ubongokid
JF-Expert Member
- Apr 30, 2017
- 2,265
- 4,452
Natumaini wote mtamaliza mwaka salama pamoja na wengine wetu kuanza kuharibiwa kipindi hiki na watu wasiojulikana.
Tanzania ina mashujaa wengi sana ambao ama wamepoteza maisha au kuumia katika harakati za kuleta mabadiliko katika taifa.
Kuna shujaa mmoja ambaye nafikiri ni busara kabla ya mwaka kuisha tutambue nafasi yake adhimu katika ujenzi wa demokrasia hapa Tanzania
Hapa namzungumzia Mh.Freeman Aikael Mbowe.Mwanamapinduzi halisi muwazi asiyekuwa na chuki wala unafiki.Kijana mwenye mawazo endelevu na anayeonyesha kuwa na fikra mbadala ya kupeleka taifa letu mbele.Ni mtu ambaye pamoja na vitisho vingi,manyanyaso mengi,na fedheha nyingi bado amekuwa ni mtu mwenye msimamo na mtazamo wa kipekee.
Freeman Mbowe ndio mwanasiasa pekee ambaye pamoja na ukweli kwamba alitofautiana kimtazamo na mzee Edward Lowasa lakini imani aliyokuwa nao juu ya uwezo hekima ya Mzee Lowasa ulimfanya akubali kusimama mbele ya Watanzania na kusema pamoja na yote huyu ndie anayefaa kuiongoza Tanzania.
Kwa msimamo ule alituonyesha kuwa yeye sio mtu wa visasi na chuki na kwamba anaamini atika uwezo wa mtu na kwamba anaweza kumpa yeyote fursa.
Freeman Mbowe amewapa fursa vijana wengi ndani ya Chadema.Ni katika uongozi wake uliotukuka tumeona vijana machachari na wenye uwezo wa kujenga hoja wakiibuka katika medani za siasa tena bila kujikomba bali ni kwa kuonyesha uwezo wao thabiti.
Freeman Mbowe amekifadhili chama chake kwa kujitoa kwa pekee na kuhatarisha usalama wake na wa familia yake na mali zake lakini bado hakukata tamaa kutokana na imani yake kwamba tanzania bora itajengwa na wenye moyo
Freeman Mbowe anawasilisha mawazo na fikra za wana mageuzi,vijana wa kisasa wenye imani kuwa Tunaweza kuwa taifa la kipekee katika bara la Afrika
Kwa kusema haya napenda nimtakie mwaka mpya mwema ndugu Mbowe na kumwambia kuwa asife moyo wakati wa ushindi u karibu na Mungu yuko upande wake
Aluta Continua
Wasalaam
PBK
Tanzania ina mashujaa wengi sana ambao ama wamepoteza maisha au kuumia katika harakati za kuleta mabadiliko katika taifa.
Kuna shujaa mmoja ambaye nafikiri ni busara kabla ya mwaka kuisha tutambue nafasi yake adhimu katika ujenzi wa demokrasia hapa Tanzania
Hapa namzungumzia Mh.Freeman Aikael Mbowe.Mwanamapinduzi halisi muwazi asiyekuwa na chuki wala unafiki.Kijana mwenye mawazo endelevu na anayeonyesha kuwa na fikra mbadala ya kupeleka taifa letu mbele.Ni mtu ambaye pamoja na vitisho vingi,manyanyaso mengi,na fedheha nyingi bado amekuwa ni mtu mwenye msimamo na mtazamo wa kipekee.
Freeman Mbowe ndio mwanasiasa pekee ambaye pamoja na ukweli kwamba alitofautiana kimtazamo na mzee Edward Lowasa lakini imani aliyokuwa nao juu ya uwezo hekima ya Mzee Lowasa ulimfanya akubali kusimama mbele ya Watanzania na kusema pamoja na yote huyu ndie anayefaa kuiongoza Tanzania.
Kwa msimamo ule alituonyesha kuwa yeye sio mtu wa visasi na chuki na kwamba anaamini atika uwezo wa mtu na kwamba anaweza kumpa yeyote fursa.
Freeman Mbowe amewapa fursa vijana wengi ndani ya Chadema.Ni katika uongozi wake uliotukuka tumeona vijana machachari na wenye uwezo wa kujenga hoja wakiibuka katika medani za siasa tena bila kujikomba bali ni kwa kuonyesha uwezo wao thabiti.
Freeman Mbowe amekifadhili chama chake kwa kujitoa kwa pekee na kuhatarisha usalama wake na wa familia yake na mali zake lakini bado hakukata tamaa kutokana na imani yake kwamba tanzania bora itajengwa na wenye moyo
Freeman Mbowe anawasilisha mawazo na fikra za wana mageuzi,vijana wa kisasa wenye imani kuwa Tunaweza kuwa taifa la kipekee katika bara la Afrika
Kwa kusema haya napenda nimtakie mwaka mpya mwema ndugu Mbowe na kumwambia kuwa asife moyo wakati wa ushindi u karibu na Mungu yuko upande wake
Aluta Continua
Wasalaam
PBK