Free talk: Mwanamke shtuka!

Hahahaaaaa! NANDERA nilikumisimo jamani.
Heaven Sent njoo huku.

Nyakati zimebadilika ujue, naona mabadiliko makubwa hata kwao wanaume. Soon marioo watajikuta wamegeuka tunagombania nao wanaume maana hakutakuwa na mwanamke mfuga marioo.
 
Ni kweli mama, ukishajizoesha kutafuta unaunga tela tu, ila kama haujazoea ndio unaanza upyaaaa. Mtoto alikuwa feza unamrudisha kidumu na mfagio. Hadi mambo yaje yakae sawa umeisoma namba vya kutosha.
 
Na kuna wanaume nao wanapenda kutegemewa ili wamuendeshe mwanamke. Anajua hata akufanyie nini hutapata uwezo wa kuondoka. Nawaambiaga rafiki zangu hata kama unapewa mpaka hela ya pad jifunze kutafuta chako ili siku kupewa kukikata ujue kujisimamia.
Mwanaume mzigo huyo, mawazo mgando kabisa hayo. Fanya nafasi yako kama mwanaume nawe utaheshimika tu, haina haja ya kumnyanyasa mtu kwa kigezo cha "kuheshimiwa".
 
Umenifanya nimekumbuka kuna story ililetwa humu na mtu ambae kaka yake aliwasomesha wao alafu alipokufa wakasahau familia yake. Watoto na mama yao wakapigwa na maisha hatari. Na ni kwasababu hakumuandaa mkewe kwa maisha ya kesho.
 
Kuna watu ujue hawatoi zaka,fungu la 10 wala sadaka ya kuteketeza wala ya kawaida si kanisani wala msikitini...lakini kumpa hata mtu pipi tuu ya 150 anaona dhambi,.basi hata uonge napo 0 jomoniii....mfyuuuu
Hahahaaaa!! Kutotoa sadaka haoni kama ni dhambi ila kukupa mpenzi wake ndio anaona dhambi.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…