Birthday ya Mzee Simaro Masiya Lutumba, kumaliza miaka 70.
Huyu Mzee aliandika zaidi ya asilimia 50 ya miziki yote ya TPOK Jazz. Sam Mangwana na Boyibanda wakiwa kwenye stage. Boyibanda ni yule jamaa alikuwa akicheza Break (robot) kwenye zile video za mwaka 1975.
Hata watoto mitaani waliamua kumpa heshima yake mzee kwa kuimba miziki yake.
Hapa mzee na wanae wakizi-Medley miziki ya POET Lutumba.
Safari, lazima umsikilize huyo mtoto hapo juu. Kwa kweli aliniuwa hasa anapoimba "Bina na ngai na respect."
Watu wanaimba,wengine wana bana pua,wengine studio za kichina zinawashine suati zao...LAKINI..huyu jamaa... alikuwa mwanamziki kweli na kipaji kutoka kwa Mungu.Mfalme wa rhumba(Le grand maiter),mchawi wa gitaa(guitar sossuor).
Kwa upande wangu mimi ndio chaguo langu la kwanza dunian pamoja na kundi lake loooote la Le Tuitor Puisant (All Power)ok jazz,kuanzia Madilu,Sager essuso,Simaro lutumba masia,Sam Mangwana'KICHWA BALAA', josky kiambukata,Mavitukuvisi & much moreee!
Je wewe unamuelewaje Franco na TP Ok jazz nzima??????
Translation and lyrics za Layile by Franco & Jolie Detta
SIDA na wimbo unaitwa Attention na SIDA, maana yake Be careful with AIDS.niliwahi kusikia kuwa alifariki kwa Ukimwi, 1989 nadhani.
Ugonjwa ambao hata yeye mwenyewe aliupiga vita kupitia wimbo wake wa SADA (tafsiri ya AIDS kwa Francais).
All in all, Franco was great...
Nakumbuka wimbo wake wa Balo Baki ft. Mangwana...
Kuna pale penye wanaimba Kiswahili,
"...Mimi na wewe, kisa gani Mwanamboka?"
Top ten yangu ya nyimbo za Franco TP OK JAZZ:
1. Sadou 2. Matata ya Mwasi Esilaka te. 3. Liberte, 4. Non, 5. Mamou, 6. Testament ya Bowule. 8. Tangawusi. 9. Kadima. 10. Bondowe. TP OK JAZZ.
Mkuu wewe umeniona nini nna headset hapa nasikilita Tangawusi. Huyu jamaa mungu alimtunuku hasa, nikisikiliza nyimbo zake nakumbuka miaka ya mwanzo ya themanini nikiwa mdogo kaka zangu walikuwa wakizisikiliza sana hizi nyimbo na mzee wangu! na hata quality ya nyimbo zake ni za hali ya juu sana zilirekodiwa kwenye mitambo ya kisasa sana tena mnoo! hebu sikiliza Tokabola sentiment aliyoimba Josky kiambukuta!
Nakumbuka mwaka 1984 nikiwa songea tulikuwa na kanda yake, moja ya wimbo uliokuwepo ni mbanda ako ti kikumbi, saa yale matamshi ukisikiliza ni km anaimba matakoni kivumbi, basi si nikajirekodi kweli hiyo chorus eti matakoni kivumbi eeeeh mwanamama hahaha sister angu alikuwa anacheka hana mbavu.
Wimbo wa Mario part 1 unanikumbusha sana bustani ya nyanya aliyolima kaka yangu mwaka 1984-85. nilikuwa nikirudi toka shule wakati huo nipo std 4 basi nakuta bro kauweka, nikiingia ndani tu mdingi anaamka ananiambia badirisha yuniform nenda kamwagie nyanya, wakati huo mie sina mpango kabsaa wa kwenda bustanini, natorokea kiwanjani kupiga chandimu, nikirudi tuu saa moja moja ni bakora kwa kwenda mbele!
Hebu sikiliza Matata ya mwasi basi kwa leo halafu uniambie Franco amekukuna vipi
Ktk zoote mkuu fanya ubandue kadhaa kisha weka ngungi, mobutu, na pesa position.