Michael Amon
JF-Expert Member
- Dec 22, 2008
- 8,775
- 3,610
Jinsi ya kutengeneza fruit salad ya nanasi, machungwa na maembe
Mahitaji
Jinsi ya kutengeneza
Mahitaji
- 4 vikombe vya mananasi yaliyomenywa na kukatwa vipande vidogo vidogo
- 2 machungwa yaliyomenywa na kukatwa vipande vidogo vidogo
- 2 maembe yaliyomenywa na kukatwa vipande vidogo vidogo
- 2 ndizi zilizomenywa na kukatwa vipande vidogo vidogo
- Vijiko 2 vya maji ya limao au ndimu
- Vijiko 2 vya sukari
Jinsi ya kutengeneza
- Chukua matunda yote yaliyomenywa na kukatwa katwa na uyachanganye katika bakuli.
- Weka maji ya limao au ndimu na sukari kisha endelea kuchanganya.
- Baada kuchanganya vizuri, ifunike na uiweke kwenye friji kwa muda wa saa moja.
- Baada ya hapo fruit salad yako itakuwa tayari kwa kuliwa.