Fumbo pasua kichwa 5: Inspekta Kamazima alijuaje kwamba Katibu Muhtasi ndiye muuaji?

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
upload_2016-10-13_8-33-34.png


Ilikuwa majira ya saa 11:15 jioni Inspekta wa polisi afande Kamazima alikuwa ndiyo amefika kwenye eneo la tukio. Ilikuwa ni maeneo ya Posta katika jengo la Bujibuji Plaza. Hapo ndipo zilipokuwa ofisi za kampuni ya Bima iliyokuwa ikimilikiwa na Bwana Mlaponi. Aliitwa baada ya kutokea mauaji ya Bwana Mlaponi, Mkurugenzi na mmiliki wa kampuni hiyo ya Mlaponi Insurance Agency

Hapo ofisini alikuwepo Katibu Muhtasi wa Bwana Mlaponi aitwaye Nshemele, ambaye alizungumziwa na watu wa ofisi za jirani waliohojiwa awali kama Katibu Muhtasi muadilifu wa Bwana Mlaponi.

Kwa mujibu wa maelezo ya Nshemele alidai kwamba alitoka saa 9:45 jioni na kuwaacha bosi wake na mgeni wake aliyemtaja kwa jina la Makanyaga wakizungumza na yeye alitoka kwa ajili ya kwenda kufanya manunuzi ya vifaa vya ofisini katika duka la Msemo Printers ambapo alikuwa na risiti zinazoonyesha kwamba alifanya manunuzi hayo majira ya saa 10:15 jioni.

Kwa mujibu wa maelezo yake Nshemele alidai kwamba, aliporudi majira ya 10:30 ndipo alipokuta Bosi wake ameuawa kwa kuchomwa kisu mgongoni.

Muda alioutaja kwamba ndiyo aliyorudi kutoka Msemo Printers unaonyesha kwamba alikuwa nje ya ofisi kwa takriban muda wa dakika 45 ambazo zinatosha kutumika kwa mtu kwenda Msemo Printers na kurudi kutokana na umbali ilipo ofisi za Mlaponi Insurance Agency na ilipo Msemo Printers.

Pale mezani kulikutwa gloves, matone ya kahawa, na pia meza hiyo ilikuwa imevurugika huku baadhi ya mafaili yakiwa chini na hata baadhi ya mafaili mengine yaliyokuwa kwenye kabati nyuma ya kiti cha mkurugenzi huyo yakiwa yameanguka chini kuashiria kwamba kulikuwa na mapigano kati ya muuaji na mkurugenzi huyo na pia shubaka kubwa la kuhifadhia fedha lilikuwa wazi na ndani hapakuwa na fedha na pia funguo za shubaka hilo hazikujulikana zilipo.

Mkononi mwa mkurungenzi huyo alikuwa amevaa saa ambayo nayo pia ilikuwa imevunjika na ilikuwa imesimama kufanya kazi ikiwa imesimama katika muda wa saa 9:55.

Nshemele alipoulizwa kama bosi wake huwa ana kawaida ya kunywa kahawa, akasema hapana bali mgeni aliyemuacha na bosi wake yaani Bwana Makanyaga ndiye aliyekuja na kahawa ikiwa katika kikombe cha Karatasi ngumu cha take away na wakati wanazungumza Bwana Makanyaga alimaliza kunywa Kahawa yake na kukiweka kikombe chake juu ya meza yake (yeye Nshemele) ambapo alikitupa kwenye dust bin yake.

Askari wa upelelezi alipochunguza ndani ya ile dust bin aliona kikombe kile cha kahawa na kikachukuliwa kwa ajili ya kuchunguzwa alama za vidole.

Kwenye daftari la wageni kumbukumbu inaonyesha wageni watatu wa mwisho waliorekodiwa walikuwa ni Kiranga (8:35), Mkumbange (9:10) Makanyaga (9:40).

Kisu alichochomwa nacho Bwana Mlaponi hakikukutwa na alama za vidole, kikombe cha kahawa kilichokutwa kwenye dust bin kilikutwa na alama za vidole vya Makanyaga na shubaka la kuhifadhia fedha lilikutwa na alama za vidole za Bwana Mlaponi.

Baada ya kuchunguza eneo la tukio kwa makini Ispekta Kamazima alibaini muuaji aliyehusika na mauaji ya Bwana Mlaponi si mwingine ni Katibu Muhtasi wake Nshemele ambapo aliamuru akamatwe na kuhojiwa zaidi kwa kuhusika na mauaji ya Bosi wake.

Baada ya kuhojiwa kwa umakini mkubwa kwa kuangalia mazingira ya tukio zima hatimaye Nshemele alikiri kuhusika na mauaji ya Bosi wake.

Je ni kitu gani kilimfanya Inspekta Kamazima amjue muuaji kirahisi vile?


Hint: Ipo sababu moja ya msingi ambayo inaunganisha dot na ndiyo iliyopelekea kukamatwa kwake.


Sitaki majibu ya jumla jumla.
 
Ila hiyo ya Bwana Kizito nilikuwa nimeshau kabisa ndo maana hukuniona hapo...hahahah!!!!
 
View attachment 417152

Ilikuwa majira ya saa 11:15 jioni Inspekta wa polisi afande Kamazima alikuwa ndiyo amefika kwenye eneo la tukio. Ilikuwa ni maeneo ya Posta katika jengo la Bujibuji Plaza. Hapo ndipo zilipokuwa ofisi za kampuni ya Bima iliyokuwa ikimilikiwa na Bwana Mlaponi. Aliitwa baada ya kutokea mauaji ya Bwana Mlaponi, Mkurugenzi na mmiliki wa kampuni hiyo ya Mlaponi Insurance Agency

Ha! Kumbe Bujibuji ana mjengo City Centre! Safi sana.
 
Kitu hicho ni matone ya kahawa maana kwa mujibu wa huyo katibu muhtasi huyo mgeni alimaliza kunywa kahawa na akaweka kikombe juu ya meza yake wakati huo huo akiwa na mazungumzo na bosi hapa panaleta utata
 
Mazingira ya muda ndiyo yalimfanya Inspekta Kamazima kuugundua ukweli, Nshemele anasema alirudi Ofisini sana 10:30 na kukuta bosi wake kafariki, lakini saa ya bosi insaonyesha iliacha kufanya kazi saa 10:55 na ilikuwa imeharibika kutokana na purukusha zilizotokea pale Ofisini.

Hii inaonyesha kuwa kabla ya hizi purukushani na bosi kuuawa tayari Nshemele alikuwa amerejea pale Ofisini.
 
Alitumia gloves kukitupa kikombe,kwaiyo inaonekana kikombe alikitupa baada ya tukio hivo kufanya fingerprints zionekane za makanyaga na sio zake..kama ingekua kweli maneno take basis fingerprint zingekua zake
 
jibu ni hivi Nshemele alitupa kikombe cha kahawa kwenye dustbin na fingerprints zake hazikuoneka na muuaji aliyemchoma kisu mkurugenzi pia fingerprints hazikuonekana sooooooo ....hahaahaaaa
 
muuaji alijisahau akatupa kikombe bila kuvua gloves alizotumia kufanyia mauaji
 
Mazingira ya muda ndiyo yalimfanya Inspekta Kamazima kuugundua ukweli, Nshemele anasema alirudi Ofisini sana 10:30 na kukuta bosi wake kafariki, lakini saa ya bosi insaonyesha iliacha kufanya kazi saa 10:55 na ilikuwa imeharibika kutokana na purukusha zilizotokea pale Ofisini.

Hii inaonyesha kuwa kabla ya hizi purukushani na bosi kuuawa tayari Nshemele alikuwa amerejea pale Ofisini.
Umenifanya nirudie kusoma malezo yangu mkuu
saa ilisimama kufanya kazi saa 9:55 jioni na Nshemele alirudi ofisini saa 10:30 jioni kuna tofauti ya dakika 35 tangu BHosi wake kuuawa na yeye kurudi ofisini
 
Mazingira ya muda ndiyo yalimfanya Inspekta Kamazima kuugundua ukweli, Nshemele anasema alirudi Ofisini sana 10:30 na kukuta bosi wake kafariki, lakini saa ya bosi insaonyesha iliacha kufanya kazi saa 10:55 na ilikuwa imeharibika kutokana na purukusha zilizotokea pale Ofisini.

Hii inaonyesha kuwa kabla ya hizi purukushani na bosi kuuawa tayari Nshemele alikuwa amerejea pale Ofisini.
Hili ndio jibu ila hukumalizia.kuwa na alipotupa kikombe alivua glofsi na kufungua sanduku la pesa. Hizo ndio alama mbili zilizomjulisha inspekta kuwa nshemele ndio muuwaji.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom