Freeman Mbowe naomba usistaafu siasa 2018

Freeman Mbowe naomba usistaafu siasa 2018

Kama alivyo poteza muelekeo mkwere baada ya magu kuingia magagoni na sasa siri zote zinaanikwa hadharani mchana kweupeeeeee
Siku zote huwa nasema,chadema inaangamia kwa kukosa maarifa,JK hatagombea uraisi tena....msipigane na kivuli.
 
Upinzani unahitaji fikra mpya. Slaa aanzishe chama.

Mind myopia ni hatari sana, huyu mbowe kama ni kiongozi bora siangeandaa vijana wa mrengo wake? Sisi wote tunajua time is limited, hivyo kuna haja ya kuandaa mbegu bora ya baadae. Mawazo ya MTU mmoja hayawezi kuwa msaada wakati wote, kwa maana hiyo tunahitaji fikra mpya na uongozi mpya ambao utafanya mambo kwa uwazi. Kwa kusema Haya mnaweza kufikiri na kusema Mimi ni mwanaccm,siwazuii ila tuache ukweli utamalaki. Ni kwanini mapato na matumizi ni siri kuu, kwanini ruzuku itumike makao makuu kusiko na wanachama? Nakuwaambia makatibu wa kata,wilaya/majimbo na mkoa kuwa pesa hakuna? Ni lini upendeleo wa ujengaji chama(vifaa na fedha) utakuwa sawa nchi nzima?
Mgawo wa viti maalum vya ubunge imekuwa mwenye kingi kuongezewa, kuna eneo wabunge wakuchaguliwa ni wengi na wanaongezewa wa viti maalum, kwa fikra rahisi ilikuwa ni lazima kuteua wengi kusiko na upinzani ili kuleta vuguvugu la mabadiliko kuliko kuwatenga kabisa.
Nafikiri ni sawa mbowe astaafu.
 
Dr.Mbowe alishamuuzia Chadema Lowassa pamoja na nyumbu wote ndiyo maana siku hizi ofisi za Chadema zipo Masaaki kwa Lowassa.
 
Kipindi kingine cha uongo. Muda ukifika atasema mwenyewe.
 
Wasalaamu humu jukwaani

Mimi sipendi sana kutundika uzi humu
Ila kwa hili Sina budi kujitokeza hadharani kutoka huku milimani na kupitia jukwaa hili kufikisha ujumbe wangu kwa Comrade Dr. Freeman mbowe.

Kutokana na tetes mbalimbali zinazopita masikion mwangu ni kuwa Dr. Freeman mbowe amepanga kustaafu kutoka kwenye siasa za majukwaani na kupisha watu wengine, hizi tetes kiukweli zinatukosesha Amani sisi watanzania tunaopenda maendeleo ya nchi yetu.

Nia yetu ni kukuomba Dr Freeman mbowe ugombee uenyekiti wa Chama tena Kwan bado una millage ya kuona mbali... Chini ya mikono yako Chadema imekuwa kwa 85% bado tunahitaji hizo 15%
kutoka kwako ndio tutakuruhusu upumzike tukiwa Tayari tumeshatimiza malengo yetu
Kukuomba ugombee haimanishi kuwa hakuna mwenye sifa ya kugombea la hasha wapo wengi kina kamanda Lissu, Kamanda mnyika, kamanda sugu, kamanda halima mdee, kamanda mwalimu na wengine wengi ila kwa Kuwa wewe bado uko Safi tunakuomba uendelee kupambana ili tufike kule tunakokusudia, tumetoka mbali naamin tutafika salama japo tumeumia sana kuna ndugu zetu waliotangulia mbele ya haki kwa kuipigania taasisi hii muhimu kwetu wa Tanzania, tena wengine wamedhulumiwa uhai wao na watawala wasiopenda ukwel Lakin damu Yao ndio ujasiri wetu.. Nakumbuka hata wewe walikukosa risasi pale nmc ila hukurud nyuma

Kazi yako tunaitambua Mr. Chairman wengine hawawez kuelezea uhodari wako wanasubiri hadi ufe ndio waje wakupigie saluti

Mungu akulinde Dr mbowe jujawahi kuwa mnafik wala mwongo wa nafs yako juu ya dhamira ya kuikomboa Tanzania kutoka kwenye makucha ya mafisad papa yasiojali wananchi

Ni mimi mtanzania mzalendo
 
Victor
Kama unamenda sana MBOWE nenda kwake kamfulie / kampikie ,toteleea shudu zako hapa kwenye uzi
Hizi sio kauli za kujenga.. Lete mawazo tumshauri Mr chairman aendelee kuongoza jahaz

Kuna mdau hapo juu kasema nyerere aliongoza ccm kwa zaid ya miaka 23 ili tu kukijenga na kukua
 
Kwanza kabisa wee ni mbowe unajipigia promo, KUSTAAFU KUKO PALE PALE, wanachama wanajua hilo.
Pili, yaani mleta mada ktk watu wenye sifa ya kuwa mwenyekiti wa chadema na sugu pia ana sifa?? Kweli nyie bado!
Tatu, unathubutu kabisa kusema mbowe sio mnafiki na sio muongo, unajua maana ya kuaminisha umma kuwa fulani ni fisadi kisha kubadilisha mawazo baadae? Huo ni UNAFIKI na UONGO uliopitiliza.
Acha kumpigia/ kujipigia promo. Mbowe kaexpire ya amebaki na siasa za matukio na chafu. Hafai hata kuwa kichwa cha familia.
Kama kikwete aliweza kuwa Rais wa Tanzania
Sugu anaweza kuwa mwenyekiti bora kabisa
 
Kwani Mtei alipoanzisha hicho kitega RUZUKU alianzishia Canadai? Mbowe ni mkwe wa Mtei na hiyo ni taasisi yake. Mbowe ametengua katiba ya ili aendelee kuongoza. Zitto alipotaka uenyekiti akafukuzwa. Zitto kwa weledi wake wa uchumi alitaka hesabu za ruzuku zikaguliwe,Chama kikataka akitonye. Mbowe hawezi staafu maana alishatengua katiba ya chama ili aendelee kuwa Mwenyekiti milele. Aeleze Lowasa alileta shilingi ngapi na ripoti za ukaguzi wa kujitegemea zitoke. Ruzuku ni mali ya watanzania.
Mkuu huu mchezo hauitaji hasira
Acha kutoa mishipa
Mwerevu hawezi kutunga story hizi na wenye akili wakakuamini
Ayatollah ni pandikizi toka familia ya kikwete kupitia vijana wake kina February na mwigulu
 
Mkuu huu mchezo hauitaji hasira
Acha kutoa mishipa
Mwerevu hawezi kutunga story hizi na wenye akili wakakuamini
Ayatollah ni pandikizi toka familia ya kikwete kupitia vijana wake kina February na mwigulu
Pandikizi mtu aliyewapa umaarufu. ZZK. Hamna stori ya kutunga hapo juu kijana,wewe shupaa watu wanakula maisha kwa ruzuku.
 
Wasalaamu humu jukwaani

Mimi sipendi sana kutundika uzi humu
Ila kwa hili Sina budi kujitokeza hadharani kutoka huku milimani na kupitia jukwaa hili kufikisha ujumbe wangu kwa Comrade Dr. Freeman mbowe.

Kutokana na tetes mbalimbali zinazopita masikion mwangu ni kuwa Dr. Freeman mbowe amepanga kustaafu kutoka kwenye siasa za majukwaani na kupisha watu wengine, hizi tetes kiukweli zinatukosesha Amani sisi watanzania tunaopenda maendeleo ya nchi yetu.

Nia yetu ni kukuomba Dr Freeman mbowe ugombee uenyekiti wa Chama tena Kwan bado una millage ya kuona mbali... Chini ya mikono yako Chadema imekuwa kwa 85% bado tunahitaji hizo... 15%
kutoka kwako ndio tutakuruhusu upumzike tukiwa Tayari tumeshatimiza malengo yetu
Kukuomba ugombee haimanishi kuwa hakuna mwenye sifa ya kugombea la hasha wapo wengi kina kamanda Lissu, Kamanda mnyika, kamanda sugu, kamanda halima mdee, kamanda mwalimu na wengine wengi ila kwa Kuwa wewe bado uko Safi tunakuomba uendelee kupambana ili tufike kule tunakokusudia, tumetoka mbali naamin tutafika salama japo tumeumia sana kuna ndugu zetu waliotangulia mbele ya haki kwa kuipigania taasisi hii muhimu kwetu wa Tanzania, tena wengine wamedhulumiwa uhai wao na watawala wasiopenda ukwel Lakin damu Yao ndio ujasiri wetu.. Nakumbuka hata wewe walikukosa risasi pale nmc ila hukurud nyuma

Kazi yako tunaitambua Mr. Chairman wengine hawawez kuelezea uhodari wako wanasubiri hadi ufe ndio waje wakupigie saluti

Mungu akulinde Dr mbowe jujawahi kuwa mnafik wala mwongo wa nafs yako juu ya dhamira ya kuikomboa Tanzania kutoka kwenye makucha ya mafisad papa yasiojali wananchi

Ni mimi mtanzania mzalendo
 
Hii ni tetesi haswaa!

Kwamba chama amekikuza kwa 85%, unapenda amalizie hiyo 25%! Dah ama kweli ni Tezi la tetesi! Shule zingine hizi jamani!!!!
Umeona Hilo tu

Kwa hiyo ndio unahisi mimi ninaweza kufanana na wewe kufikir
Bora uongee mengine brother usimdharau usiemjua tena nyie mnaojifanyaga mnamjua mmetokea kwenye dhiki ya kutupwa
 
Kama habari za kustaafu za bwana Mbowe ni za kweli basi zitakuwa habari njema kwa wale wote wanaoitakia mema CHADEMA.CHADEMA pale ilipo inahitaji mabadiliko makubwa sana, mabadiliko kuanzia kwenye image ya nje ya chama.CHADEMA inahitaji Mwenyekiti mpya ambaye akiingia tu jambo la kwanza ni kuhakikisha chama kinajenga makao makuu yake mapya,tena ya kisasa na ya kupigiwa mfano ambayo ita_accommodate offices za jumuiya mbalimbali za chama kama vile BAVICHA,BAWACHA,BARAZA LA WAZEE,nk.Ikiwezekana pia office ya media house ya chama iwemo humo humo kwa mfano TV na radio. Mwenyekiti mpya anapaswa kufanya mabadiliko makubwa ya kimfumo,hasa kuweka sawa baadhi ya vipengele vilivyomo kwenye katiba,vingi vina mapungufu mengi sana vinavyopelekea baadhi ya viongozi ku_abuse katiba kwa maslahi yao.Ifike wakati katiba izipe meno mamlaka za kimaamuzi kama baraza kuu la chama,kamati kuu ya chama na mkutano mkuu wa chama kuwadhibiti viongozi wabadhilifu na wanaotumia madaraka yao vibaya.Lazima CHADEMA ianze kujenga misingi imara itakayosaidia kuwapata viongozi safi na wenye uwezo mkubwa, tena watakaopatikana ktk mazingira ya haki na ya kidemokrasia.CHADEMA haiwezi kwenda mbele kwa kumng'ang'ania mtu mmoja tu,hiyo tu peke yake inaonyesha jinsi chama kilivyo dhaifu mno kama taasisi.Chama kinahitaji mawazo mapya,fikra mpya,mwonekano mpya,muundo na mfumo mpya ili kisonge mbele.
Mkuu kujenga afisi sio kipaumbele cha Chama

Kipaumbele ni kutoa uraia kwa mwananchi aweze kijitambua na kujielewa
Chadema inawanachama ziadi ya million 6 bado washabik bila kutoka elimu ya Uraia wanachama wasingefika hata million

Sawa na kumpa mtoto wako pesa afanye biashara wakati hajaitimu hata shule ya msingi, that's the worst of money
 
Pandikizi mtu aliyewapa umaarufu. ZZK. Hamna stori ya kutunga hapo juu kijana,wewe shupaa watu wanakula maisha kwa ruzuku.
You can't be serious
Ayatollah aipe umaarufu chadema kwa Dr slaa ningekubali kuwa anamchango wake

Ayatollah anamchango bungeni kabla ya kuhadaiwa na pesa.... Na mchongo ulikuwa ni kujenga jina Lake sio taasisi ya chadema
 
Mie nashauri atumie busara aachie wengine waje na mawazo mapya mambo aliyoyafanya ni mengi na makubwa ni wakati muafaka akabaki kama mshauri tu
 
Ulikimbia hesabu. Hebu rudia upya

Nusuhela,
Naona huyu jamaa hesabu alipata sifuri yenye masikio!Anampongeza Mh.Mbowe kwa kufanikisha CHADEMA/UKAWA kwa 85% halafu anamsihi asistahafu ili amalize 25% iliyobaki! Hesabu sahihi ni 100-85 inabaki 15%.
Lakini niseme kuwa Mh. Mbowe ni mwanasiasa mahiri,mweledi, mwenye maono na mikakati mipana sana!Ni bakhti mbaya sana nchi hii haina Demokrasia ya kweli vinginevyo CHADEMA/UKAWA wangelikuwa Ikulu kwa sasa kama siyo rafu za CHAMA CHA MAJIPU-CCM kwa Uchaguzi wa 2015!
CCM wanalijua hili hata JPM analijua hili!
Wasalaam.
 
You can't be serious
Ayatollah aipe umaarufu chadema kwa Dr slaa ningekubali kuwa anamchango wake

Ayatollah anamchango bungeni kabla ya kuhadaiwa na pesa.... Na mchongo ulikuwa ni kujenga jina Lake sio taasisi ya chadema
Tehe tehe! Mbowe amewauza kwa EL kavuta chake. Si unajua Pombe atachomoka 2025,2025 tunawapiga mpaka 2035. Endeleeni kula ruzuku na SACCOS yenu. EL atasimama tena 2020 anahisi alikosea padogo! Elimu.. Elimu ... Elimu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom