kitwangaz
Member
- Aug 22, 2016
- 92
- 32
Nyie ma Leteni michango ya wahanga wa tetemeko.Mhalifu afanye yake halafu aje mjadiliane? Ndugu Focus Bora umeamua kumshtaki kwa umma huyu 'mchawi' ajulikane.
Mwambie sizonje asitufanyie usanii
Nyie ma Leteni michango ya wahanga wa tetemeko.Mhalifu afanye yake halafu aje mjadiliane? Ndugu Focus Bora umeamua kumshtaki kwa umma huyu 'mchawi' ajulikane.
Kwa hiyo unaMCHAMBA baba yake Ben au!?Sasa Kama unamuuliza Mbowe nyie mna polisi,usalama wa taifa na jeshi na nyie bado mnalalamika na kumlaumu Mbowe,Kama mmeweza kwa Lema mkamweka ndani Leo mwezi na ushee mnashindwa nini kumkamata Mbowe.kama mliweza kumtumia Hakim SMS na kubadili mawazo ya kumpa Lema dhamana mnashindwa nini kumkamata Mbowe
sheer irrelevantNyie ma Leteni michango ya wahanga wa tetemeko.
Mwambie sizonje asitufanyie usanii
Huyu baba angemwangukia rafiki wa mwanawe, wengine wakiingilia wataonekana wanaharibu evidence. Nashindwa kumuelewa kabisa.View attachment 449192
BABA WA BEN SAANANE AFUNGUKA
UPENDO MOSHA NA SAFINA SARWATT – MOSHI
SAKATA la kupotea ghafla kwa aliyekuwa msaidizi wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Bernard Saanane, limechukua sura mpya, baada ya familia yake kumjia juu mwajiri wake, Chadema, kwa kile inachodai chama hicho kimeshindwa kuonyesha dhamira ya dhati ya kumtafuta.
Akizungumza na MTANZANIA jana, baba mzazi wa Saanane, Focus Saanane, alisema anashangazwa na hatua ya Chadema kushindwa kujitokeza hadharani kumtafuta mwanae ambaye amepotea katika mazingira ya kutatanisha.
“Tangu mwanangu Ben amepotea, hatujawahi kumuona (Freeman) Mbowe ambaye ndiye mwajiri wake kama amechukua hatua yoyote ya kukutana na familia yangu, tukashauriana namna ya kumtafuta. Ukimya huu umenistajabisha mno.
“Nilitegemea angekuwa mtu wa kwanza kuja kwangu, tuone njia gani ambayo tunaweza kutumia kumpata Ben. Naumia mno ndugu yangu,” alisema Focus.
Alimtaka Mbowe ajitokeze na kuipa familia taarifa za mahali alipo Ben, kwani wao wametawaliwa na hofu kubwa kutokana na kijana wao kutoweka akiwa mikononi mwake.
“Ninamtaka Mbowe aniletee mwanangu Ben akiwa mzima, nashindwa kujua yupo wapi na nini kinaendelea mpaka sasa kati yake na Ben, haiwezekani mwajiri ashindwe kujua mfanyakazi wake alipo mpaka sasa… bado haliniingii akilini mwangu… suala hili halileti taswira nzuri kwa jamii kama anaendelea kukaa kimya na hazungumzi chochote, si haki,” alisema.
Akizungumza kwa jazba, Focus aliiomba Serikali na vyombo vyake vya dola isaidie kumtafuta Ben kwa nguvu zote kutokana na juhudi za familia kugonga mwamba.
Pia alikanusha vikali taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii na baadhi ya vyombo vya habari, kuwa Ben amefariki dunia. Kwamba familia yake imeitwa na Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro kwenda kutambua maiti moja iliyochomwa moto maeneo ya Uru Ongoma. Kata ya Uru Kaskazini wilayani Moshi.
CHADEMA
Akijibu malalamiko hayo, Msemaji wa Chadema, Tumaini Makene, alisema si kweli kama Mbowe ameamua kukaa kimya, bali wao wameiachia Serikali kufanya uchunguzi wa kina na kutoa taarifa.
“Wakati jambo hili linatokea, mwenyekiti wetu (Mbowe) alikuwa nje ya nchi, naelewa presha aliyonayo mzazi wa Ben katika suala hili, tunaendelea kuhangaika nalo na kutaka vyombo vya dola vichukue hatua.
“Tunaitaka Serikali ifanyie kazi mambo matatu ambayo yako ndani ya uwezo wake, iseme wapi alipo Ben, mara ya mwisho aliongea kwa simu yake na nani na wapi na itumie kila aina ya uwezo wa kumleta kwa sababu si mtuhumiwa,” alisema Makene.
RPC
Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa, aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake jana, kuwa uchunguzi uliofanywa na jeshi hilo kuhusu mwili uliookotwa eneo la Uru Ogoma, si wa Ben kama ambavyo iliripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari.
“Uchunguzi uliofanywa umebaini aliyefariki ni Steven Kimario (55), mkazi wa Sanya Juu wilayani Siha, ambaye aliuawa kwa kupigwa na wananchi wenye hasira, baada ya kukutwa akifanya jaribio la kubaka mtoto wa dada yake mwenye umri wa miaka tisa.
Inawezekana hawana urafiki wa karibu. Kwani mwigulu alishaenda kumwona.Yaani kwa jinsi alivyoongea huyo Focus Saanane hakika siamini kama kuna mtu atajitokeza kumtetea Mbowe
Duh! Just imagine maumivu anayopitia huyu mzeeView attachment 449192
BABA WA BEN SAANANE AFUNGUKA
UPENDO MOSHA NA SAFINA SARWATT – MOSHI
SAKATA la kupotea ghafla kwa aliyekuwa msaidizi wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Bernard Saanane, limechukua sura mpya, baada ya familia yake kumjia juu mwajiri wake, Chadema, kwa kile inachodai chama hicho kimeshindwa kuonyesha dhamira ya dhati ya kumtafuta.
Akizungumza na MTANZANIA jana, baba mzazi wa Saanane, Focus Saanane, alisema anashangazwa na hatua ya Chadema kushindwa kujitokeza hadharani kumtafuta mwanae ambaye amepotea katika mazingira ya kutatanisha.
“Tangu mwanangu Ben amepotea, hatujawahi kumuona (Freeman) Mbowe ambaye ndiye mwajiri wake kama amechukua hatua yoyote ya kukutana na familia yangu, tukashauriana namna ya kumtafuta. Ukimya huu umenistajabisha mno.
“Nilitegemea angekuwa mtu wa kwanza kuja kwangu, tuone njia gani ambayo tunaweza kutumia kumpata Ben. Naumia mno ndugu yangu,” alisema Focus.
Alimtaka Mbowe ajitokeze na kuipa familia taarifa za mahali alipo Ben, kwani wao wametawaliwa na hofu kubwa kutokana na kijana wao kutoweka akiwa mikononi mwake.
“Ninamtaka Mbowe aniletee mwanangu Ben akiwa mzima, nashindwa kujua yupo wapi na nini kinaendelea mpaka sasa kati yake na Ben, haiwezekani mwajiri ashindwe kujua mfanyakazi wake alipo mpaka sasa… bado haliniingii akilini mwangu… suala hili halileti taswira nzuri kwa jamii kama anaendelea kukaa kimya na hazungumzi chochote, si haki,” alisema.
Akizungumza kwa jazba, Focus aliiomba Serikali na vyombo vyake vya dola isaidie kumtafuta Ben kwa nguvu zote kutokana na juhudi za familia kugonga mwamba.
Pia alikanusha vikali taarifa zilizozagaa kwenye mitandao ya kijamii na baadhi ya vyombo vya habari, kuwa Ben amefariki dunia. Kwamba familia yake imeitwa na Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro kwenda kutambua maiti moja iliyochomwa moto maeneo ya Uru Ongoma. Kata ya Uru Kaskazini wilayani Moshi.
CHADEMA
Akijibu malalamiko hayo, Msemaji wa Chadema, Tumaini Makene, alisema si kweli kama Mbowe ameamua kukaa kimya, bali wao wameiachia Serikali kufanya uchunguzi wa kina na kutoa taarifa.
“Wakati jambo hili linatokea, mwenyekiti wetu (Mbowe) alikuwa nje ya nchi, naelewa presha aliyonayo mzazi wa Ben katika suala hili, tunaendelea kuhangaika nalo na kutaka vyombo vya dola vichukue hatua.
“Tunaitaka Serikali ifanyie kazi mambo matatu ambayo yako ndani ya uwezo wake, iseme wapi alipo Ben, mara ya mwisho aliongea kwa simu yake na nani na wapi na itumie kila aina ya uwezo wa kumleta kwa sababu si mtuhumiwa,” alisema Makene.
RPC
Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa, aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake jana, kuwa uchunguzi uliofanywa na jeshi hilo kuhusu mwili uliookotwa eneo la Uru Ogoma, si wa Ben kama ambavyo iliripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari.
“Uchunguzi uliofanywa umebaini aliyefariki ni Steven Kimario (55), mkazi wa Sanya Juu wilayani Siha, ambaye aliuawa kwa kupigwa na wananchi wenye hasira, baada ya kukutwa akifanya jaribio la kubaka mtoto wa dada yake mwenye umri wa miaka tisa.
Binadamu watu wabaya sana, wanaweza kufanya lolote kwa ajiri ya madaraka.
Inashangaza ya kuwa unaamini kuwa amepotea. Nani asiejua kuwa ameshikwa na vikosi vya usalama chini ya amri ya serikali? Umekaa kama ni mtoto mdogo sana, nani tanzania asiejua kuwa mwanaharakati wa siasi wa upinzani anapopotea ni kuwa huwa amekamatwa na vyombo vya usalama almaarufu watu wasio julikana?Msaidizi wako anapotea unakaa kimya? Inshangza sana!