mbingunikwetu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 13,663
- 18,037
- Thread starter
- #101
Usishangae, soma maandiko! Alimwingilia mjakazi kwa kushawishiwa na Sara mke wake! Baada ya kitendo hicho Hajiri aliendelea kuitwa MJAKAZI na Ibrahimu (Mwanzo 16:6), na mwanzo 21:10-12. Hapa Ibrahimu aliambiwa na Sara "mfukuze MJAKAZI huyu na mwanawe.....". Sara hakusema mfukuze mkeo huyu!Hayo maneno ya kashfa dhidi ya baba wa Imani Ibrahim yanaogopesha, hivi utaanzaje kwa mfano kumuita baba wa Manabii, baba wa Mataifa, Baba wa Imani kuwa ni mzinifu?.
Hivi mnalijua nyinyi daraja la Abraham mbele ya Mungu.
Yaani mwamhukumia dhambi Baba wa Imani?.
Ogopeni ndugu zangu, acheni kabisa ni hatari
Kingine ambacho unapaswa kukijua ni kuwa Waisrael walikuwa hawaruhusiwi kuacha wake zao kipindi hiki! Kama Hajiri angekuwa mke isingewezekana kumfukuza! Waisrael walikuja kuruhusiwa baadaye na Musa kuwapa talaka wake zao kutokana na ugumu wa mioyo yao, lakini tangu mwanzo haikuwa hivyo. Hayo ni maneno ya Yesu kama ninavyomnukuu kwenye Mathayo 19:7-8 "Wakamwambia, jinsi gani basi Musa aliamuru hati ya talaka na kumwacha? Akawaambia , Musa kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu, lakini tangu mwanzo haikuwa hivi"
Ni ukweli mchungu kwa baadhi, lakini ni ukweli ulio wazi kuwa Ishmael ni wa nje ya ndoa! Hapaswi kurithi hata kwa mujibu wa hiyo dini yenu!