Foleni za magari dar zapatiwa ufumbuzi

Ukitazama kwa makini foleni za magari jijini kati Dar utagundua kuwa almost 60-70% ya magari ni ya watu binafsi. Utakuta foleni kwa mf inatoka manzese hadi magomeni ina magari 40 binafsi na mtu mmoja au wawili kila gari, jumla 40-70 na utakuta costa 5 tu zenye watu jumla zaidi ya 100.

Ningekuwa mimi ni Raisi au Waziri mwenye dhamana ningefanya yafuatayo kupunguza foleni.
1. Ningenunua mabasi ya serikari, 5 kila route then ningepiga marufuku gari binafsi kuingia jijini kati. Magari hayo yangeendeshwa na kusimamiwa na SUMATRA
2.Ningeanzisha congestion fee ambayo ni pesa taslim mtu atakayolipa kama anataka kuingia na gali lake mjini kati.
3.Wenye magari binafsi ningewashauri waache magari yao nje ya mji mfano, mbezi ya kimara, tegeta, buguruni, tabata, n.k. then wapande costa au magari ya serikali ambayo nauli yake ingekuwa reasonable.
Kwa kufanya hivyo;
1. Nina uhakika kama kuna foleni ya magari kutoka jangwani hadi magomeni itakuwa ina magari 20- 30 yenye watu kati ya 500- 1000, je hapo si nitakuwa nimebakiza safari kaTI YA 5-10 na kuwamaliza watu walio kariakoo wanaongoja kwenda mbezi? nina uhakika foleni haitakuwa ndefu na safari ya kufika kimara au mbezi kutoka kariakoo itachukua muda usiozidi dk90 badala ya masaa 3 ya sasa.
2. Nitawapunguzia kazi traffic kwani hawatakuwa na ulazima wa kuongoza magari kwenye mataa labda umeme ukatike.
3. Nitapunguza gharama ya maisha kwa wenye magari ya kununua mafuta ya 20,000 kila siku.
4. Nitakuwa nimeleta usawa barabarani kati ya tajiri na maskini.
5.Nitakuwa nimewapa nafasi vijana wanaokopa pesa benki na kununua magari(starlet n.k.) kuitumia pesa hiyo kwa mambo ya maendeleo kama kununua viwanja, kujenga nyumba, kununua furniture n.k.
6. Nitakuwa nimetoa nafasi za kazi kwa madereva na wafanyakazi wa magari hayo ya serikali.
7.Nitakuwa nimeondoa adha ya watu kuamka saa 10 alfajiri kutoka mbezi ili wawahi foleni.
8.Nitawapa wanandoa muda wa kuwahi kutoka kazini kwenda nyumbani kuonana na familia na kutoa malezi kwa watoto badala ya sasa ambapo wafanyakazi wanangojea foleni iishe posta saa3 usiku ndo wawashe magari yao kwenda mbezi wanakofika saa 4.30 usiku na kukuta watoto wamelala na wapenzi wao wamechoka hata hawawezi kufurahia ushirika wa familia.
9. Kwa kufanya hivyo hata barabara zangu za mabasi yaendayo kwa kasi zitakuwa na maana na maisha ndani ya bongo yatakuwa super.
Hayo ni mawazo yangu, I stand to be corrected.
Mawazo yako naona bado hatasaidia tatizo la foleni Kwa jiji la DSM, swali ni mjia gani walitumia mfumo huo na kufanikiwa? Bado kila siku majengo makubwa yana jengwa city center na miundombinu ni ileile. Solution kwa wazuiwe ujenzi waa majengo makubwa city center, wizara na ofisi za serikali zihamie Dodoma, yatengenezwe masoko manne pembeni mwa mjia kama mbadala wa Kariakoo, miundombinu ipanuliwe na kuboreshwa, zijengwa fly high way
 
Maskini umesahau kuwa mapato yetu yanatokana na ukamuaji kodi kwenye mafuta. Wakipunguza magari/foleni wapi tutapata ankara mkuu. Subiri kidogo tupate vyanzo mbadala.
 
Kwa ufupi jibu ni hili hapa:

Watu (Wahandisi) wa URBAN PLANING na TRAFFIC ENGINEERING kukaa pampja na kuupanga MJI mzima wa Dar na vitongoji vyake. Watu wa fedha nao inabidi wawepo karibu kusema watatowa hela kiasi gani .......

Serikali ikubali kulifanyia kazi JIBU litakaloletwa na hao Wahandisi.

POLISI na hasa Traffic Polisi, wawe tayari kulinda SHERIA mabadiliko yote yatakayowekwa kwenye barabara.

Camera ziwekwe kwenye maungio yote na juu ya barabara ili kuwadaka wavunja sheria zote.

Hilo likifanyika basi foleni zitapungua sana. Vinginevyo itakuwa kupoteza tu hela.

Mleta MADA: Mabasi matano kwa ROUTE kwenye mji wa Dar ambao sasa kama sikosei una watu Milioni 3, sijui kama ulikuwa unasema kweli au ulikuwa unatania. Kwa walioishi miaka ya 70 na 80 wakati hakuna Daladala, watakuambia kulikuwa na UDA ngapi kwa route moja. Pia haya mambo yote, huwa yanaamuliwa kwa kufanya utafiti wa kuhesabu watu wakati wa PEAK hours na hapo ndipo utaamua kila route ipate magari mangapi na si kusema kila moja magari matano...... kwa basic zipi?

Huwezi pia kuweka malipo ya kuingia mjini na gari wakati hujaweka njia mbadala ya watu kutumia. Wenzenu wana Trains, Trams, ferries, Metro, Mabasi kwenye lanes special, nk nk. Sasa Tanzania ukisema watu walipe, ili iweje? Watakugomea siku moja nchi nzima watu wasiende kazini, hapo ndiyo utajiona hazitoshi.
 
Ningekuwa mimi ni Raisi au Waziri mwenye dhamana ningefanya yafuatayo kupunguza foleni.
1. Ningenunua mabasi ya serikari, 5 kila route then ningepiga marufuku gari binafsi kuingia jijini kati. Magari hayo yangeendeshwa na kusimamiwa na SUMATRA
3.Wenye magari binafsi ningewashauri waache magari yao nje ya mji mfano, mbezi ya kimara, tegeta, buguruni, tabata, n.k. then wapande costa au magari ya serikali ambayo nauli yake ingekuwa reasonable.

Kwa kufanya hivyo;
3. Nitapunguza gharama ya maisha kwa wenye magari ya kununua mafuta ya 20,000 kila siku.
4. Nitakuwa nimeleta usawa barabarani kati ya tajiri na maskini.
.
Hayo ni mawazo yangu, I stand to be corrected.

Namba 1 na 3 hapo juu, unadhani hayo mabasi matano ndiyo yatatosheleza kuchukuwa abiria wote wa maeneo hayo?
Wenye magari tuwache magari yetu nje ya mji kuna usalama gani na miundombinu gani ambayo itawezesha magari kukaa kwa usalama?

Kwenye namba 3 ya chini aliyenunua gari bila ya shaka ameshajifanyia tathmini ya uwezo wake wa kununua mafuta. Kwa nini ikutie hofu wewe?

Usawa wa barabarani mjomba hautakuwepo mpaka mwisho wa dunia. Hebu angalia hata hivi sasa wengine wanapanga bajeti kuongeza lita 10 za mafuta, wengine wana magari cylinder 8 akivurumisha tu tayari lita 5 zimeshakwenda na anaweka full tank.

Kwa hivyo hiyo haina uhalisia.
 
Wazo zuri ila unazungumzia mji ambao:-
1.watu bado wanaliwa pesa kwa kucheza karata tatu.
2.watu bado wanagongwa na magari manzese pamoja na kuwepo kwa daraja la watembeaji.
 
Serikali ianze kutoa huduma kwa wananchi!! huu ni upuuzi mwingine. Hivi lini sekta binafsi itatambulika? Katika utoaji huduma hakuna serikali inayoweza kujiita efficiency zaidi ya sekta binafsi. Kitu cha msingi na cha maana ni kutengeneza miundo mbinu. Hili halikwepeki. Jiji la Dar halina magari mengi kihivyo. Ukimaliza ni uwezeshaji wa sekta binafsi kupitia mabenki, sheria na masoko ya fedha kuwepo na mabasi ya abiria 100+. Makampuni ndio yafanye hii na mabasi yawe na lane zao. Watu wanakpimbia starlet kwa sababu ya usafiri mbovu. Usafiri ukiwa wa kueleweka haya hayatakuwepo. Miundombinu iwepo maeneo mengi ya jiji. Watu maofisini wajifunze kuwa shida za wananchi zinaweza kujibiwa kwa barua na hata email na simu pia.
 
Ukitazama kwa makini foleni za magari jijini kati Dar utagundua kuwa almost 60-70% ya magari ni ya watu binafsi. Utakuta foleni kwa mf inatoka manzese hadi magomeni ina magari 40 binafsi na mtu mmoja au wawili kila gari, jumla 40-70 na utakuta costa 5 tu zenye watu jumla zaidi ya 100.

Ningekuwa mimi ni Raisi au Waziri mwenye dhamana ningefanya yafuatayo kupunguza foleni.
1. Ningenunua mabasi ya serikari, 5 kila route then ningepiga marufuku gari binafsi kuingia jijini kati. Magari hayo yangeendeshwa na kusimamiwa na SUMATRA
2.Ningeanzisha congestion fee ambayo ni pesa taslim mtu atakayolipa kama anataka kuingia na gali lake mjini kati.
3.Wenye magari binafsi ningewashauri waache magari yao nje ya mji mfano, mbezi ya kimara, tegeta, buguruni, tabata, n.k. then wapande costa au magari ya serikali ambayo nauli yake ingekuwa reasonable.
Kwa kufanya hivyo;
1. Nina uhakika kama kuna foleni ya magari kutoka jangwani hadi magomeni itakuwa ina magari 20- 30 yenye watu kati ya 500- 1000, je hapo si nitakuwa nimebakiza safari kaTI YA 5-10 na kuwamaliza watu walio kariakoo wanaongoja kwenda mbezi? nina uhakika foleni haitakuwa ndefu na safari ya kufika kimara au mbezi kutoka kariakoo itachukua muda usiozidi dk90 badala ya masaa 3 ya sasa.
2. Nitawapunguzia kazi traffic kwani hawatakuwa na ulazima wa kuongoza magari kwenye mataa labda umeme ukatike.
3. Nitapunguza gharama ya maisha kwa wenye magari ya kununua mafuta ya 20,000 kila siku.
4. Nitakuwa nimeleta usawa barabarani kati ya tajiri na maskini.
5.Nitakuwa nimewapa nafasi vijana wanaokopa pesa benki na kununua magari(starlet n.k.) kuitumia pesa hiyo kwa mambo ya maendeleo kama kununua viwanja, kujenga nyumba, kununua furniture n.k.
6. Nitakuwa nimetoa nafasi za kazi kwa madereva na wafanyakazi wa magari hayo ya serikali.
7.Nitakuwa nimeondoa adha ya watu kuamka saa 10 alfajiri kutoka mbezi ili wawahi foleni.
8.Nitawapa wanandoa muda wa kuwahi kutoka kazini kwenda nyumbani kuonana na familia na kutoa malezi kwa watoto badala ya sasa ambapo wafanyakazi wanangojea foleni iishe posta saa3 usiku ndo wawashe magari yao kwenda mbezi wanakofika saa 4.30 usiku na kukuta watoto wamelala na wapenzi wao wamechoka hata hawawezi kufurahia ushirika wa familia.
9. Kwa kufanya hivyo hata barabara zangu za mabasi yaendayo kwa kasi zitakuwa na maana na maisha ndani ya bongo yatakuwa super.
Hayo ni mawazo yangu, I stand to be corrected.

Pole sana Oba kwa mawazo ya Kusadikika. Nikirejea kwenye kitabu cha Shabaan Robert nakumbuka kuna kiongozi mmoja wa nchi ya Kusadikika alinga mawazo ya kupanua barabara kama yalivyowasilishwa na mmoja wa wajumbe waliotumwa. sababu yake alisema hakuna sababu ya kupanua barabara na kujenga madaraja yanayodumu kwa miaka zaidi ya 100 kwa vile eti mguu wa mwanadamu si zaidi ya futi moja na aushi ya mwanadamu haizidi miaka 100. Endelea na njozi zako
 
Nitakutafutia ajira kwenye magazeti ya udaku naona unajua kuweka kichwa cha habari cha kuvutia huku habari haivutii!, umenipotezea muda!
 
Good idea. Lakini parking ya hayo magari yote yanayoachwa nje kidogo ya jiji inatakiwa ijengwe kwanza ikiwepo ulinzi wake pia.
 
Back
Top Bottom