From Goatherd to Governor, Edwin Mtei's Autobiography

Huyu mzee hakuwa gavana kwa merit bali alibebwa na nyerere ndio maana uchumi ukafa.kwenye hicho kitabu kaeleza alivymzuia zitto kabwe ili mwanawe awe mwenyekiti?

Ni kitabu cha kikabila zaidi kuliko utanzania.ndio maana mengi amepewa nafasi kubwa.huyu mzee anatapata tu

- Mkulu Kanda bwana, heshima mbele sana sometimes huwa unanishangaza sana na jeuri uliyonayo! Una jeuri flani hivi sio ya kawaida!

Respect.

FMEs!
 
na juzi anakuja kuibaka demokrasia hivi hivi bila sababu za msingi.

Mtei anasema CCM walipenyeza fedha pasi kuwataja ni akina nani waliopokea fedha.!

Chuki binafsi tu hakuna kitu hapo.
Heko mzee Mtei tunatambua mchango wako na tunatambua unaona mbali.
 
Kumridhisha mtanzania ni ngumu sana, baba yangu Mtei wengine wanakushambulia kwa kukuona mjinga vile hukuiba mali za taifa hili kama ndg zao wanavyofanya, wengine wanakushambulia kwa vile hawakuelewi, wazee wangapi wa umri wa baba yangu huyu wameandika vitabu/historia ya nchi yetu? tunapenda udaku zaidi ya serious issues!
 
..Mzee Mtei ni Gavana mwanzilishi wa Benki Kuu ya Tanzania.

..moja kati ya majengo ya BOT yanapaswa kupewa jina lake kama heshima kutokana na mchango wake kwa taasisi hiyo.

..Mzee Mtei pia alikuwa mwenyekiti wa Tume ya Raisi ya kurekebisha mfumo wa kodi Tanzania.

..mapendekezo ya ripoti ya Tume ya Mtei ndiyo yaliyopelekea kuanzishwa kwa Mamlaka ya Mapato[TRA].
 
Huyu mzee hakuwa gavana kwa merit bali alibebwa na nyerere ndio maana uchumi ukafa.kwenye hicho kitabu kaeleza alivymzuia zitto kabwe ili mwanawe awe mwenyekiti?

Ni kitabu cha kikabila zaidi kuliko utanzania.ndio maana mengi amepewa nafasi kubwa.huyu mzee anatapata tu

Navyojua Mtei aliteuliwa (i.e., appointed) na Rais kuwa Gavana kama magavana wote wa Benki Kuu ya Tanzania tokea Uhuru.

Sasa hiyo "merit" unayozungumzia sijui inakuja vipi hapa. Au pengine utupe mfano wa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania aliyepata cheo hicho kwa ushindani kwenye soko huria la kazi na matokeo yake ikawa uchumi wa nchi ukaboreka kutokana na uongozi wake?
 
jamani sasa nadhani ustaarabu umetushinda. mtu kaandika historia ya maisha yake anaitwa mkabila....huu ni upunguani kabisa. je mnataka historia yake iiandikwe akishakufa ili mpotoshe zaidi........ najua watu wengi walialikwa kwenye uzinduzi wakaingia mitini kisa mzee ni mwanzilishi wa chadema....subiri hapo mdogo wake ridhiwani aoe watakimbizana kutoa michango kama mbuzi wanaokimbilia maji mtoni..... akifariki kesho mzee mtei kwenye mazishi utwaona watu kibao na sifa za unafiki

mzee kaonyesha njia wengine waandike zao, tuzione

kanda2 pata nakala, soma, jifunze mazuri yake, alipopotoka wewe usiyarudie kwisha!!!!


tanzania will never develop under ccm
 
Nimefungua JF ili nione wenzangu mnasemaje juu ya kitabu nilichoandika nikijaribu kuweka kumbukumbu ya yale niliyofanya na ninayoyafahamu. Nawashukuru wote wanaonipongeza kwa kukiandika.

Hata hivyo, kila mtu ana uhuru wa kueleza maoni yake, na sioni ni ajabu wanaJF kadhaa kunilaumu. Lakini nikiri kwamba siwaelewi wanaonilaumu kwa kuandika historia hii. Nawashauri watulie na wapate wasaa wa kukisoma hiki kitabu, na ikiwezekana nao waandike upande wao katika kushiriki kuendeleza hili taifa.

Wanaosema Mwalimu Nyerere alinibeba kunipa nyadhifa nilizoshika ktk utumishi wangu, wasome kitabu na historia ya Tanzania kwa jumla. Nilibahatika kuwa miongoni mwa wananchi wachache tuliopata Shahada ya Chuo Kikuu na Nyerere hakutaka kuteua Mzungu aongoze uundaji wa Benki Kuu. Ninavyosema kitabuni, angeweza kumchagua Mtanzania mwingine, na mimi nilijitahidi kwa uwezo wangu kutekeleza majukumu kwa uadilifu na kwa uzalendo kama Mwalimu alivyonuia mambo yafanyike.

Ni upuuzi mtupu kusema Mwalimu alipendelea Chadema eti kwa vile binti yangu aliolewa na mwanae. Huu ni oungo usiothibitika. Wanaosema hivyo wamechanganyikiwa kwa vile Mwalimu alisifu Chadema mwaka wa 1994, mimi nikiwa mwenyekiti. Mbowe alikuwa hajulikani na alikuwa tu ni kijana ktk chama.

Tulitofautiana na Mwalimu, na nakiri kwamba kushindwa kwangu kum persuade kuwa yale niliyokuwa napendekeza yangesaidia Tz, ndiyo weakness yangu kubwa. Kama ningefaulu, historia ya nchi yangu ingekuwa tofauti, na wakina kanda mbili wangekuwa wachache nchini sasa.

Najivunia kuacha BoT ikiwa imara na uchumi ukinoga. US $ 1.00 = Tsh 7.14 wakati niliondoka BoT, 1974. Najivunia pia kwamba niliweza kuchaguliwa Mwenyekiti wa Bodi ya Magavana wa IMF na Benki ya Dunia, 1979/80. Hakuna aliyenibeba hapo. Nilichangia pia katika mchakato w Reform of Monetary system nilipokuwa Deputy katika the Committee of Twenty. Soma kitabu.

Wanaolaumu kuwa nimebaka demokrasia licha ya kuwa najivunia kuasisi Chadema, nawashauri wazungumze na viongozi wa sasa wa chama. Naamini chama kiko imara kutokana na ushauri wangu, na siku muafaka itafika wakati vijana shupavu, jasiri, wabunifu, waadilifu na wazalendo wanaojali maslahi ya wanyonge na ya nchi yao, kama Freeman na Zitto, wataridhisha WaTz. kwamba chama chao kinaweza. Subiri. Iko siku.

Mwishowe nikiri sijui ningefanya nini katika kuzindua kitabu changu ili nijivue uChagga. Ndugu zangu wamezaliwa hivyo na Mchapishaji wa kitabu aliwaalika. Nilikuwa nimwemwalika mrithi wangu BoT, Profesa Ndulu awe mgeni rasmi lakini akapata safari ya ghafla. Hakuweza kuja.

Reginald Mengi akakubali, dakika za mwisho, kuwa mgeni rasmi, na hata haikuwezekana kumtaja ktk card kuwa ni Mgeni rasmi. Watanzania wa nyadhifa za juu, wanaonifahamu vizuri, kama Jenerali Ulimwengu na Ibrahim Kaduma wakakubali kusema machache ktk ile sherehe. Wao sio Wachagga! Ningefanya nini nionekane mimi ni Mtanzania wa kweli?

Nashauri JF wasiwe na prejudice. Tutaweza kufanya makubwa tukiacha prejudice.


Edwin Mtei
 
Huyu mzee hakuwa gavana kwa merit bali alibebwa na nyerere ndio maana uchumi ukafa.kwenye hicho kitabu kaeleza alivymzuia zitto kabwe ili mwanawe awe mwenyekiti?

Ni kitabu cha kikabila zaidi kuliko utanzania.ndio maana mengi amepewa nafasi kubwa.huyu mzee anatapata tu

Kanda2 for your info, Mzee Mtei is well read by the 1960s standards (Makerere University Degree holder). President Nyerere did not pick Mzee Mtei as BoT Governor out of blues but on merit. When Mzee Mtei fell out with President Nyerere the World Bank gave employment to Mzee Mtei. The economic down turn was not caused by Mzee Mtei but by President Nyerere's refusal to adhere to the IMF and World Bank dossier after the Uganda war. What is your opinion as regards the 1995 situation when Nyerere turned down the election of Kikwete in favour of Mkapa? Was Nyerere a father inlaw to Mkapa?
 
Huyu mzee hakuwa gavana kwa merit bali alibebwa na nyerere ndio maana uchumi ukafa.kwenye hicho kitabu kaeleza alivymzuia zitto kabwe ili mwanawe awe mwenyekiti?

Ni kitabu cha kikabila zaidi kuliko utanzania.ndio maana mengi amepewa nafasi kubwa.huyu mzee anatapata tu

Na kweli wewe ni kanda2 kama ulivyojiita. Mawazo yako hayatofautiani na jina ulilojipachika. Mtei alipewa ugavana kwa merit...why not you? Why? Alimzuia zitto kabwe...how? Ni kitabu cha kikabila..wewe andika cha kabila lako tulione!
 
Ni kitabu cha kikabila zaidi kuliko utanzania.ndio maana mengi amepewa nafasi kubwa.huyu mzee anatapata tu

Mzee unaonekana swala la ukabila ni tatizo sana kwako

UKiona mtu anazungumzia ukabila lazima huyo ni MCHAWI (Nyerere)

Na mtu wa namna hiyo ni LESS THINKER

Wewe kwenye hiyo lounch umeona ukabila tuu na hukuona jambojingine la maana.
 
Mzee Mtei,

..asante kwa maelezo yako.

..rafiki yangu ameninunulia kitabu chako kama zawadi.

..nimekipitia kwa haraka-haraka, na so far, sijaona kama kuna ukabila ktk kitabu chako.

..weekend hii nitakisoma nadhani baada ya hapo nitakuwa tayari kujadili kitabu chako na wale waliokisoma.
 
Mzee Mtei,

Hongera! Tuko pamoja!

Ni utamaduni mzuri sana kwa Viongozi wetu kuandika historia ya yale waliyoyafanya kama historia ya nchi yetu!

Nategemea sasa itakuwa changamoto kwa Warioba, Salim, BWM, Mzee Malecela, AHM na wengineo kuandika yao ili kuwapa vizazi vingine urithi tu wa historia yetu!
 
Huyu mzee hakuwa gavana kwa merit bali alibebwa na nyerere ndio maana uchumi ukafa.kwenye hicho kitabu kaeleza alivymzuia zitto kabwe ili mwanawe awe mwenyekiti?

Ni kitabu cha kikabila zaidi kuliko utanzania.ndio maana mengi amepewa nafasi kubwa.huyu mzee anatapata tu

Mkuu huo wimbo wako wa ukabila ni kama kanda upande mmoja,tafadhali geuza upande wa 2 hiyo kanda yako ili tuone kama kuna jipya....Maana naona inasomeka "Kanda2" wakati unapiga oneside peke yake all this time...Bear in mind Utapimwa kutokana na mchango wako,tafadhali changia badala ya kutapatapa,kama mwalimu alikubali kuwa alifanya makosa kutokumsikiliza Mzee Mtei then kubebwa nani alibebwa?Kama alijiuzulu ni wazi alikataa "Kuzombwa" na wala si kubebwa.
Hongera Mzee Mtei,mchango wako kwenye jamii unakubalika na historia itadhihirisha hilo.
 
Wakuu nani mwenye taarifa tunapoweza kukipata kitabu hiki?

Nimekinunua hichi kitabu duka linaitwa "Tanzania Publishing House" au TP House liko mtaa wa Samora karibu na askari monument, next to Saptna au opposite Salamander ilipokuwaga.

.
 
Nimekinunua hichi kitabu duka linaitwa "Tanzania Publishing House" au TP House liko mtaa wa Samora karibu na askari monument, next to Saptna au opposite Salamander ilipokuwaga.

.

Ombi kwa wenye hilo juzuu,

Nomba mliweke pale scribd ili nasi tuweze kulidownload jamani.. msiogope sana akina Mtei walishakula vya kutosha kwani lengo zima si ni kutaka watu wengi waelewe historia ya inji yetu ama ni faida zaidi??

amani
.
 
Ombi kwa wenye hilo juzuu,

Nomba mliweke pale scribd ili nasi tuweze kulidownload jamani.. msiogope sana akina Mtei walishakula vya kutosha kwani lengo zima si ni kutaka watu wengi waelewe historia ya inji yetu ama ni faida zaidi??

amani.

kama hutaki kununua kitabu then acha matusi
na kama unaomba pia uache kejeli na matusi
 
Kweli kwa hakika kuwa mambo kama haya lazima yafanyiwe kazi kutoka kwa waandishi wengine makini Tanzania
 
waheshiwa lazima mjue tofauti ya kitabu ambacho mtu anandia kueleza view zake kisiasa (political views)na kitabua mtua anadika kueleza masha yake (Up bringing) msipamie tu na kutoa lawama manake ni sawa na mtu atakaye soma kitabu cha Mzee Kawawa na kusema mbona hajalaumu kufeli kwa serikali ya CCM na hasa alivyoshiriki yeye.
 
Back
Top Bottom