa taarifa na maelezo hapo juu ina maana tayari kama mtu ni fundi mzoefu ana uwezo wa kuchukua hizo taarifa kuzifanyia kazi na kisha anitafute ama kwa email au pm kisha anieleze kidogo kuhusu kazi yake uzoefu wake na gharama zake ili nifanye mchakato.Naona wengi huku wamezoea ama kupewa kazi kwa kujuana au kuonewa huruma au kupendelewa na sio kwa kuwa competitive.Ila naendelea kusubiri labda atatokea mwenye uelewa achangamkia hii kazi.
Tatizo we ushaweka limitation kwamba fundi lazima atoke Arusha.......
 
Nyumba ya vyumba 7,sitting room, toilets be gani finishing..
Vyumba ni 2.5x2.5 mita kasoro viwili, kuna 3.5 x2.5 na 3.5x7.5 mita, sebule 4.5x10 meter toilet na bafu ni 3.5x2.5 mita pia kuna kolido mbili moja ina upana na urefu wa 1x14mita na nyingine 1x8mita veranda ni 3.5x3.5.
Makadirio ya chini kabisa kwa nyumba ya kisasa
Finishing ya nyumba inategemea na wewe client unataka ufanye umaliziaji wa materials gani......
 
Tatizo we ushaweka limitation kwamba fundi lazima atoke Arusha.......
Sio tatizo ninataka fundi ambaye ana uzoefu wa kufanya kazi kule Arusha.Kuna Project zingine zitafanyika Dar ila mpaka mwezi wa Tano au wa Sita kwa wale wa Dar nitwatafuta

Karibu
 
Nimependa mpango kazi jinsi ulivyo inaonekana kazi za ujenzi unazielewa, lakini doubt yangu iko kwenye uimara wa nyumba itakayojengwa kwa sababu ya muda uliotolewa kukamilisha kazi, japokuwa sijui RATIO ya zege kwenye beam na mortar/udongo wa kujengea (Mchanganyo) ni daraja la ngapi, ukizingatia muda wa umwagiliaji kitaalamu, otherwise Nakutakia kazi njema. NB ukihitaji msimamizi wa kazi usisite kunijulisha mkuu.
 
Mimi ni mtaalamu wa ujenzi, sihitaji hio kazi lakini naweza kukupa ushauri bure wa kitaalamu.
Toa ushauri hata kwa manufaa ya sisi wengine mkuu, njoo pm unisaidie mawazo
 
Nyumba ya vyumba 7,sitting room, toilets be gani finishing..
Vyumba ni 2.5x2.5 mita kasoro viwili, kuna 3.5 x2.5 na 3.5x7.5 mita, sebule 4.5x10 meter toilet na bafu ni 3.5x2.5 mita pia kuna kolido mbili moja ina upana na urefu wa 1x14mita na nyingine 1x8mita veranda ni 3.5x3.5.
Makadirio ya chini kabisa kwa nyumba ya kisasa
Sebule mita 10!!! aysee fanya uwaone Forbes waiweke nyumba yako kwenye record za dunia
 
Ni kweli mkuu tena hapo ni juu tu bado underground size ya kiwanja hicho hicho ila ramani yake ni siri sijataja.
Sebule mita 10!!! aysee fanya uwaone Forbes waiweke nyumba yako kwenye record za dunia
 
Ni kweli mkuu tena hapo ni juu tu bado underground size ya kiwanja hicho hicho ila ramani yake ni siri sijataja.
kwa Mara ya kwanza ndo nasikia kwako, au unataka uwe unawalaza wageni sebuleni?
 
Hahahaha mkuu ni ya kawaida sema imekaa kimstatili mno.

Sebule kubwa inapendeza hatakama mnajadiliana mnakaa mbalimbali ukitokea ugomvi hadi aje urushe ngumi utakuwa umejipanga....

Ilafu inakupa uhuru hata msiba ukitokea hakuna haja ya kutoa thamani njee
Sawa mkuu ila naamini kuwa unaijua vyema hiyo mita 10 inafananaje kiurefu
 
Hahahaha mkuu ni ya kawaida sema imekaa kimstatili mno.

Sebule kubwa inapendeza hatakama mnajadiliana mnakaa mbalimbali ukitokea ugomvi hadi aje urushe ngumi utakuwa umejipanga....

Ilafu inakupa uhuru hata msiba ukitokea hakuna haja ya kutoa thamani njee
kumbe umejipanga kwa mikutano!! Bila shaka ktk ukoo wenu nyumba yako ndo watakua wanakuja kufanyia vikao mbali mbali (harusi, misiba n.k) hamna haja tena ya kutafuta ukumbi wa kukodi koh koh
 
Hahahaha mkuu sio kwa ajili ya ukoo.
Dharura tu si unajua binadamu mkuu.

ingekuwa wewe ni size ipi inatosha.
kumbe umejipanga kwa mikutano!! Bila shaka ktk ukoo wenu nyumba yako ndo watakua wanakuja kufanyia vikao mbali mbali (harusi, misiba n.k) hamna haja tena ya kutafuta ukumbi wa kukodi koh koh
 
Back
Top Bottom