Hukumuzuku
JF-Expert Member
- Aug 29, 2008
- 6,666
- 4,999
It really beats me...sijui kwa nini hawakutumia juzuu ya "takbiru alaa walibalu" misikitini badala ya kufanya fujo na mauaji ya kutisha dhidi ya "makafiri" ....
Salaam toka mlimani .
Nimekuwa msomaji wa muda mrefu sana haa .JF ni hodari sana kw aissues za Kitaaifa na Kitaifa na vijimatukio.Ila nimeona jambo hili la Nigeria watu kuuana hapa halijaguswa kabisa .Kiini wanasema western values kuwa introduced eneo lile kama education system nk .
Nina maswali haya
1.Eneo lile nao walianza na madai ya haki za waislam ndipo wakaamua kusema litawaliwe na sharia ?
2.Je walikisha kuwa na sharia ina maana wale wasio waislma walipaswa kuondoka ama walitakiwa kuishi kufuata sharia ?
Una matatizo gani wewe hata unalifahamu neno "sharia" katika negative badala ya positive inayokusudiwa? Au ndio kwasababu inatokana na uislamu? Unafahamu nini maana ya "Western democrasy" au British common law? Mbona watu hawahami miji na kuhamia vichakani? Wanaishije miongoni mwetu watu wasioamini mifumo hiyo? Sio kuheshimu tu utawala as long as kama unatawala kihaki na usawa?
3.Wakisha weka sharia ina maana Serikali sasa inakuwa imetupwa mambo yanakuwa kama porini tu kwa wanyama wakubwa na wadogo ama kule kwa Talebani ?
Hichi tena kichekesho!!! Unafikiria nini kichwani kwako wewe? Nani kakushibisha kasumba namna hii? Unafikiri kama ingekuwa hivyo hata hao waislamu wangeiamini, kuitekeleza na kuitetea?. Kwa kifupi tu serikali inakuwepo, mahakama zinakuwepo na sheria zinazotawala ni zitokanazo na Qu-ani na Sunna za Mtume Muhammad na zinawalinda watu wote kwa haki na usawa kuliko hizi sheria tulizonazo based on British common Law au secularism ambazo zinayaacha masuala ya morality uchi. "Sharia" zitokanazo na Qur-ani na Sunna zinatokana na kwa Mwenyezi Mungu (SW). Mweneyezi Mungu wa Adam, Ibrahiim, Nuhu, Daudi, Mussa, Jesus na wa mwisho katika watakatifu hao ndio Muhammad ambae ndiye aliyetumwa na Qur-ani na Sunna zake. Wewe kama John, Patrick, Abdalla, Mahendra, Said bin Said na unaishi chini ya Sharia, basi utalindwa kama kawaida na mali zako na sehemu zako za ibada wakati upo katika nchi, Lakini bila shaka wewe, Abdalla, Hassani, Mahendra,Said bin Barhashi, Mike Jones nk nk, usifanye vitendo vichafu, morality wa binadamu katika sharia za kiislamu haukuachwa uchi kama katika sheria nyenginezo zisizokuwa za kiislamu, umelindwa na umelindika, na hili hasa ndio hao mafisadi katika ardhi ndio wanalouchukia uislamu kutokana nalo. Soma zaidi ndugu yangu usibabaishwe na kasumba tu. Hebu muulize Robin Williams ukimpatia nafasi, uko wapi ndugu
Ni haya tu kama kuna wachambuzi zaidi wanipe mwangaza nione mbele .Asanteni
It really beats me...sijui kwa nini hawakutumia juzuu ya "takbiru alaa walibalu" misikitini badala ya kufanya fujo na mauaji ya kutisha dhidi ya "makafiri" ....
WARNING: The following image is disturbing.
mwili wa Shehe muhamed yusufu ukiwa umetobolewa tobolewa na risasi......nawashukuru jeshi la Nigeria kwa kazi nzuri
Hivi rais wa Nigeria ni wa dini gani ?
Dini ya Rais haihusiani na hii kadhia. Chanzo cha tatizo ni hizi CULTS zinzojisingizia dini.
Mkuu,
i was just asking for cross reference purposes. Hawa jamaa wa hizi cults
nadhani pia wanamatatizo ya kisaikolojia kisha wanasingizia dini.
Dini yeyote inayohubiri chuki na utenganishi hiyo ni cult tu hata ijisingizie vipi hiyo ni cult.
Ok, rais wa Nigeria ni Ustadh al Hadj Umaru Yar'Adua, nadhani ni mdogo mtu wa Musa Yar'Adua aliyeuawa na fisadi dikteta nduli Sani Abacha. Ni muislamu kutoka kaskazini hukohuko mwa Nigeria. Ni msomi kama mdau mmoja alivyotanabahisha hapo awali kuwa ni mwalimu wa Chuo Kikuu ktk medani za Kemia.