Fruit Mix/Matunda Mix

AshaDii

Platinum Member
Apr 16, 2011
16,190
18,078
Fruit Mix/Matunda Mix

Hii ni aina ya uandaaji wa matunda ambayo hutengenezwa kwa kuchanganywa ukizingaitia aina ya matunda…. Waweza Manipulate vovote mradi ladha usiharibu – kutegemea na kuoana kwa matunda… Ni mara chache saana kupata haya matunda kwa pamoja lakini kuna kipindi hutokea… Take advantage…

Matunda husika…

  • Papai Moja kubwa
  • Embe Mbili kubwa
  • Tikiti Kubwa nusu yake
  • Nanasi Kubwa nusu yake
  • Tango moja kubwa
  • Chungwa 2/3
Unaosha vizuri haya matunda na lukewarm water, Kisha unamenya kila tunda (na kutoa peke kwa matunda yenye mbegu); na kuweka chombo chake huku ukikata saizi ndogo ndogo mithili ya chip ya viazi mviringo. Baada ya hapo chukua chombo kikubwa cha kutosha mchanganyiko woote wa matunda… Mimina matunda toka vile vyombo taofauti katika hicho chombo – kisha chukua chakuchanyia… (Mwiko unaopikiwa mboga haufai saana bora kijiko vikubwa kabisa vile vya mezani…)… Baaada ya kuchanganya gently chukua sukari kiasi weka kwenye kikombe kidogo cha chai ukamulie yale machungwa, koroga mpaka ilainike kisha mimina katika huo mchanganyiko… Hilo tango utakata slices ndongo mno – mana lengo moja wapo la muhimu ni harufu yake katika matunda kuliko hata ladha.yake…

Note;
Best eaten when chilled, na mara nyingi ni bora yakatengenezwa kwa ajili ya kuliwa siku hiio hio… Ukifuata vipimo hivo hapo juu inatosha kama 5 to 7 servings… na ni nzuri saana kuwapa wahusika saa moja kabla ya mlo au saa moja baada ya mlo.


Pamoja Saaana..
ADI

 

Similar Discussions

Back
Top Bottom